Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara hii, pia naipongeza Serikali kwa bajeti hii, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Serikali kwa kuisaidia Wizara kuweza kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utahusu Maafisa Ustawi wa Jamii wanafanya kazi kubwa sana na wanafanya maamuzi ya kesi mbalimbali za wakubwa na Watoto, lakini hawapewi posho yoyote kwa kazi kubwa wanazofanya. Utakuta wanaamua kesi moja kuanzia asubuhi mpaka usiku. Kazi kubwa sasa wanafanya maafisa hawa.

Mheshimiwa Spika, naipongeza sana Wizara hii kwa kutoa mikopo kwa vijana na kuwezesha mikopo hiyo kurudishwa. Si jambo rahisi sana kwa wakati tulionao hongereni sana.

Mheshimiwa Spika, ombi langu ni vyema wale wanaohusika na fedha za Halmashauri wakajifunze kwa Wizara hii.

Kuhusu ongezeko la watoto watukutu mitaani naomba sana Serikali isaidie kuwatoa watoto wanaoombaomba mitaani kwani wanajifunza tabia mbaya. Ni bora waombe watu wazima lakini wasiwe na watoto wao.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja bajeti hii ipite kwa kishindo.