Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mwaka 2022 tulipokuwa tukijadili Wizara ya Ardhi, moja kati ya mjadala mkubwa ni kwamba nchi yetu mpaka sasa haina mpango wa matumizi bora wa ardhi uliokamilika. Mwaka jana 2022 tulikuwa tunapigana hapa kuomba Tume ya Taifa ya Mipango ipate Shilingi bilioni 10 tu ili ifanye mipango tujue ardhi ya kilimo na ardhi ya wafugaji, ili tuweze kuepukana na migogoro. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu Waziri wa Kilimo ambaye hana dhamana kwenye masuala ya ardhi, ana jukumu la kugawa hekta milioni moja za ardhi ya nchi hii wakati hatuna taarifa za hali ya ardhi ikoje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku zote nasema, tuangalie kizazi kinachokuja, tusiangalie sasa. Mheshimiwa Waziri kwenye hotuba yako unasema, 2050 tutakuwa na Watanzania milioni 136 kutoka milioni 61 ya sasa hivi. Tunapozungumza sensa ya makazi, asilimia 44 ni ya watoto chini ya miaka 18; sijazungumza chini ya miaka 21, sijazungumza chini ya miaka 35. We have a very young generation. Tunagawiana ardhi. Sipingi vijana kupata ardhi, napinga concept ya Wizara kutafuta wakulima kama ambavyo tunatafuta ma-nurse na walimu. Ndiyo shida yangu kubwa na ninyi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha kwa sababu, hata hayo mashamba yenyewe, nilisoma tangazo lenu, hizo block farms bila kuwa na mwekezaji mkubwa, hii program haiwezi ku-take off; kwa mujibu wa tangazo lenu na kwa maelezo yenu. Unahitaji mwekezaji mkubwa ambaye atapewa kuanzia heka 1,000 mpaka 20,000 na vijana wetu ambao watapewa kuanzia hekta moja mpaka hekta 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasikitika kwa sababu, Waziri anasema, katika hizi hekta milioni moja atakazozigawa, wastani wa kusafisha hekta moja ni shilingi 16,800,000; kusafisha, kusawazisha udongo, kuweka miundombinu ya umwagiliaji. Hapa tuna wakulima. Hivi kweli mkulima anaweza kusafisha heka moja, kusawazisha kwa Shilingi milioni 16 na kuweka miundombinu ya umwagiliaji? Mheshimiwa Waziri anasema mpaka 2025 – 2030 wanatarijia kutumia Shilingi trilioni 16.8. Hiki ni kilimo cha iPad, hiki ni kilimo cha mjini. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza kusaidia nchi. Mheshimiwa Mama Kilango anazungumza vizuri hapa. Majimbo 188 ni ya wakulima, tena wakulima wanaolisha nchi hii ni wakulima wadogo wadogo, wanasaidia 26 percent ya GDP ya nchi hii miaka yote. Hivyo, tujiulize basi, Mheshimiwa Bashe, kama ni wakulima wadogo given the fact kwamba Tanzania ni young generation, vijana wakulima wako kule; wakike wakiume wako kule. I can assure you my friend, najua you guys are working hard, lakini lazima tushauriane. Hii Shilingi trilioni 16 mkienda mki i-pump in kwa wakulima tuliokuwanao, I can assure you GDP ita-move from 26 to 50 even to 60 percent. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sikiliza. I am very disappointed! Tusifanye kilimo cha politics, tusifanye kilicho cha kusema tunaangalia uchaguzi 2025. Tufanye kilimo kwa kuangalia the coming generation. Mheshimiwa Bashe nakuomba, hao watoto wa watu hapa umeshawakusanya, ndiyo hivyo, umeshawapa matumaini, huna namna. Ninachokisema ni hivi, hii tuitumie tu kama case study, kuwamba ngoma, ndiyo imeshapanuka hivyo, huwezi kuwakatisha tamaa, lakini kuanzia mwaka ujao wa fedha 2023/2024 tunataka utuambie ni kwa namna gani hayo mafungu mengine yaliyobaki mnaenda ku-inject kwa wakulima wadogo tuliokuwanao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ni akili ya kawaida! Nasikia Wabunge wenzangu hapa wanashukuru ruzuku, hivi unafikiri wakulima wetu wangekuwa na hela wangekuwa na njaa ya mbolea? Poor commonsense! Yaani tuko hapa, kila mtu anashukuru eti ruzuku, sijui kimeenda, kimerudi, ruzuku hiyo ni ya mbolea, for God’s sake, that is poverty! That is poverty! Kwa hiyo, tunafurahia wakulima wetu waendelee kuwa masikini halafu tunakuja kuwapa mbolea, halafu mbolea zenyewe za Wazungu tunazoagiza huko kwa billions of money. We should use our brains.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi, mmeanza hapa, mmeshaita Watoto, mmeshawakusanya huko, sawa hao wapoozeni. Mwaka ujao wa bajeti tunataka tuambiwe mnawasaidiaje wakulima wadogo wa nchi hii? Mheshimiwa Bashe, kingine, hivi mazao ya kimkakati ya nchi hii ya kutuingizia foreign currency ni vipi? Huwezi kuridhisha kila mtu my friend. Wamezungumza juzi hapa, wamesema ngano kila mwaka more than five hundred billion tunatumia; na sita nimesoma ripoti ya CAG ya ufanisi kwa miaka minne tumetumia 2.7 trillion kuagiza nje. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, parachichi, OUSB na FAO wanasema, by twenty thirty thamani ya soko la parachichi duniani ni fourteen trillion. Bashe, nchi hii ina mikoa zaidi ya nane, inalima parachichi tena inayotakiwa Ulaya huko, inayotakiwa Asia huko. Why aren’t you using common sense? This is fourteen trillion, tungeenda kuwasaidia wakulima wa parachichi, wakulima wa ngano, wakulima sijui kwenye maeneo strategic, nchi ingepata fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu ndugu yangu, we should think of the next generation. Unagawa hekta milioni moja, hivi ninyi mnajua hekta milioni moja! Hivi mnazijua, ama ni kwa sababu huko Wizarani hakuna wakulima! Kenya kwa parachichi pekee, kwa sababu Kenya ndio a leading country kwa ku-export parachichi kwa Afrika. eighty five percent ya export za parachichi zinachangiwa na wakulima wadogo wa Kenya. The remaining fifteen percent ndio wakulima wakubwa. Kwa hiyo, ni vizuri kuwa na wakulima wakubwa, lakini tusijipe utumwa wa wakulima wakubwa, tusaidie wakulima wetu, nchi itasogea. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)