Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiw Rais kwa kazi nzuri katika maboresho ya sekta zote.

Pili, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri kwa kipindi kifupi katika nafasi hiyo; na tatu, kumekuwepo na jitihada ya kuboresha Chuo cha Uvuvi Mikindani, Mtwara ambapo Serikali ilipeleka fedha za kujenga maabara na madarasa, bado samani ili kozi za muda mrefu ziendeshwe. Kwa sasa kuna programu ya atamizi ambayo imekuwa na manufaa sana na wanafuika wamefurahia kujifunza kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ni kuharakisha mchakato wa kukamilisha kozi ndefu kwenye Chuo cha FETA Mikindani, Mtwara.

Mheshimiwa Spika, lipo tatizo la kukamilisha mchakato wa muundo wa watumishi wa Vyuo vya FETA ambapo mpaka sasa kwa mfano Meneja wa campus ya Mikindani, Mtwara amekaimu kwa miaka 13 sasa pamoja na vyuo vingine vya Gabimori, Rorya, Kibirizi, Nyegezi Mwanza lakini pia Wakurugenzi wanakaimu na hawajatambuliwa na utumishi jambo ambalo linaondoa ari na ni kinyume na taratibu za utumishi.

Mwisho narudia kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha programu ya atamizi ya miezi mitatu kwa wahitimu mafunzo ya uvuvi ili waweze kujifunza kwa vitendo.