Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba unipe ruhusa ya dakika moja niwatakie kila la kheri Timu ya Wanachi kesho wanapofanya kazi kubwa ya kupeperusha bendera ya nchi katika hatua kubwa hiyo ya nusu fainali, ambayo ni hatua kubwa sana kwenye mashindano hayo ya hapa Afrika. Niwape pole wenzetu juzi walipambana kule Mtwara lakini wamekufa kiume, mashindano ndivyo yalivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumepokea hoja zote ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezitoa. Hoja ambayo inaangukia katika upande wa Wizara yetu, ya kwanza illikuwa masuala ya kikodi. Kama nilivyosema wakati tunajadili Wizara zingine za Kisekta ambazo masuala ya kikodi yalijitokeza. Nilisema kwamba tunaendelea na mchakato wa kuandaa hatua za kikodi ambazo tutazileta hapa Bungeni na masuala ya Kilimo na yenyewe yapo ambayo yatafanyiwa rejea na kuweza kuboreshwa ili kuweza kutengeneza mazingira rafiki ya kuweza kukuza kilimo chetu. Wizara ya Kisekta inahusika pamoja na sekta binafsi wanahusika katika kuandaa hatua hizo mpya za kikodi ambazo zitakuwa rafiki katika kukuza kilimo chetu.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo lilijitokeza pia suala la Benki yetu ya Maendeleo ya Kilimo, Benki yetu ya Maendeleo ya Kilimo tumezipokea hoja ikiwepo ushauri wa namna ya kutunisha mfuko huo kwa kuhusisha taasisi za kifedha za ndani ya nchi pamoja na nje ya nchi. Tumepokea ushauri huo na tutakuja na tamko la kisera tutakapoleta hotuba kuu ya Serikali mapema mwezi ujao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaahidi Waheshimiwa Wabunge Benki hii ya Kilimo ni Benki yetu na ni engine katika hatua za Mheshimiwa Rais za kuhakikisha tunakwenda kwenye kilimo cha kibiashara. Kwa hiyo tutakuja na tamko la kisera ambalo litakuwa linaendana na maono hayo ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, kwa maslahi ya muda, hoja ya tatu ambayo ilikuwa imetolewa imeongelewa na Waheshimiwa Wabunge na nimesikia Mheshimiwa Mpina akiliongelea na lilikuwa suala la fedha za maendeleo. Utaratibu wetu wa kibajeti tunaotumia hapa nchini ni cash bajeti. Tukishapata ridhaa ya Bunge hapa Bungeni tunapitishiwa makadirio ya mapato na matumizi, hatupitishiwi fedha kwamba ziko mahali hivi zianze kugawanywa kwenda kwenye kila Wizara. Tunapitishiwa makadirio ya mapato tunakwenda kukusanya na tunapitishiwa makadirio ya matumizi, tunapata ridhaa ya kwenda kutumia kwa kila miradi.

Mheshimiwa Spika, kwenye miradi ile ambayo wakati wake wa utekelezaji ni mfupi tunatumia force account. Pale kwenye force account tunatanguliza fedha tunawapatia wanaendelea kutekeleza, lakini kwenye miradi mikubwa kama ya barabara, miradi mikubwa kama ya umwagiliaji, tunachofanya tunafanya kwanza taratibu za mapitio ya taratibu za manunuzi kufuatana na bajeti iliyopitishwa. Tukishapitishiwa taratibu za kimanunuzi, mikataba inasainiwa, mikataba ikishasainiwa hatua ya kwanza ni kutekeleza taratibu za mkataba ambayo ni kulipa asilimia ya kwanza ya awali ambayo ni down payment kwa kila mradi.

