Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ninapenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa hai na salama. Ninapenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazozifanya katika Taifa letu hili, kwa kuzidi kuiongeza bajeti ya Wizara ya hii ya Kilimo kwa mwaka wa 2023/2024. Haya yote ni kwamba Mheshimiwa Rais anawapenda wananchi wake wa Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, pia ninapenda kumpogeza Waziri na Naibu wake, uongozi wote wa Wizara hii. Hakika maneno ya wazee wetu kwamba pumu imepata mkohozi Wizara hii imepata mtendaji hodari sana.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Wizara ya Fedha itoe pesa kwa Wizara hii ili mipango yote mizuri iliyoletwa iweze kutekelezwa kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Wizara kuimarisha masoko na huduma za masoko kwa wakulima na kuwasogezea masoko, sambamba na kuimarisha miundombinu ya kuyafikia masoko.

Mheshimiwa Spika, kuimarisha usafirishaji kutoka mashambani na kwenda katika maeneo ya masoko hasa barabara za vijijini zifanyiwe matengenezo ili ziweze kupitika kipindi chote.

Mheshimiwa Spika, ninaomba Wizara iwajengee uwezo zaidi Maafisa Ugani ili kufanya shughuli zao na kumudu majukumu yao.

Mheshimiwa Spika, Serikali iendelee kuongeza mashamba darasa ili kuwawezesha wakulima kuendelea kujifunza kupitia mashamba hayo.

Mheshimiwa Spika, pia wakulima wapatiwe ujuzi na maarifa baada ya mavuno ili waweze kutunza na kuhifadhi mazao yao wakati wakisubiri kupata soko la mazao hayo.

Mheshimiwa Spika, Serikali kuimarisha wigo wa kuongeza thamani ya mazao ili kuongeza tija kwa wakulima kwa kupata masoko ya ndani na nje.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa wananchi wengi wanazalisha mazao ya chakula, tunaomba Serikali izidi kuhamasisha wananchi wetu waweze kuzalisha mazao ya biashara ili waweze kupata kipato cha kujikimu katika maisha yao.

Mheshimiwa Spika, Serikali kuhakikisha inatafuta masoko ya kutosha kwa mazao ya wakulima ili kuepusha kupata hasara, mfano alizeti, ufuta, mbaazi na mbogamboga.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja.