Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya kuendeleza kilimo na kuwaletea ustawi wananchi. Pili, nimpongeze Waziri Mheshimiwa Hussein Bashe pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Anthony Mavunde, Katibu Mkuu Ndugu Gerald Mweli na Naibu wake pamoja na watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, nashauri mchango uliotolewa na Mheshimiwa Benaya Kapinga kwa kusema kuhusu utaratibu wa sasa wa kununua kahawa ufanyiwe kazi. Wakulima wanalalamika sana ikiwemo wa Wilaya ya Nyasa kutokana na kukopwa kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, shukrani kwa miradi ya umwagiliaji ya Chiulu, Lundo na Kimbande kuonekana katika mipango ya uendelezaji katika bajeti hii. Kuna mahali katika skimu za ukarabati Kimbande inasomeka kuwa katika Wilaya ya Mbinga. Ili mradi usipotee naomba Kimbande isomeke ipo Nyasa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri alinidokeza kuwa Skimu ya Lituhi imo kwenye mikakati ya bajeti hii. Nilipoenda kwenye mwenge kwa furaha kabisa nikawaeleza wananchi, wakakushukuru na kukuombea sana Mheshimiwa Waziri na pia Mheshimiwa Rais. Sasa Lituhi ambayo pia niliuliza swali humu Bungeni na ukanijibu wewe mwenyewe, imeyeyukia wapi? Nadhani imekumbana na changamoto za kiuandishi.

Mheshimiwa Spika, Nyasa ipo pembezoni, bado ni maskini lakini ina rasilimali za kuanzia kama hizi. Msimu uliopita hatukupata chochote, tunawaamini mwaka huu hamtatuacha.

Mheshimiwa Spika, namalizia kuwashukuru kwa kutuletea Engineer Faraja, yupo vizuri, akipewa nyenzo atafanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, nashauri pia bajeti yenu ishuke chini kiutekelezaji.