Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, naongezea mchango wangu wa jana.

Mheshimiwa Spika, nianze na Kiwanda cha TANICA Kagera. Naomba Wizara kupitia Bodi ya Kahawa ilipie hisa ambazo hazijalipiwa zenye thamani ya shilingi bilioni 8.6 katika Kiwanda cha TANICA cha Mkoa wa Kagera. Pia nashauri Wizara itusaidie kutafuta wawekezaji zaidi kwenye kiwanda hicho ili kiweze kupata teknolojia mpya. Kiwanda hiki ni muhimu sana kwani kinaongeza thamani kwenye kahawa yetu, tusikiachie kife Mheshimiwa Waziri.

Pili ni Skimu za Kyamyorwa, Buhangaza na Kyota Wilaya ya Muleba; nashukuru sana, naona Tume ya Umwagiliaji imepeleka wafanyakazi Kagera na zaidi Wilaya ya Muleba. Aidha nawashukuru wamepewa vitendea kazi.

Mheshimiwa Spika, naumba sana Waziri, Skimu za Kyamyorwa, Buhangaza na Kyota, Wizara kupitia Tume ya Umwagiliaji itusaidie kukamilisha skimu hizi ambazo Serikali yetu imeweka pesa nyingi ya walipakodi lakini haina tija kwa wakulima wetu kwa sababu haijakamilika. Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri, nimechangia sana Bungeni kuhusu skimu hizi, nakuomba uzikamilishe kwa ajili ya watu wa Muleba na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Building Better Tomorrow (BBT), Muleba tuna eneo kubwa la Mwisa II zaidi ya hekta 80 ambazo ndio busket food kwa Wilaya ya Muleba na Mkoa Kagera kwa ujumla. Eneo hili linafaa sana kwa kilimo, sana mahindi, maharage na mchele. Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kupitia NARCO walipima eneo hili vitalu jambo ambalo linatishia usalama wa chakula mkoa wa Kagera. Nawaomba eneo angalau nusu yake litumike kwenye mradi wa BBT.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.