Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nianze kwa kusema ninaunga mkono hoja. Ninampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri lakini pia ninampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuongeza fedha kwenye Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono mapema kwa sababu najua muda hautoshi; lakini nataka kutoa ushauri ambao Mheshimiwa Waziri usiutafsiri kama napinga lakini nataka kuliboresha jambo hili ili liwe na nyama nzuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naangalia kwenye takwimu mbalimbali za kidunia, nikaangalia nchi gani duniani inaongoza kwa kuuza nanasi; na nimekwenda huko kwa sababu kwetu Geita tunalima nanasi, na inauza nanasi za kiwango gani na wanunuzi wakubwa ni kina nani.

Mheshimiwa Spika, Costa Rica wanauza nanasi nje zaidi, wanauza tani 2,900,000, na kupitia nanasi wanapata 1.7 USD billion. Anayefatia pale chini ni Philippines, halafu anafuata Indonesia ambaye anauza tani milioni mbili na kitu, ambaye anafata 1.4 billion. Anakuja Philippines. Afrika nzima mtu anayeuza nanasi kwa wingi ni Nigeria, ambaye anauza 1.5 million tones; na katika hapa anapata zaidi ya dola 700,000,000.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nimechukua eneo hili, na ukiangalia sasa kwenye market share Costa Rica anauza asilimia 51 ya mananasi kwenye nchi hizo za Ulaya. Anafuatia Philippines kama nilivyosema na hao wengine. Kwa nini nimechekua takwimu hii? Tuliwahi kutoa ushauri humu Bungeni, yapo mazao ambayo si kipaumbele na hayajawahi kuwa kipaumbele lakini yana uwezo wa kutuletea mabadiliko makubwa kwenye uchumi wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, takwimu hizi ambazo ninazitoa ni takwimu ambazo kwetu sisi hakuna muujiza. Kinachowasumbua wakulima walioko Geita leo kwa nini hawauzi nanasi nje, ni kwa sababu wanalima matunda ya kula hawajasaidiwa kutafuta mbegu ambayo wanaweza ku- export. Sasa kama tunataka kuleta mapinduzi katika eneo hili, ni mfano mzauri sana Mheshimiwa Waziri ukapeleka block farming katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, nimefanya hii study nikaenda kwenye andiko moja la mtu mmoja wa Nigeria ambaye alikuwa sponsored na Rockefeller; wamegundua kwamba ili waongeze mauzo ya nanasi na mihogo nchini Nigeria na Ghana wakaingia kwenye block farming. Walichokifanya wao, cha kwanza umefanya wewe, umetafuta ardhi, thats fine; walichofanya cha pili wakatafuta credit facility, nani atakwenda kutoa credit pale, na hii ni MOU ya mkulima na yule anayeenda kutoa fedha. Utapewa fedha unayoitaka kwa MOU. Lakini la tatu huyo anayekupa credit amekuwa connected na masoko, kwa hiyo hautakuwa na tatizo na soko.

Mheshimiwa Spika, sasa sisi ambacho tungeweza kukifanya, wakulima wa nanasi, hao ambao ni kama neglected, wanalima madawa sijui ya kienyeji sijui nini, na Ulaya wanapokea nanasi zilizokaushwa sio nanasi mbichi. Sisi tunashindwa wapi hapa? Miaka michache nyuma avocado ilikuwa inalimwa nchi nzima lakini ilikuwa haiuzwi nje. Kuna mtu akaleta specie ya avocado akajua hii specie ina soko Ulaya akaenda Ulaya, leo tumeangalia kwenye takwimu Mheshimiwa Waziri, nchi inakata kata deni kutokana na mauzo ya avocado. Kwa hiyo kinachosumbua sasa ni aina ya specie ambazo ziko sokoni.

Mheshimiwa Spika, na wakulima wetu wala hawahitaji nguvu nyingi. Nimesema hapa kwamba kule Geita wako tayari, Costa Rica wanalima hekta 40,000 peke yake, wanapata 1.7 bilion USD. Kule Geita ambako mimi natoka, takribani Jimbo zima la Musukuma wanalima nanasi. Kwa hiyo you could make it a block farming halafu wewe ukapeleka credit ukapeleka mbegu inayopuzwa Ulaya, ukapeleka wanunuzi wa masoko yale, uka-transform kile kilimo kuwa kilimo cha kisasa tukapata fedha nyingi kuliko hata fedha ambazo zinapatikana kwenye pamba na mazao mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda, Mheshimiwa Waziri alinifata nilipochangia kwenye hotuba ya Waziri Mkuu, akaomba ku-share na mimi jambo hili. Sina mgogoro na block farming, shida yangu ni moja tu. Tanzania leo, amesema hapa muhamasishaji mmoja, almost 30 percent ni watu chini ya miaka 18. Ukiwapa watu leo wenye miaka 25, ukawapa hati ya miaka 60 hao wenye miaka 18 ten years to come wenye miaka 15 watakuwa na miaka 25. Kama project unataka iwe sustainable walichokifanya Nigeria wamewa- connect hawa na wale wanunuzi na wakawapa hekta mbili za mkataba. Na yule anapopewa ana-access kwenye fedha, anauza, baada ya miaka ile anayopewa kimkataba ame-graduate anakwenda kufanya kutafuta mashamba kwenye maeneo yake mengine.

Mheshimiwa Spika, sisi kwa population tuliyonayo hawa tulionao wote wakifikia huo umri wa kuhitaji kukopeshwa, kama hii ndiyo source ya ajira, na mimi nafurahi; Mheshimiwa Waziri kwa sababu unataka kutengeneza ajira 1,500,0000; market seekers wa kila mwaka wanaotafuta kazi wanaoingia kwenye kutafuta kazi kila mwaka wanafika takriban 800,000. Sasa ukianza kumilikisha ardhi kwa miaka 60 nataka nikwambie after hii miaka mitatu hautakuwa na ardhi ya kumpa mtu yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ziko nchi Jirani tunazo, ardhi nzima inamilikiwa na watu. Nahofia tunaeza kuelekea huko. Kuna nchi ambayo ukienda hata kupata heka moja hakuna, Serikali haina ardhi. Sasa mimi umeshanipa miaka 60 na kuna mtu anategemea kweli, Kanyasu atakuwa mkulima maisha yake yote, yaani mimi nina miaka 25 leo umenipa hati nilime miaka mitano, halafu niendelee kuwa mkulima hadi nifikishe miaka 50 ambayo ninayo leo, kweli? Inawezekana? Zamani mimi nilikuwa mvuvi, nimesomea uvuvi, nime-practice uvuvi miaka 10 nimeacha sasa hivi Mbunge.

Kwa hiyo, hao mliowapa miaka 15 ijayo wamejaa humu Bungeni, watakuja kuwa Wabunge. Sasa una uhakika gani kwamba una mkataba hawatabadili kazi? Mheshimiwa Waziri ni ushauri tu lakini naunga mkono. Nakushukuru sana.