Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi ningeanza kwa kuchangia utawala bora. Mtu mmoja aliwahi kusema, it takes a political consciousness and political will for the good governance to prevail. Utawala bora na utawala wa sheria hauanzi na bajeti, bajeti sio takwa la msingi la utawala bora. Kwa hiyo, inaanza political will kwamba tunataka tuwe na utawala bora ndiyo bajeti inakuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nazungumza haya? Toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani neno na dhana nzima ya utawala bora halionekani. Mtu mmoja pia naomba nimnukuu amesema, utawala bora ni kuongoza nchi kwa ufanisi na tija, kwa uwazi, uadilifu, uwajibikaji na ushirikishwaji wa watu kwa kufuata utawala wa sheria. Tangu Serikali hii imeingia madarakani, kuna mambo kadhaa ambayo imekanyaga huo utawala bora, halafu leo Waziri bila hata kuwa na uso wa soni anakuja kuomba hela zaidi ya shilingi bilioni mia nane hapa za utawala bora ambao haupo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na la kwanza. Serikali hii imeanza kufanya kazi kienyeji. Mawaziri wote hawa wameanza kazi bila kupata instrument, huko ni kukanyaga sheria maana yake hawa Mawaziri ni sawa na sisi Mawaziri Vivuli walikuwa wanatoa maagizo wakati hawako kwa mujibu wa sheria, huo siyo utawala bora. Aidha, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumekaa kimya, hatusemi wakati wajibu wetu ni kuinyoosha Serikali, watu wote tumekaa kinafiki.
Hata Mawaziri wengine tukiwa kwenye chai mnalaumu utaratibu huu, mkija hapa mnageuka kama vinyonga, hamsemi na wakati hii ni kazi ya Bunge. Mkibisha tutataja mmoja mmoja ambao mnapinga utawala huu kwa taratibu hizo na wengine tumewarekodi kama Rais anavyosema amerekodi, kama mnabisha tuweke hapa. Hata ninyi hamkubali halafu tukikaa humu ndani ya Bunge hamsemi na kazi ya Bunge ndiyo hiyo tumekuja hapa kusema. Tunazungumzia utawala bora, mnafanya kazi bila instrument, that is wrong and thas is not good governance, shame with you.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, toka Bunge la Tisa…
KUHUSU UTARATIBU.....
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati wa kuchangia tunakuwaga na taarifa hatuna mwongozo, nashangaa huyu ameomba mwongozo umempa, Kiti bado kinayumba tu. Naendelea kuchangia, unayumba bado, hakuna mwongozo wakati wa kuchangia, sheria ndivyo inavyosema.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba muda wangu uzingatiwe. La kwanza nililokuwa nachangia ni Serikali kuongoza bila instrument.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, toka Bunge la Tisa la Mheshimiwa Sitta na utawala uliopita pamoja na kwamba kulikuwa na upungufu lakini utawala uliopita ulijitahidi kukuza demokrasia kwa kiwango fulani, Bunge lilikuwa linaoneshwa live, tumeona wakati wa madam Spika, Wabunge tulikuwa na uhuru. Kwa Wabunge wengine ambao ni washabiki Bunge halijaanza Tanzania, tusome kidogo kutoka Ugiriki, Wagiriki walifanyaje Bunge mpaka tukafikia hatua hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge ni mkutano wa wazi wa wananchi wote. Serikali hii inaanza kuminya inaweka siri, huu siyo mkutano wa unyago, tunaongelea matumizi ya hela za Watanzania, tunahitaji Watanzania waone kila kinachojadiliwa kwa manufaa yao. Serikali inayokandamiza uwazi ni Serikali ambayo ni oga, ni Serikali inayoficha madudu. Kama mnasimama hapa mnasema mnakusanya pesa za kutosha, mmevunja rekodi, haijawahi kutokea, mmeikuta Hazina tupu, mnaficha nini tusiwaoneshe Watanzania hayo mnayoyafanya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo la pili, mnakanyaga wenyewe sheria halafu mnakuja kuomba bajeti ya utawala bora ambao hamnao. Pamoja na udhaifu wa Serikali iliyopita lakini Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alikuwa jasiri, aliruhusu humu ndani tuongee, tuikosoe Serikali kwa uwazi na hilo nampongeza bila aibu. Tulimsema, tulimkosoa na mambo mengine aliyafanyia kazi pamoja na kwamba mengine hakuyashughulikia. Leo mnakuja hapa kwa ujasiri mnasema Hapa Kazi Tu, kukosolewa hamtaki, kazi gani ambayo hamtaki kukosolewa?
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wote bila aibu wakati ule tunamkosoa Kikwete hapa mlikaa kimya, mlituzomea lakini leo mnaufyata. Inaonekana Mheshimiwa Magufuli hata akidondosha kijiko ninyi mtapiga makofi kwa sababu ya uoga wenu. Wabunge hatuwezi kuwa waoga kwa kiwango hicho, wajibu wetu ni kuisimamia na kuikosoa Serikali. Waliosoma physics sasa imegeuka kama ile pendulum swing, Serikali iliyopita alikuwa upande huu, sasa hivi tumeendelea upande huu badala ya kukaa katikati, lengo letu ni kuinyoosha Serikali, huo ndio wajibu wa Bunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, Waziri unapata wapi uhalali wa kutuletea bajeti hii wakati Serikali yako inakanyaga utawala bora wa sheria? Serikali inayoogopa uwazi ni Serikali isiyojiamini, ni Serikali ambayo inaficha uovu.
Tulitegemea demokrasia sasa inapanda ngazi kutoka pale tulipofika, kwa sababu mambo haya ni ya wazi, ni ya nchi, ni ya wananchi, tulitegemea sasa uwazi uwepo ili tukosoe, tudadisi, tuhoji kwa manufaa ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Sugu alizungumza hapa alisema numbers don‟t lie, imagine Serikali inayosema uwazi Dar es Salaam mmezidiwa, Mameya 11 lakini bado mnang‟ang‟ania, hata hiyo shule sasa imetusaidiaje kama hesabu tu inakataa, mmezidiwa, mnapiga danadana, mnakataa, huo ni uwazi gani mnaozungumza hapa?
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naikataa taarifa kwa sababu anasema uongo.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo na wewe umemwita bwege, kuna mtu kule Arusha alimwita Mheshimiwa Magufuli bwege akapelekwa Mahakamani na wewe utakwenda Mahakamani. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, mna dhana ya kusema tutumbuane majipu, ili Serikali ya Chama cha Mapinduzi ipone lazima tuwe na Bunge imara. Kama ni jipu linaanzia kwenye Bunge, Bunge hili ni jipu, limekuwa dhaifu, haliwezi kuikemea Serikali. Kuna maamuzi ya msingi na makubwa ambayo Bunge hili linayatoa na mimi kama Kamishna na Makamishna wengine hatushirikishwi, hili ni jipu, lazima tutumbuane humu ndani.
NAIBU SPIKA: Muda wako umekwisha,