Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

Hon. Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii nami nichangie hoja ya Wizara ya Afya. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kunipatia uhai hata sasa hivi niko naendelea na shughuli hii hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Mheshimiwa Ummy Mwalimu Waziri wa Afya na Naibu wake Dkt. Molel na timu yote ya Wizara ya Afya hakika mnafanyakazi na tunawaombeeni usiku na mchana Mungu awabariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii ya Wizara ya Afya inawezeshwa na Jemedali mwenyewe Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kipaumbele kwa huduma ya afya kwenye nchi yetu hata amewezesha kujenga vituo vya afya, zahanati, hospitali kuanzia ngazi ile kule ya kaya, ngazi ya msingi hadi ya taifa kwa kweli tuna mshukuru sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa zahanati hizi na utoaji wa vifaa tiba kwenye zahanati hizi na hospitali hizi zimefanyika nchi nzima hata sisi watu wa Mkoa wa Lindi tumefaidika ni wanufaika wakubwa wa huduma hizi tunashukuru sana. Hata kule Nachingwea kumejengwa ICU nzuri na vifaa tiba vimekwenda na watalam wamekwenda ingawaje bado hawatoshelezi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma za ICU na huduma za emergency ni muhimu sana zinavyojengwa kwenye hizi Hospitali zetu za Wilaya kwa sababu jambo hili la kubadilika afya zetu inaweza ikabadilika hata wakati unatembea vizuri hivi lakini hali yako inaweza ikabadilika muda wowote lakini kunavyokuwa na hizi huduma za emegency na huduma za ICU unaweza maisha yakanusurika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan tunamshukuru sana. Lakini pia kuna huduma bobezi tumeziona kwenye wasilisho la Mheshimiwa Waziri, huduma bobezi hizi zinaboresha na zinatufanya Tanzania tuwe kitovu cha huduma hizi muhimu na pia kufanya nchi yetu iwe tuwe katika eneo lakuwa na medical tourism. Ukienda pale Ocean Road, ukienda pale Muhimbili, ukienda pale MOI, ukienda pale JKCI hakika mambo ni mazito yanayofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nijikite kwenye mafunzo, eneo hili la mafunzo naweza niaeleza sana lakini muda hautanitosha kwa sababu ni eneo ambalo limelifanyia kazi kwa zaidi ya miaka 30. Mafunzo ya Afya, mafunzo haya ya afya kwa vyuo vya kati tunaomba mafunzo hayo yaboreswe kwa sababu wahitimu hawa tunaowapata kwenye eneo hili la huduma za afya za kati, mafunzo ya afya ya kati hao ndiyo wanaenda kutumika kwenye zahanati, kwenye vitu vya afya na ndiko kule kuna mapungufu na ndiyo watu wetu wengi wako kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba katika hili miundombinu ya maeneo yale hasa kwenye vyuo vya Serikali naomba viboreshwe. Kwa mfano kuna jengo pale Nachingwea limeanzishwa lakuendelea kuboresha kile chuo ambacho mafunzo yake yalisitishwa na NACTE wakati ule ambayo sasa hivi ni NACTVET tunaomba na chuo kile kikamilishwe na jengo lile likamilishwe maana hata sasa wananchi wale wa Nachingwea na Lindi kwa ujumla tunategemea chuo kile ndiyo cha uuguzi pekee cha Serikali kwa Mkoa wa Lindi. Lakini jengo lile limesitishwa, hatujui kinachoendelea kwa kweli wananchi wale wana sintofahamu nini kinachoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika hii huduma ninafurahishwa sana leo nilivyosikia yale mafunzo ya integrated and comminated community heathy worker. Nimefurahi sana Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu alivyosema yale mafunzo yanakuja tena ni program ambayo anaileta tena ile itakuwa ni tija kubwa katika jamii yetu kwa sababu wale watakuwa kwenye ngazi ya jamii kule. Wale watashughulika hasa kwenye kutoa ushauri na huduma mbalimbali kuhusu magonjwa yasiyo ambukiza na mambo mengine ambayo yangefanya yawe makubwa zaidi mpaka yakahitajika huduma kubwa zaidi. Hili napongeza wizara, nawapongeza sana Mheshimiwa Ummy Mwalimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna huduma za mama na mtoto, huduma hizi za mama na mtoto naomba ziboreshwe mtoto wa chini ya miaka mitano, mama mjamzito bado kuna maeneo mengine Mheshimiwa Waziri bado wamama wale wanahitajika kununua vifaa kwenda kujifungua tafadhali, tafadhali ninaomba suala hili liangaliwe. Kuna maeneo mengine Tanzania kuna shida mtu anakosa hata shilingi 500 sasa mtu huyu atakapoambiwa anunue vifaa hivi, kifaa hiki, kifaa hiki ili akajifungue hiyo tena itakuwa ni shida na tutazidi kuongezea ule uzito wa tatizo la vifo vya wazazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, yote kwa yote ninawapongeza sana Mawaziri hawa na Serikali yote ya Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi wanayofanya kuboresha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)