Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kuchangia lakini pia nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa namna ambavyo siku kwa siku anaendelea kuongeza bajeti ya Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilitishwa sana, wakati Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Magu Mheshimiwa Kiswaga anachangia alisema maneno yafuatayo; nayanukuu alisema kwamba; “Watu wa Jimbo la Magu wamelima mpunga au mahindi na hapo katikati mvua imekatika kwa hiyo, mahindi yamekauka kwa namna yeyote ile watahitaji mahindi ya msaada mwaka ujao kwa sababu watakuwa na njaa” nanukuu alivyosema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliposikia maneno hayo nilitishika sana na kuogopa sana lile eneo ambalo Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Magu analitamka liko eneo mita 300 kutoka kwenye Ziwa Victoria narudia tena mita 300 kutokea kwenye Ziwa Victoria mahindi yamekauka na watahitaji chakula cha msaada mwaka ujao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme mita 300 ni nini? Kiwanja cha mpira kina mita 100. Mita 300 ni viwanja vitatu vya uwanja wa mpira ukiviunga kwa pamoja. Kwa hiyo, wananchi wana mashamba mita 300, mahindi yamekauka, mpunga umekauka, mwaka kesho Serikali itahitaji kuwapa chakula cha msaada au mahindi ya msaada watu wanaoishi kati ya maji yenye uwezo ambayo maji wanaweza wakatumia kwa ajili ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tukubali there is a problem that we must addresses the country lazima tukubali asiyekubali anatatizo binafsi. Sasa basi kwa kusema maneno haya nataka kusema kwamba unless tumefika kwenye agricultural revolution kwa maana ya kuhamisha kilimo chetu na kuingia kwenye kilimo cha umwagiliaji hatutafaulu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme dunia inakabiliwa na majanga mbalimbali yanayosababisha mabadiliko ya tabianchi na pia mabadiliko ya tabia za wanadamu. Kwa mtu yeyote anayejua projections za dunia, shida ya mvua, mabadiliko ya hali ya hewa yataendelea kuendelea miaka ijayo kwa wingi sana ni kitu gani ambacho kinatuzuia kuwekeza kwa nguvu nyingi sana kwenye suala la umwagiliaji kiasi kwamba tufike wakati tuhame kabisa kwenye kilimo cha kutegemea mvua tutegee umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nani atakaye kuelewa ukisema kwamba mwaka kesho Serikali inategemea kutoa chakula cha msaada kwa watu wanaolima mita 300 kutoka Ziwa Victoria wapate cha msaada? Ni kitu gani hiki kinaendelea? Ni kukosa maono ya muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme watu wanasema hivi kuna namna mbili ambayo kiongozi yeyote tukiwemo Wabunge anatakiwa kuona mambo. Namna ya kwanza a leader must see far more than others kiongozi lazima aone mbali kuliko wengine, a leader must see more than others kiongozi lazima aone zaidi ya wengine, a leader must see before others kiongozi lazima aone kabla ya wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaona tayari kwamba mwaka kesho tutahitaji chakula cha msaada kwa watu wanaoishi mita 300 kutoka kanda ya Ziwa ya Victoria na wana mashamba pale. Then what do we say? Ninaomba sana Mheshimiwa Waziri wa Kilimo rafiki yangu Bashe ushauri mamlaka tuwekeze sana kwenye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya vizuri so far so good, so far so good, lakini nilikuwa nakushauri tuwekeze sana, sana kwa sababu mabadilikoo ya hali ya hewa ukiangalia vita duniani mabadiliko ya jiografia, mabadiliko ya kisayansi yanategemewa kuwepo tena na tena. Kwa hiyo, na sisi tuone kwa mbali tuweze ku–invest kwenye umwagiliaji kwa kuwa nchi yetu na Mikoa yetu imezungukwa na maziwa ya kutosha, huo ni ushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nikuhusiana na Benki ya Mbegu za Asili. Mwaka 1980 watu walianza mchakato wa kuanza Benki ya Dunia ya Mbegu za Asili na kufikia 2008 kule Norway karibu na north pole wakakamilisha kutengeneza benki ya mbegu ya asili ambayo ina mbegu zote za chakula duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata bahati ya kuingia kwenye hiyo benki ya mbegu nikaona literature moja, nilikuwa interested kujua kwanini benki ya mbegu? Literature moja inasema benki ya mbegu kwa sababu watu wana wasiwasi yanaweza kutokea majanga duniani yakaharibu mbegu ama kwa vita ama kwa silaha za nuclear wao ni watakuwa sehemu ya kuuza na kusaidia mbegu duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya pili kwanini benki ya mbegu duniani? Wakasema ni kwa sababu wanahisi kwamba siku zijazo mbegu itakuwa ni biashara kubwa kuliko biashara zote duniani. Hili nalithibitisha kwanza mbegu tulizonazo sasa hivi nyingi ni genetic modified seed zinatoka Ulaya zamani ukipanda yale mazao unayo yavuna unayafanya kuwa mbegu ya mwaka ujao hizi mbegu genetic modified seeds ukipanda yale mazao, ukiyapanda hayawezi yakaota tena inabini ununue na ununue na ununue. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utumwa wa mbegu unakuja duniani, narudia tena utumwa wa mbegu unakuja duniani na genetic modified seeds ni nini? Ni mbegu ambazo zimetengenezwa ki–genetic zimewekewa RNA information zina taarifa ndani yake mlaji aweje? Kwa ajili ya nini? Kwa jili ya mambo yajayo waswali wanasema anaekulisha anaamua hatma yako, anaekulisha anaamua utaishi muda gani? Utakuwa na akili gani? Utakuwa na afya kiasi gani? na Taifa lako litakuwaje hapo badae? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashauri, nashauri sana Wizara ya Kilimo tuweke fedha kwenye taasisi zetu za utafiti tuwe na utafiti wa mbegu zetu za asili na tuwe na benki ya mbegu zetu za asili hapa Tanzania ili ikitokea janga lolote tutatumia mbegu zetu za asili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, ahsante sana. (Makofi)