Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Iringa ni mkoa wa kilimo hususani hata Manispaa ya Iringa. Sasa sisi hatuna eneo la kufanya block farming na Iringa Manispaa ndiyo lango la utalii Kusini na tunajengewa uwanja wa ndege ambao utaruhusu hata ndege ya mizigo kutua na kuchukua kama mboga mboga.

Mheshimiwa Waziri wewe unajua utalii ni pamoja na huduma nzuri ya chakula. Hivyo basi, rejea mazungumzo yetu, tunaomba sana sana tupewe eneo la Serikali lililokuwa la Kilimo au Utafiti Gingilanyi, katika Kata ya Nduli ili tutumie kama block farming kwa vijana wa manispaa ya Iringa, pia tunaweza tukatumia eneo lililokuwa Kituo cha Utafiti cha Kilimo kilichopo Ipogolo Kata ya Ruaha.

Mheshimiwa Spika, pia tunaeneo la umwagiliaji la Mkoga Kata ya Isakalilo. Tunaomba litengewe bajeti kwa ajili ya kuboresha ili kuwa na kilimo cha umwagiliaji na chenye tija.

Mheshimiwa Spika, tunaomba changamoto ya upatikanaji wa mbolea karibu na wakulima itatuliwe, kwanza, kwa kuweka mfumo madhubuti ambao utafanya kazi kwa wakati wote bila kukatikakatika, kuwa na wasambazaji wa kutosha mpaka vijijini hivyo kuimarisha utendaji kazi wa mawakala wadogo kwa kuondoa urasimu usio kuwa wa msingi kwa mawakala wadogo. Pia kuufanya mfumo usiruhusu QR code kuwa scanned zaidi ya mara mbili, iwe kama ilivyo kwenye voucher za simu au namba za LUKU ukiingiza mara moja haiwezi kuruhusu tena kuingiza au ku- scan. Pia zisitolewe zinazofanana kwa makampuni mawili.

Mheshimiwa Spika, mbolea hii ya ruzuku ikiwezekana iwe na limit ya mifuko itakayotolewa. Labda Serikali iseme itatoa ruzuku kwa mifuko kadhaa tu. Wale wenye mahitaji makubwa maana yake wana uwezo mkubwa hivyo waweze kununua kwa bei ya kawaida isiyokuwa na ruzuku. Wakulima wakubwa wengine huchukua mbolea ya kutosha wakulima wa Wilaya nzima hawa wanaweza. Mbolea ya ruzuku itolewe kwa mwaka mzima. Pia usajili wa wakulima kama wapo ambao bado hawajamaliza basi waendelee kutumia mpaka wamalize na usajili wa wakulima uwe ni endelevu.

Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.