Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa fursa hii. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara na Katibu Mkuu, kwa kazi nzuri wanayoifanya, kweli inaonekana. Niwapongeze sana uongozi mzima wa Wizara pamoja na Mheshimiwa Rais ambaye anawasimamia.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme machache tu, mambo kama manne. La kwanza, kuna eneo zuri sana na la kimkakati la kuweza kuweka kongani au kuweka export processing zone kwenye Jimbo la Vunjo, eneo lile la mpakani na Nchi ya Kenya ambalo linaitwa Lokolova. Ni eneo ambalo limekuwa na migogoro kidogo kwa sababu ya wafugaji na wakulima wanapigana kidogo pale, lakini kuna eneo la zaidi ya eka 2,500 na Serikali tayari ina eka 140 ambazo zinaweza zikachukuliwa na zikaanza kutumiwa kwa kujenga kongani hilo.

Mheshimiwa Spika, naamini hilo litakuwa jambo la msingi kwa sababu litakuwa limefungua nchi yetu na mpaka wa Kenya pamoja na South Sudan, Djibouti na kadhalika ambapo naamini sehemu ile ilikuwa tayari pale Himo palikuwa pameibuka Soko la Kimataifa la Grain, ikawa ni reference point ya bei za mahindi na nafaka nyingine kwa nchi zote za kaskazini pale. Kwa hiyo naamini kwa vile zimepakana kuna eneo la kutosha, naamini kwamba Wizara itafikiria kuona mkakati wa kujenga kongani au export processing zone kama itawafurahisha.

Mheshimiwa Spika, kuna suala tulikuwa tunaizungumza sana la ETS. ETS naizungumza kwa sababu baadaye nitazungumza kidogo kuhusiana na uwekezaji pamoja na Business Competitiveness Index ya Tanzania. ETS sijui imekuja kuishia wapi, hatujui, sisi kama Wabunge hatujapata ripoti ambayo inaweza ikaturidhisha kwamba suala hili limekamilika na kwamba wanaviwanda wale ambao wanalipa hela nyingi sana kwa kutumia electronic tax stamps ambapo kweli ni kitu kimoja ambacho naamini hao watu watakuja kufidia gharama kwa walaji kwa kutumia hizo.

Mheshimiwa Spika, kuna suala ambalo mwenzangu, Mheshimiwa Mnzava, amelizungumzia kidogo, kuhusiana na idadi ya viwanda. Nilipoingia hapa Bungeni mwaka 2021 tulikuwa tunaambiwa kwamba viwanda vilivyotengenezwa katika mwaka ule vilikuwa ni 8,000 sijui, sasa hatujapata tena hiyo idadi. Sijui vimefika vingapi sasa hivi, lakini inaonekana kwamba pengine ile dhana ya kutaka kwamba kila mkoa au wilaya iwe na specialization fulani ya kiwanda chake ambacho Serikali itasaidia kuhimiza wawekezaji waweze kwenda kule kufanya na kupewa incentives ili waweze kuendeleza viwanda vile, sijui ile sera imeishia wapi.

Mheshimiwa Spika, niseme pia suala nyingine kwa harakaharaka kwa sababu yale ya jumla nitayasema mwishoni hapa, suala la SIDO, TEMDO na kadhalika wamekuwa wanajaribu kubuni mashine na vitendea kazi mbalimbali ambavyo vitasaidia kwenye ujasiriamali wetu; kwenye kilimo na kwenye viwanda na kadhalika, lakini nafikiri kwamba kazi ya ubunifu imekuwa ni ndefu sana, kama vile unataka ku-invent a wheel, unataka kuvumbua gari ambayo tunaona linatembea ambayo hata hayatushangazi sana sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, sasa wewe unataka kuvumbua kwa kujenga, kutengeneza mwenyewe. Nafikiri kwamba wangekita nguvu zao sana kwenye kwenda kwenye maonyesho ya bidhaa za viwanda kwenye nchi hizi ambazo wana maonyesho ya muda mrefu kama China au India wanakuwa nayo, waone vitu gani halafu tu-expose vijana wetu kwa teknolojia ambazo zipo rahisi, very simple ambazo pia zinazaa matunda kwa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pale kwenye jimbo langu kwa mfano nikiwaambia kwamba kuna mashine ya shilingi 200,000 ya kuchakata ndizi na kuweza kuzigeuza zikawa ni chipsi wanashangaa kwa sababu ni cheap, lakini pia unaweza ukatumia kwenye scales mbalimbali, scale kubwa na ndogo, lakini ukweli ni kwamba ukisema unabuni, innovation lazima tujaribu ku-leverage na ku-leapfrog kwenye vile vitu ambavyo viko sehemu nyingine.

Mheshimiwa Spika, kuna suala hili la TIC; ukienda kwenye website yao unashangaa. Mtu anasema je, kuna fursa gani ya uwekezaji Tanzania wanasema iko fursa kwenye sekta ya mining, kwenye kilimo. Lakini huwezi kujitangaza namna hiyo, kwa kusema njoo kwenye industry au kwenye mining au kilimo.

