Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi leo hii asubuhi na mimi niweze kuchangia katika Wizara yetu hii ya msingi kabisa na ya muhimu.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kabisa Wizara hii ni Wizara kwa kweli ambayo imebeba dhamana kubwa ya Taifa letu katika kuhakikisha usalama wa nchi yetu kimaadili, kiuchumi na kuweza kusaidia mambo mbalimbali ya Taifa hili yaweze kwenda mbele.

Mheshimiwa Spika, mimi niseme tu ninampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuwa-support Wizara hii, na amekuwa akiendela kuwapa support; nadhani ni vile kwa sababu na yeye ni mtaalamu wa maendeleo ya jamii; kiukweli angalau tunaona Wizara hii inaendelea kuonekana machoni pa Watanzania. Na pia Mheshimiwa Waziri Gwajima na Naibu wake na timu nzima yake ya uendeshaji wamekuwa wakiendela kupambana kuhakikisha angalau afua za maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii zinakuwa zinajulikana katika makundi mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mimi nitaongelea nitapenda nijikite sana kwenye masual ala NGO; na niseme tu, uwepo wa NGO katika nchi yetu umetusaidia katika meneo mbalimbali. Niseme, kwamba tunafahamu kama Taifa tunakabiliwa na changamoto mbalimbali hususani za kimaadili. Tunaona kiwamba kuna masuala ya ushoga ambayo sasa hivi ndio yana-hit, na yamekuwa yakitupa stress Watanzania wengi, kuona kwamba jambo hili ni kitu kisichokubalika, ni kitu ambacho kinatweza utu wetu na vitu kama hivyo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tumeona kuna changamoto ya dawa za kulevya, kitu ambacho kipo. Kiko underground lakini ukiweza kufuatilia wataalamu wanaoshughulika na masuala ya dawa za kulevya utagundua kwamba ni kitu kiko kikubwa lakini bado watanzania kama Watanzania hatujakipa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna biashara ya ngono. Ni kitu ambacho kimendelea kushamiri; na biashara yoyote haiwezi kushamiri kama hakuna wateja. Lakini pia kuna suala la ubakaji na ualawiti ambalo limekuwa likiendelea katika jamii yetu.Hili suala limeenda mbali, kwenye shule zetu tumekuwa tukipata tarifa mbalimbali ambazo wataalamu wa ustawi wa jamii wamekuwa wakiendelea kufuatilia na kubaini kwamba zipo shule ambazo watoto wengi wameweza kuharibiwa na wameweza kushirikishwa katika matendo haya ya ngono ambayo ni ukatili wa kijinsia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi niseme tu, na nitoe masikitikop yangu hapa, niliweza kupata taarifa kutoka kwenye shule moja inaitwa Haloli Mbozi, kwamba watoto 30 kati ya watoto wa darasa la tatu na la nne walibainika kuwa wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kingono; wengine wamelawitiwa na wengine wamebakwa. Na wale wanaobainika wamefanya matendo haya mpaka leo sijasikia kauli wamefanyiwa nini?

