Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipatia nafasi hii na mimi iwe mchangiaji kwa jioni hii ya leo. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa kunijalia afya ili niweze kusimama katika Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Spika, naomba kipekee nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa jitihada zake za kuhakikisha kwamba kilimo kinapewa msukumo kwani ni ukweli usiopingika kwamba zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania wanategemea juhudi zake katika shughuli za kilimo. Ndio maana hakukosea kwa kuhakikisha kwamba bajeti inaongezeka ili kuweza kuwakomboa Watanzania walio wengi, ambao ni zaidi ya asilimia 75.

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba niungane na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wasaidizi wake wote kwa jinsi ambavyo wanajitahidi Kwenda kufanya mapinduzi katika suala zima la kilimo, na hili sisi sote tumekuwa tukisema tunataka Pato la Taifa linachangiwa na kilimo lionekane bila kutumia tochi, lionekane kwa wazi. Kwa sababu katika kilimo pekee ndipo ambapo wabilionea wa Kitanzania wataonekana bila kupepesa macho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kupongeza maeneo hayo mimi nakusudia kuongelea eneo moja na muda ukiruhusu nitaenda maeneo mengine mawili. Nimejikita katika suala zima la mbegu na leo nimechagua mbegu aina tatu tu. Mbegu ya mahindi, mbegu ya soya na mbegu ya michikichi. Kwa nini nimechagua mbegu ya mahindi? Kilimo chetu kimepewa majina mengi, kilimo cha kufa na kupona which I don’t believe kwamba kilimo ni kufa na kupona. Inawezekana kwa sababu wakati ule ilikuwa kwamba unapolima ni kama vile either uishi au ufe, sasa, kilimo kinatakiwa kiwe ni kilimo cha kibiashara ambacho kinapaswa kiwakomboe wananchi kutoka katika wimbi la umasikini na kuwa matajiri.

Mheshimiwa Spika, ili uwe na uhakika juu ya mavuno yaliyo sahihi, kwa maana yield per acre, ni pale uinapokuwa unajihakikishia kwamba unakuwa na mbegu iliyo bora, maana ukisia mbegu iliyo bora una uhakika wa kuvuna vizuri. Kwa hiyo ukikosea katika kusia mbegu usiyo bora kwa vyovyote vile utarajie kwamba hata mavuno yake hayatakuwa na tija.

Mheshimiwa Spika, siamini kama katika nchi ya Tanzania kuna sehemu yoyote, mkoa wowote Tanzania ambao hawali ugali, hawapo. Ndiyo maana nimechagua mahindi nikiwa najua kwamba takriban Watanzania wote wanategemea chakula kinachotokana na mahindi. Ndiyo maana ninamuomba Mheshimiwa Waziri; na hii inawezekana ikawa ni kasumba, kwamba wakoloni wametuwekea mipaka na sisi tunaishi kwa hiyo mipaka ilhali hakuna kitu cha maana ambacho kinatutengnanisha. Walifanya hivyo ili waweze kututawala kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri amekiri yeye mwenyewe katika ukurasa wa 25 kipengele cha 58, kwamba tuna uhaba wa mbegu za mahindi na mbegu zingine. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba kwa sisi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, ziko nchi ambazo wanafanya vizuri katika suala zima la kuzalisha mbegu iliyo bora. Wenzetu Malawi, Zambia na Zimbabwe wanafanya vizuri sana. Sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri, hizi colonial boundaries isiwe kwamba mwananchi wa Kalambo anapoenda kununua mbegu ya mahindi ambayo ana uhakika inafanya vizuri ionekane kama vile amebeba madawa ya kulevya sio sahihi hata kidogo.

