Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika hoja iliyo mbele yetu. Nitajikita zaidi kwenye mambo yanayohusu jimboni kwangu kwa sababu kuna mambo ambayo hayajakaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri na Naibu Waziri wake kwa kutuandikia speech nzuri sana. Pamoja na hayo, Wananjombe bado tuna masikitiko kwa sababu sekta hii ya mifugo, kama wengi wanavyosema, tunaiona ina potential kubwa, lakini bado ina matatizo makubwa sana na yanaji- reflect katika namna bajeti ilivyogawanywa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kabisa kwamba, ukiangalia importation ya maziwa kama moja ya main product ya sekta hii, ni kubwa mno kuliko export. Tuna-export karibu lita 280,000, hazifiki hata milioni moja, lakini tuna-import lita milioni 11.6 kwa gharama ya Shilingi bilioni 22. Ni wazi kwamba hapa kuna tatizo, aidha tija ni ndogo au hakuna uwekezaji. Kwa kesi yetu hapa, ni wazi kwamba vyote viwili vina-apply; kwamba hakuna tija kwenye uzalishaji, na hakuna uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msemaji aliyepita amejaribu kuliongea vizuri sana, nami nisingependa kurudia yale aliyoyasema, lakini niseme wazi, iko haja ya Serikali kuongeza uwekezaji katika sekta hii na katika Wizara hii ya Mifugo. Twende mbali zaidi, tuangalie kwamba mwekezaji mkubwa ni Serikali kwa kutengeneza mazingira, lakini tuangalie kwamba mwekezaji anayeweza akawa game changer ni private sector kwenye sekta hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimefarijika kuona Waziri anaongelea kwamba wanakwenda kupitia taratibu, kanuni na sheria za sekta hii. Nina matumaini kwamba zinapitiwa kwa nia ya kuondoa maeneo ambayo yana-frustrate hii sekta. Wizara inatakiwa i-facilitate, siyo i-frustrate hii sekta. Kwa hiyo, ni matumaini yangu kwamba hilo litafanyika na likifanyika nina uhakika sekta inaweza ikatoa mchango mkubwa na tukaacha kulalamika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja kwenye mambo ambayo yananitatiza. Jimbo la Njombe Mjini ni Jimbo la wakulima na wafugaji. Tumeanza kufuga kule Njombe toka miaka ya 1930 na ufugaji umekua na kumekuwa na taasisi nyingi zimesaidia ufugaji. Miaka ya karibuni kumekuwa na mdororo mkubwa sana wa eneo la ufugaji. Mwaka 2018 tulikuwa na kaya 2,190, karibu kaya 3,000; kila kaya ilikuwa na angalau ng’ombe watatu; mwaka 2022 tumeporomoka mpaka kaya 1,000. Kaya moja ina ng’ombe mmoja mpaka mmoja na nusu au wawili. Sababu kubwa kwa wakati wa miaka hii ya karibuni ni kutokana na kutokuwa na kiwanda au soko la uhakika la maziwa kwa mkoa wetu, wilaya yetu na Halmashauri yetu ya Njombe Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Njombe tuna kiwanda cha maziwa. Kiwanda kile ni moja ya viwanda ambavyo ni model nzuri sana, kwa maana ya kwamba kinamilikiwa na wafugaji, Halmashauri zetu na taasisi binafsi kama makanisa. Kiwanda hiki kimeingia katika mgogoro wa deni. Tunawashukuru TADB kwa kutaka kukikwamua kiwanda hiki na kuleta deni kubwa la karibu shilingi bilioni 1.2. Deni hilo lingeisha mwaka 2025, lakini kutokana na trend mbaya TADB waliamua kwamba ingekuwa ni vizuri pengine kufanyike re-organization.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa, napenda kusema, TADB hawajaweza kutusaidia sana kwenye ku-reorganize na ku-restructure kiwanda hiki. Napenda kusema, kumekuwa na jitihada nyingi za makusudi za kukikomboa kiwanda hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda hiki bado kina potential, ukiandika business plan inaonyesha kabisa kiwanda hiki kinaweza kikalipa deni la TADB bila matatizo yoyote. Kiwanda hiki kina asset value ya 2.6 billion lakini deni la TADB ni kama 1.6 billion. Kama kiwanda hiki TADB watachukua approach ya kusaidia kama ambavyo nia ya TADB ni kusaidia na ku-promote wakulima na wafugaji, nina uhakika tunaweza tukafikia mahali pazuri kwa sababu wazalishaji, wazaaji wakubwa wa products za kiwanda hiki ni mahoteli ambayo mengi yako Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda hiki kwa cheese pekeyake kinaweza kikazalisha kwa mwaka karibu shilingi bilioni tatu. Kwa hiyo, naona kina potential kubwa. Hakuna sababu kwa nini tusiweke focus kwenye hiki kiwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kusikitisha wenzetu wa TADB badala ya kuliangalia jambo hili kwa upana na kwa kuangalia nia kubwa ya Serikali ya kuchakata mazao ya kilimo na biashara hapa hapa nchini wameamua kuweka dalali auze hiki kiwanda. Sasa hatuna tatizo na TADB kutafuta njia za ku- recover lakini tatizo ni njia gani wanazitumia za ku-recover? Njia wanazotumia za kuweka dalali zinaenda kinyume kabisa na matakwa na dhima nzima ya kwa nini TADB iliundwa ili isaidie wafugaji na wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa na kiwanda ambacho kina matatizo unachotakiwa kufanya ni ku-reorganize na ku- restructure. Ukiweka dalali kazi yake ni moja tu. Yeye anafanya kitu kinaitwa asset stripping, anaua. Kwa hiyo, nipende kuiomba sana Serikali kwa kweli ifanye utaratibu na nimelisema hili hapa Bungeni siyo mara moja. Nimeongea na Waziri aliyepita, nimeongea na Waziri aliyepo lakini vile vile Mheshimiwa Waziri Mkuu naye nimeongea naye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba sana Waziri na ninashukuru Waziri ametoa commitment kwamba atakwenda kulishughulikia. Naomba jambo hili lishughulikiwe mwanzo mpaka mwisho lifikie mwisho ieleweke kwamba tunawakomboa wakulima ambao wao wenyewe wamejikomboa kwa kuanzisha kiwanda wakishirikiana na halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii modal ni modal nzuri, tuiendeleze badala ya kuiua kwa kutumia benki yetu ambayo kazi yake ni kuendeleza wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye mambo mawili matatu ambayo nayo yamejitokeza katika bajeti hii ambayo kwa watu wa Njombe.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Deo muda wako umeisha malizia.

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza; ni mawili tu. Sisi watu wa Njombe tumesahaulika kwenye uhimilishaji. Sisi tunasemekana kwamba kuna tatizo kubwa sana la udumavu na tungetegemea Serikali ingeipa focus Njombe kwenye masuala yote yanayosaidia maziwa kuzalishwa kwa wingi ili kutatua tatizo hilo. Kwenye majosho tuna shukuru Serikali kwa kutupa fedha ya kutosha lakini tungeomba tuongezewe angalau majosho mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa kwenye ufugaji wa samaki nipende kuomba sana vile vile tumesahaulika tuna ufugaji wa samaki karibu wafugaji 200 mabwawa karibu 300 lakini kwa vile tunaonekana ni Njombe mjini inadhaniwa kwamba hatuhitaji na hatufugi samaki. Tuombe na sisi tupate majosho na madarasa ya samaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)