Mheshimiwa Spika, niseme tu, kulingana na changamoto hizi tumekuwa na NGO ambazo zinafanya kazi nzuri na zinahitaji kupongezwa. Wamekuwa wakiendelea kuwabaini na kuwatambua waathirika wa matendo haya yote ya ukatili au matendo haya ya hovyo ambayo yamekuwa yakiendelea. Wametengeneza afua ambazo wanaendelea kuwabadili kitabia na kuwasaidia kiuchumi, na hawa watu wanakuwa wanafanya wanabadilika kitabia na kuweza kusimama binafsi na kuachana na matendo ambayo yanakuwa hayana maadili mema kwa nchi yetu. Kwa taasisi hizi nazipongeza sana.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kumekuwepo na NGO ambazo Mheshimiwa Mwakyembe aliweza kuongea kwa huzuni sana. Alisema kwamba tuna NGO nyingi ambazo zimeeendelea kuwafundisha Watanzania ushiriki wa ngono za jinsia moja. Sasa, ninapata hofu kwamba kama Taifa tunakuwa na NGO ambazo zimeingia mpaka zimefika site zimefanya kazi, zimewafundisha watu ushoga na kama Taifa hatuna habari; mpaka wanakuja wanaharakati ndio wanaenda kuibua. Ninapata shaka na usalama wa nchi yetu kwamba kama hii ni ushoga tu taasisi nyingi zimeshapewa fedha na zimeshafanya kazi nzito na hakuna kilichokuwa kinaeleweka mpaka wanaharakati, ninapata hofu kubwa.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kama huu ni ushoga umefanya hivi, je, mambo mengine yanayohatarisha hali ya usalama wa nchi yetu hali ikoje? Na hii inaonesha kuna ulegevu wa ufatiliaji wa NGO hizi. Kwa hiyo nilitamani Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anakuja atuambie, baada ya kauli zile nzito za Mheshimiwa Mwakyembe kwenye lile kongamano na yule mwanaharakati ambaye alikuwepo pale, Catherine Kahabi, wamefanya nini kuhakikisha kwamba kauli zile kama zina uhalisia au hazina uhalisia, au ijoke? Kwa hiyo kwenye hili nitamtaka Mheshimiwa Waziri aje na kauli atuambie ilikuwaje na imekuwaje mpaka leo tunakuwa na miongozo ambayo inaelekeza namna ya watu kuwasiliana wanaume wa jinsia moja, yaani jinsi ya kufanya mapenzi na practical zao? kwa sababu zile tuhuma ni nzito sana kwa nchi yetu. Kwa hiyo nilitamani Mheshimia Waziri aje atuambie.

Mheshimiwa Spika, lakini kitu kingine ambacho nataka nikiongelee nataka niongelee dhamana ya maadili ya Taifa letu. Kwamba tunataka kuiacha dhamana ya maadili kwa watu ambao si watu wa Taifa letu. Yaani imagine NGO’s kutoka mataifa mengine ndio wanakuja kuanza kubadili tabia za watu wetu ama kuzitengeneza tabia za watu wetu. Kwa hiyo ninatamani kada ya ustawi wa jamii ipewe kipaumbele. Ni kada ambayo inasahaulika sana. Yaani unakuta unapoongelea maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii, Wizara imejikita kwenye masuala ya maendeleo ya jamii tu. Ustawi wa jamii hausemwi. Ukiangalia ukienda ufuatilia bajeti ya ustawi wa jamii ndani ya Wizara hii unaweza ukakuta ceiling ni ndogo sana; na nilitamani Waziri atakapokuwa anakuja mwishoni kuhitimisha atuambie kwenye ajira hizi 800 za maendeleo ya jamii zilizotangazwa ndani yake ustawi wa jamii ni ngapi?

Mheshimiwa Spika, haiwezekaniki ajira 800 kutoka Wizara moja ziwe za kada moja watu wa ustawi wa jamiii hawapewi hizo nafasi. Asilimia 95.3 ni upungufu. Yaani katika hali ya kawaida utaona kabisa kama nchi hatuna uelekeo kwenye suala la kulinda zile values za nchi yetu. Kwa hiyo kwenye hilo Waziri pia nitamtaka mwishoni atuambie ana mkakakti gani wa kuhakikisha ajira za ustawi wa jamii zinaongezwa? na ikiwezekana kama kunakuwa na sintofahamu kwenye wizara kati ya ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii ustawi wa jamii ipewe iwe institution, yaani inayojitegemea. Ikiwa idara maalumu inayojitegemea tunaamini itakuwa na uongozi wake na hata management ya masuala ya ustawi wa jamii kwa nchi hii yataenda vizuri. Tunafahamu ni kada mtambuka ustawi wa jamiii inagusa Wizara nyingi, lakini itakapokuwa kwenye idara moja ambayo inajitegemea tunaamini management yake itakuwa ni rahisi.

Mheshimiwa Spika, imagine wengine wako Wizara ya ndani, wengine wako sijui wako TAMISEMI, wengine sijui wako kwa Waziri Mkuu. Kwa hiyo niseme tu kwenye hili nitatamani kumsikia Waziri anatuambia nini kuhusu kuisimamisha kada ya ustawi wa jamii ili iweze kufanya kazi yake vizuri na kuwa na bajeti ya kutosha ili iweze…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Kengele ya pili ilishagonjwa Mheshimiwa, ahsante sana.

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo niseme ninashukuru sana kwa nafasi na naunga hoja. (Makofi)