Mheshimiwa Spika, tuache wananchi hawa watu- facilitate ili wawe na uhakika na mbegu ambazo wanapata kwa sababu zinafanya vizuri kwa majirani zao. Ninaamini, kwa bahati nzuri tuna mashirikiano ya karibu sana akatika nchi hizi za Kiafrika, hakuna sababu ya kufanya sheria zikawa ngumu sana pale ambapo mwananchi anaingiza mbegu kwa ajili ya kwenda kulima, mbegu ambazo alitakiwa awe amwekuwa supplied na Serikali. Serikali wamekiri hawana uwezo kwa sasa wa kutosheleza soko la mbegu kwa mahitaji. Niweze ku- facilitate, waingize, tena kwa kusindikizwa badala ya kukimbizwa.

Mheshimiwa Spika, vile vile vimeongelea suala la mbegu za michikichi na soya kwa sababu naamini pale mabapo unasonga ugali kwa vyovyote unategemea uwe na kutoweo ambacho radha yake inakuwepo pale ambapo yametumiaka mafuta kiasi kwa mujibu ambavyo wataalamu wanatushauri; kwamba ni vizuri mafuta yakatumika japo kwa kiasi. Amesema na wenzangu wamesema nchi kama Malaysia wamefanya vizuri baada ya kuchukua mbegu ya michikichi ambayo walichukua Kigoma, wakaenda wakafanya utafiti ukaongezea kidogo, leo wanazalisha palm oil nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri, zipo jitihada ambazo zinafanyika kuhakikisha kwamba miche bora ya michikichi inapelekwa Kigoma lakini haitoshi. Mwambao wa Ziwa Tanganyika, maeneo ya Katavi, Rukwa kote michikichi inakubali, hata Mbeya, ukienda Kyela kule inafanya vizuri. Ni wakati muafaka kwa Wizara kuhakikisha kwamba mbegu zilizo bora zinatafutwa na zinapelekwa kwa wananchi kwa bei ambayo ni affordable. Hata Serikali lile tatizo ambalo inapambana nalo kwamb ainafika kipindi wanafikiri kufunga Ziwa Tanganika kutakuwa na alternative way ya wananchi wetu; kwamba, ok, tuna michikichi, tutazalisha mawese, wakati tunafunga Ziwa Tanganyika. Lakini kama hakuna maandalizi namna gani wananchi wetu wawe na kazi nyingine mbadala ya kufanya wakati mmefunga ziwa haiwezi kutuletea tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nimekuwa nikisema na leo naomba nirudie. Kuna uhakika wa soko la dunia kwa zao la soya; kwa maana ya mafuta, lakini hata soya cake ambayo inapatikana kama makapi baada ya kukamua mafuta. Hiki ni chakula kizuri sana cha mifugo. Sasa Wizara mshirikiane. Mikoa ambayo zao la soya linakubali ni pamoja na Kagera, Ruvuma, Rukwa na Katavi. Tatizo tulilonalo ni kwamba, hatuna mbegu; na wenyewe wamekiri. Wenzetu Zambia wanazalisha mbegu bora kabisa ambayo imefanyiwa majaribio mazuri na inafanya vizuri duniani. Lakini hii kama haitoshi hata Malawi wana mbegu nzuri sana. Mimi I am a living example, haya ninayoyasema siyasemi kama theory, nafanya, nalima zao la soya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninachoomba ni support ya Serikali kwa mikoa hiyo ambayo nimeitaja. Serikali ikiamua kuwekeza; na hii importation ya cheap products ambazo hatuna hata uhakika juu ya quality yake itakuwa imekwisha. Kazi nzuri imeanza lakini tunahitaji tufanye kazi kwa juhudi Zaidi. Tumechelewa, it’s our time tuhakikishe kwamba Tanzania tulishe Afrika, Afrika Mashariki na dunia kwa ujumla. Ili tuwe na uhakika na hilo, naomba kupongeza; kuna scheme ya umwagiliaji kule Legezamwendo. Lakini hebu tazama, kamoja hakatoshi. Iko potential kubwa hebu tujaribu kutizama kwa ujumla ili tuweze kusaidia Taifa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naunga mkono hoja. (Makofi)