Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, na mimi nitatoa mchango wangu. Nitambue humbleness ya Waziri na timu yake, hamna shida na mtu, mnasikiliza. Lakini kama kawaida mimi nitashauri na tukishauri naomba msichukulie personal badala ya kujibu hoja mnafanya personal attacks, tunashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza miradi ya barabara. Mheshimiwa Waziri nilipitia randama yako ambayo imeanisha miradi mbalimbali ambayo mnataka kuitekeleza.Nimefanya uchambuzi wa miradi 69 ya barabara yenye urefu wa kilometa 11,696.88. Kiwango cha fedha ambacho kimetengwa kwa mwaka huu wa fedha kujenga barabara mlizozianisha kwa mwaka huu wa fedha ni shilingi bilioni 434.66, miradi hii 69, sizungumzii miradi yote kiujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizungumzia gharama ya ujenzi wa kilometa moja ya lami, kilometa moja ya lami ni kati ya bilioni moja ama bilioni mbili. Kwa shilingi bilioni 434 zilizotajwa inatuambia, kama gharama za ujenzi ni bilioni moja kilometa moja maana yake katika kilometa 11,699 mlizozianisha zitajengwa kilometa 434 tu kwa hii miradi 69. Kama ni bilioni mbili mbili kwa kilometa moja ambayo ndio standard ya sasa hivi zitajengwa kilometa 217.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku zote nimekuwa nikisema kwamba Wabunge tunakuwa tunaleweshwa tukiona barabara zetu zimetajwa, lakini tukienda kuangalia unaweza ukakuta, kuna hii Barabara ya Kibireshi unakuta kilometa 450 imepewa milioni tano. Sasa, bilioni tano ni kilometa mbili na nusu ama kilometa tatu. Sasa fikiria, ninazungumzia randama yenu. Kama nimekosea mtanisahihisha, lakini kibireshi imetengewa bilioni tano, na ni kilometa mbili. Sasa nawashauri wenzangu (colleagues), nendeni mkapitie randama halafu utoke ujue ulivyoambiwa umepewa kilometa 50 hela kwa mwaka umepangiwa kiasi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana Waheshimiwa Wabunge hawaishi kulalamika CAG..

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unilindie muda wangu.

MWENYEKITI: Taarifa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, atajibu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa mwache tu, mpe taarifa hiyo, Mheshimiwa Waziri.

TAARIFA

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango mzuri anaosema Mheshimiwa Halima, naomba kumpa taarifa kwamba miradi yote mikubwa ukiondoa darasa ambalo linajengwa kwa force account au zahanati miradi mingine yote inayojengwa kwanza time frame yake inazidi mwaka mmoja wa bajeti. Kwa mfano barabara ya kutoka Karatu kwenda mpaka Maswa haitarajiwi ijengwe ndani ya mwaka mmoja barabara ya kutoka Mikumi kwenda Lumecha mpaka Londo kule Songea haitarajiwi ijengwe mwaka mmoja.

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Waziri…

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: …Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Handeni, Kibireshi mpaka Singida haijengwi mwaka mmoja...

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa ananipotezea muda wangu. ulipewa dakika mbili Mheshimiwa Mwigulu utanijibu…

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: ...Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachofanyika inatolewa down payment na baada ya hapo certificate zinaanza kutolewa na kulipiwa kadri kazi inavyotekelezwa…

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa amesha kuelewa huyu. Mheshimiwa Halima.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waziri wa Fedha anaona ni value for money kwa barabara moja kwa mwaka mmoja kujengwa kilometa mbili nina mashaka. CAG katika ripoti yake amesema hivi TARURA na TANROADS, hawa hapa, wana madeni kutokana na kwanza tunakuwa na project nyingi hatuna fedha za kulipa hatulipi wakandarasi kwa wakati matokeo yake ni nini? Tunaambiwa kutokana tu na madeni haya ya bilioni 673 tumetoa riba, malipo shilingi bilioni 69. Sasa common sense bilioni 69 unajenga kilometa 69 za barabara, kama thamani ni bilioni moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa nasema, na uzuri Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mwenyekiti wangu yupo hapa, Mheshimiwa Sillo, mwaka jana 2022/2023 wakati tunatoa hotuba yetu ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa 2022/2023 tulisema masula yafuatayo; kwanza tulishauri barabara zijengwe chache zisiibuliwe mpya ili kazi ikifanyika ifanyike kwa ukamilifu wake. Tulipendekeza mapendekezo mengi sana, tukaishauri Serikali, hamsikilizi, matokeo yake ni nini? riba 70 million, can you see? Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili bandari yetu. Nitaomba nizungumze masula haya machache, la kwanza, hakuna mtu yoyote atakayepinga sekta binafsi isishirikiane na Serikali kwa uwekezaji, hayupo, kwa sababu bila sekta binafsi mambo hayaendi. Lakini muhimu ni kujiuliza sekta binafsi hii ambayo tunataka kwenda kuichukua tumejifunza tulikotoka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na TICTS for 20 years. TICTS ilikuwa ni mwiba sugu Waheshimiwa Wabunge wa mwaka 2008 wako hapa. Baada ya Serikali kuingia chaka 2008 tukaweka resolution, kwamba ikavunje mkataba, ilishindikana, TICTS imekuwa donda ndugu mpaka mkataba ulivyoisha. Ndiyo maana leo Mheshimiwa Waziri unatueleza faida ya TICTS kuanzia 2012 mpaka 2021; hujatuambia, tangu mwaka 2001, mpaka 2010, Taifa limepata nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashauri, ushauri, mtasikiliza mtaacha, tusikurupiuke, tufanye tathmini ya kina tulikosea wapi tunaendaje, tusije tukajikuta ndugu zangu makosa ya TICTS yanajirudia. Mmepewa dhamana lakini nchi hii ni ya Watanzania ninyi mnapita tu. Kwa hiyo whichever decision itakayofanyike ifanyike tathmini ya kina. Siyo tayari tunawawekezaji wetu kapuni tunakuja hapa Waheshimiwa Wabunge tunachangia hapa halafu tunashindwa kwenda kuisimamia Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hili la bandari, bandari ni usalama wa nchi, bandari ni roho ya nchi, bandari ndiyo future ya watoto wetu, tusifanye makosa, kukurupuka kwa sababu tuliamini miaka 20 iliyopita.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)