Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu wa maandishi kama ifuatavyo; kwanza Benki ya Kilimo iweke kipaumbele kukopesha wafugaji hasa wadogo na wa kati.

Mheshimiwa Spika, Wizara na taasisi husika zilizo chini ya Wizara ziendelee kutenga maeneo ya kufugia na maeneo ya malisho, mifugo ni mingi kuliko rasilimali ardhi, malisho, maji, na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kupata vitalu vya kufugia katika Ranchi za Taifa usiwe mgumu kama ilivyo sasa. Wizara iweke utaratibu rafiki kwa wananchi wanaohitaji vitalu wasipate vikwazo na vikatisha tamaa.

Mheshimiwa Spika, Serikali iweke ruzuku kujenga vituo vya maziwa na viwanda, kama inavyojenga masoko, stendi za mabasi, vituo vya afya, na kadhalika; kwa nini hawajengi vituo vya maziwa na viwanda?

Mheshimiwa Spika, wafugaji wa ng'ombe wa asili wako tayari kubadilika na wao kujaribu kufuga kisasa, shida ni upatikanaji wa ng'ombe bora wa maziwa ukitaka hata ng’ombe 100 utazunguka nchi nzima hupati, Serikali iwekeze zaidi kwenye uhimilishaji na kuagiza mitamba nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ijenge masoko ya kuuzia maziwa au vituo vya kuuzia maziwa maana si salama kiafya, wauza maziwa wanapanga maziwa chini, pia Serikali inakosa mapato mengi kupitia utaratibu huu mbovu uliopo hivi sasa. Asilimia 90 ya maziwa yanayozalishwa nchini karibu lita bilioni nne kwa mwaka huuzwa katika mfumo usio rasmi na kuikosesha Serikali mapato. Tunaomba Serikali iwekeze kujenga mifumo na miundombinu ya kukusanya na kuuza maziwa mpaka vijijini kama ilivyo kwa sekta ya nyama kila kona kuna butchery.

Mheshimiwa Spika, Serikali iwekeze sana kwa vijana na wanawake ili sekta ikue na kuwa endelevu.

Pia Serikali itenge bajeti kubwa ya kuhamasisha kulima na kuhifadhi malisho na maji kwani bila kufanya hivyo wafugaji wataendelea kuhamahama kwa kufuata yalipo malisho na maji na kuendelea kuharibu mazingira. Tupeleke mashamba darasa kila kijiji kuhusu majani ya malisho ya ng’ombe kuepuka ufugaji wa kuhama hama.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.