Mheshimiwa Spika, nilitarajia kwamba kwenye website ya TIC ukiingia utakuta a package of areas and projects ambazo tayari zimefanyiwa tathmini na upembuzi yakinifu, lakini hawatoi information yote wanatoa little/scant information kwamba tumefanyia uchambuzi na huu uchambuzi umefanyika na wabobezi, ma-investment bankers au wachambuzi wazuri ambao wana business analytics zao.

Mheshimiwa Spika, twende tu hata hii ya Liganga na Mchuchuma, kuna Mradi wa kimkakati wa Liganga na Mchuchuma na parameters zake ziko hivi na hivi, payback period yake itakuwa hivi, investment itakuwa hivi na faida itakuwa hivi. Kwa hiyo unakuwa ume-package hii miradi ya kimkakati kwa kuweka information ambayo wewe umeshaifanyia tathmini na upembuzi.

Mheshimiwa Spika, tatizo ni hili; hakuna mtu yuko nje ya Tanzania anayeweza akaufanya tathmini mradi mkubwa bila kutumia hela nyingi sana. Kwa hiyo inawa-put off, lakini akikuta kwamba imeshafanyika kuna basic information ambayo inaweza ikam-lead yeye kupeleka pesa inakuwa rahisi kwake kusema, okay, najua hiki, hebu ngoja nipate hiyo package, nitanunua.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo atakulipa wewe TIC, wewe Wizara uliyetengeneza hiyo feasibility study halafu atakulipa ili achukue ile package yeye mwenyewe akaiangalie, akafanye stressing testing zake halafu aseme anapeleka hela yake Tanzania kwenye Mradi wa Liganga na Mchuchuma. Hiki siyo kitu ambacho ni siri. Kama unajiuza useme unafanya siri, watu wanasema huu mchakato wa kupata wawekezaji wa Liganga na Mchuchuma inakuwa siri kabisa, huambiwi kuna nini on the table, what is on the table.

Mheshimiwa Spika, kwenye kila sekta kuna mradi wa kimkakati ambao ukifanyiwa uchambuzi halafu ukawekwa kwenye package yetu ya kujitangaza, siyo kusema hapana njoo tu kuna tourism. Tourism is not enough, sema ukija kule kuna eneo limekuwa identified unaweza uka-invest kwa kiasi hiki cha pesa na return yako itakuwa hivi. Kwa hiyo hiyo itakuwa ni rahisi sana kupata wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, ninachosema ni kwamba huwezi kuwa tu na Mheshimiwa Rais anayekimbizana, anapata pledges za miradi, watu wanasema watakuja lakini unaona kwamba hawaji, kwa nini; kwa sababu mpaka wanze sasa kutafuta information. From where?

Mheshimiwa Spika, nilifikiri kwamba kila mahali anapokwenda Mheshimiwa Rais au viongozi wetu wa juu wa Serikali wakasema kama kuna investors wanataka kuja Tanzania basi iundwe timu ya investment bankers au relationship managers ambao watakuwa moja kwa moja wanafanya direct communication na wale walioonesha nia ili wale watu waone kwamba wana contact person ambaye akitaka kumwona Rais yule jamaa yupo, atanipeleka. Kwa hiyo itakuwa ni rahisi sana kupata hawa watu, lakini tukikaa tu kimya hivi, haitakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili suala la blueprint. Blueprint ni nzuri, tumeitengeneza yetu wenyewe, tunasema tufanye hivi tutapanda, lakini mpaka tutengeneze blueprint actually tumeshuka kwenye Business Competitiveness Index. Ya mwisho ilikuwa 2019 kwa sababu baada ya UVIKO hawakufanya, lakini ukweli ni kwamba hii Business Competitiveness Index ya World Bank ina vigezo 98 lakini vinajikita kwenye maeneo 12.

Mheshimiwa Spika, tungejaribu kupitia hivyo vigezo vinavyotumika internationally ambavyo vimewekwa kama standard, tujaribu kupitia na tulinganishe na vile vyetu vya blueprint ili tuweze kukamilisha, kila mtu amepewa kazi yake, wewe fanya hivi, mwingine afanye hivi, tunamaliza tunaweza kuona kwamba nchi yetu ina-move kutoka 118 kwenye index ile, ije hata kwenye 70. Turudi kule, siyo tuendelee tu tunatengeneza blueprint, lakini tunaona kwamba bado hatujaweza ku-improve mazingira yetu ya biashara kwa maoni au kwa macho ya wawekezaji kutoka nje. Kwa hiyo naamini tukiweza kufanya hivyo tutaharakisha mambo.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naomba niseme hivi; kuna suala hili la masoko, sasa inakuwa ni vigumu kujua hata masoko yako wapi. Kwa mfano lile soko lililoanzishwa pale Stock Exchange linaitwa Tanzania Mercantile Exchange, linatoa fursa nzuri kwa wakulima wetu kujua bei gani wauze mazao yao kwa sababu vigezo viko pale, siyo hii ya kwenda mmoja mmoja kutafuta. Tujaribu kuingiza mengi kwenye stock exchange, lakini ninachosema ni hivi; mpaka sasa hivi hatujaelewa kama masoko yako kwenye Wizara hii ya Viwanda au yako kwenye Kilimo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa Kimei, sekunde 30.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)