Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi na mimi jioni ya leo hii niwe miongoni mwa wachangiaji wako. Awali ya yote, nalazimika kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kusimama leo nikiwa na nguvu ya kutosha na afya njema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru sana wananchi wa Kalambo, nuru mpya Kalambo ambayo tumeiahidi tutaitimiza na hasa kwa kasi hii kila mtu ana kila sababu ya kuunga mkono Serikali inayoongozwa na Rais, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. Kubeza ni kama namna tu ambavyo mtu ambaye ameanza safari unamwambia ongeza speed. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu najielekeza katika suala zima la bajeti ya mikoa. Nashindwa kuelewa kama hili limekuwa likitokea kwa bahati mbaya au ni katika design ambayo imewekwa. Ukipitia katika budget allocation, ukienda Mkoa wa Katavi, kupitia TAMISEMI wametengewa shilingi bilioni 3.9, unaujumlisha na Mkoa wa Lindi shilingi bilioni 6.1, unakwenda Mtwara na ya Mtwara imeongezeka hivi karibuni na sababu zinaweza zikawa zinapatikana lakini ni shilingi 10.7, ukienda Mkoa wa Rukwa ni shilingi bilioni 6.7, inawezekana pia hawakujua na Shinyanga nayo imetengewa kidogo…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Kandege, ni kitabu kipi hicho unachotumia?
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki hapa.
MWENYEKITI: Sawa, ili wote tuwe pamoja.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Ndiyo, maana ndiyo bajeti, hii nyingine ni porojo, sisi tunataka twende kwenye facts. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shinyanga imetengewa shilingi bilioni 9.2 na Singida ni shilingi bilioni 9 ukijumlisha mikoa yote hiyo na ukija ukilinganisha na hii yote na ukajumlisha Mkoa wa Manyara ambao ulikuwa sehemu ya Mkoa wa Arusha, mikoa hii miwili wametengewa jumla ya shilingi bilioni 38.3. Jumlisha pesa ya mikoa yote hiyo niliyotangulia kuitaja haifikii pesa ambayo imetengwa kwa ajili ya mikoa miwili na mikoa ambayo ilikuwa mkoa mmoja. Hili nimekuwa nikilisema, ifike mahali ambapo sasa Serikali ituelewe, haiwezekani ile mikoa ambayo tunasema iko nyuma kiuchumi ambayo haijaendelea, hiyo ndiyo ambayo iendelee kutengewa bajeti ndogo, hatuwezi kufika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya hawa ambao wanapata 27, hebu katafute kura, katafute jinsi gani ambavyo wanaitambua Serikali iliyopo madarakani kaangalie wametoa kura kiasi gani? Inawezekana kuna wataalam ambao wametangulia wako huko waka-design formula ambayo watahakikisha daima wao ndiyo wanapata pesa nyingi katika mikoa yao. Jambo hili halikubaliki! Tunaomba Serikali ituambie ni utaratibu gani ambao wanautumia katika budget allocation. Haiwezekani ambaye yuko nyuma useme ataendelea kuwa nyuma daima dumu. Hii nchi ya kwetu sote, keki kama ndogo tugawane kwa usawa.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara nyingi imekuwa ikisikika kwa wale ambao imegawanywa mikoa na Wilaya, Wilaya zingine zinafanana na kata zangu mbili, ukiwaambia kwamba na sisi tunaomba tuongezewe mgao wanasema hapana, huu ni ulaji lakini ni kwa sababu tayari wao ukubwa wa Wilaya ni sawasawa na kata zangu mbili. Mtu kama huyu ukimwambia kwamba Serikali iendelee kugatua madaraka kupeleka huko chini hawezi kuelewa kwa sababu tayari yeye alishatosheka. Naomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana, nimetoa sample tu ya hiyo mikoa na iko kwenye kitabu hiki. Wakati unakuja kuhitimisha ni vizuri ukatuambia formula gani ambayo inatumika katika kugawanya keki hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba niseme jambo ambalo limekuwa likinitia simanzi. Katika mikoa yote Tanzania, ukiachia hii ambayo ndiyo imeanza hivi juzi, Mkoa wa Rukwa ndiyo mkoa pekee kwa taarifa nilizonazo ambao hauna Chuo cha Ufundi kwa maana ya VETA. Kwa hiyo, naomba Serikali hii ili sisi tusilazimike kukimbilia huko ambako kuna vyuo, kupitia Wizara zote kwa namna mtakavyoweza kujikusanya ujenzi wa VETA Rukwa iwe miongoni mwa vipaumbele. Kwa sisi Kalambo tayari tulishatenga eneo na tunafuata ramani ili tuanze ujenzi tukiamini kwamba Serikali nayo itatuunga mkono hivi karibuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi na kwa bajeti finyu kama hii ambayo umeiona kupitia TAMISEMI hali kadhalika hatuna Hospitali ya Wilaya. Niiombe Serikali, huko ambako mlishapeleka vinatosha, sasa hivi tuelekeze nguvu maeneo ambayo tunaita peripherals ili wananchi wakienda sehemu zote za Tanzania wasijione ukiwa kwamba ukifika maeneo fulani inakuwa kama vile haupo Tanzania. Niiombe Serikali, bado hatujachelewa, naona Mheshimiwa Waziri wa Fedha yuko pale ana-take note, Mikoa yote ambayo ni under privileged ipewe kipaumbele tuhakikishe kwamba inapata allocation ya fedha ya kutosha na wananchi wako tayari kuiunga Serikali yao mkono si tena kwa hila bali kwa upendo wa dhati kutoka moyoni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niyaseme machache ili yachukuliwe kwa uzito niliotaka ufike, kimsingi naunga mkono bajeti. Ahsante sana.