Mheshimiwa Spika, baada ya hapo tunaanza kulipa certificate kufuatana na hatua za kiukaguzi wa utekelezaji wa mradi ambao umefikiwa. Hatuingii tu mkataba halafu tukampa fedha zote. Huu sio utaratibu kwamba kwa sababu bajeti ilipita ya bilioni 600 ama bilioni 300 basi baada ya kuingia mkataba tunaenda tunampatia bilioni 300. Huo utaratibu haupo na nimeshangaa sana kwa sababu aliyeongea Mheshimiwa Mpina ni Mbunge mzoefu na amekuwa kwenye Serikali. Ni Waziri mstaafu anajua kwamba tunapotekeleza mradi hata kama bajeti ilipitishwa hatuendi kumpatia yule mkandarasi fedha yote ili aanze kuchukua kutoka kwenye ghala lake.

Mheshimiwa Spika, tunamlipa down payment, tukishamaliza kumlipa down payment tunaanza kumlipa kwa certificate kufuatana na ngazi ya mradi alivyotekeleza na pale ambapo inatokea ngazi ya mradi ambayo ametekeleza haijafika asilimia 100 haina maana kwamba fedha ile imepelekwa kwenye matumizi mengine. Maana yake fedha hiyo inaenda hatua kwa hatua za utekelezaji kadri certificate inavyokuja. Hivyo hivyo hata Bwawa la Mwalimu Nyerere tunavyojenga hatuiingii mkataba wa trilioni sita halafu baada ya kuingia mkataba tukawapatia wakandarasi trilioni sita. Kwanza fedha zenyewe hizo haziko tu mahali zimerundikwa zisubiri kwamba unavyosaini mkataba umpatie yule anayetekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, miradi ya umwagiliaji ni miradi kama ya barabara na hata hii ya sasa ambayo tunatekeleza, tunatekeleza si vimiradi vya mzaha mzaha hivi, tumeamua kutekeleza miradi seriously ya umwagiliaji. Miradi hii kiwango cha chini kabisa cha muda wa utekelezaji itakuwa kwenye miezi 24 hivi. Sasa kama ni miezi 24 mkandarasi unaingiaje naye mkataba halafu uende ukampatie fedha yote ya utekelezaji wa mradi. Unampatiaje fedha ya utekelezaji wa mradi wa miezi 24, siku moja? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunatekeleza hivyo hivyo kwenye barabara, tunatoa kufuatana na certificate. Kwa jinsi Mheshimiwa Rais alivyodhamiria kwenye jambo hili la umwagiliaji, hatujakosa fedha ya kutekeleza miradi ya umwagiliaji na hii ni awamu ya kwanza na tutaendelea na awamu zingine na kwenye ile bajeti ambayo ameisoma Mheshimiwa Bashe bado tunamalizia majadiliano mengine na kuna miradi mingine mikubwa tunatarajia tuiseme wakati tunatoa tamko la kisera na tamko la bajeti tutakapoleta hapa kwa ajili ya kupata ridhaa hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wananchi pamoja na Waheshimiwa Wabunge, huu ni utaratibu wa cash budget wala hamna fedha ambayo ina ukakasi wowote kuhusu utekelezaji huu wa miradi hii ya umwagiliaji. Kinachofanyika ni taratibu za kutekeleza miradi mikubwa na miradi ya kielelezo. Tumedhamiria kwenye hii miradi ya umwagiliaji na tutaenda kwenye hiyo hatua ambayo tunaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni jambo ambalo si jema sana ile ambapo kila mtu ukikaa unawaza tu kudhania wanaotekeleza wanakosea. Halafu na wengine walishawahi kuwa na fursa pia kama Mpina hivi, haangalii hata yale ambayo yeye aliwahi kutekeleza na watu walikua wanamuongelea namna gani. Yeye kila wakati kuwaza kila Wizara inachotekeleza inakosea. Hii si sahihi, nadhani Mheshimiwa Rais tumtie moyo. Fikirieni tuna miaka 60 tangu uhuru, hivi kwenye hekta zaidi ya milioni 29, ni hekta ngapi zimeshajengewa miradi serious ya umwagiliaji. Sasa mwaka mmoja tu ambao ameanza tunakuja na criticism kibao. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa, kengele imeshagonga.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. hapa ndio gari lilishaanza kushika gia, nimwachie Mheshimiwa Waziri wa Kisekta ila aendeleeā€¦ (Makofi)