Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na msaidizi wake Naibu Waziri. Wote mnafanya kazi nzuri bila kuwasahau Makatibu Wakuu wa Wizara kwa kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo yafuatayo; nikianza na Maafisa Ugani; napongeza Serikali kwa kuwapa pikipiki Maafisa Ugani waweze kuwafikia wakulima. Tatizo maafisa hawa wako Wizara ya TAMISEMI pamoja na Waziri kuwa na nia njema na kilimo, lakini hawa Maafisa Ugani hawawajibiki katika Wizara yake. Niiombe Serikali waangalie mfumo wa utawala wa Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uchimbaji wa mabwawa; kutokana na mabadiliko ya tabianchi na ukosefu wa mvua naungana na Serikali kuchimba mabwawa na kufanya kilimo cha umwagiliaji tuweze kupata mazao mengi ya chakula na biashara.

Kwa upande wa rasirimali watu; Serikali itoe kibali cha ajira kwa Wizara hii kwani kuna taasisi hakuna watumishi wa kutosha kama TFC, ni vyema Wizara ipewe kibali.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Hongereni sana.