Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kutoa mchango wangu katika hoja hizi mbili ambazo zipo mbele yetu za Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Utumishi wa Umma.
Awali ya yote napenda nichukue nafasi hii, kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mungu muweza wa yote, aliyenipa nafasi kuweza kusimama na kutoa mchango wangu katika Bunge lako hili Tukufu. Naomba nianze kabisa kwanza kumpongeza sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, kwa kiwango cha hali ya juu sana.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nichukue nafasi hii kumpongeza Rais kwa masuala machache yafuatayo:-
Nitaanza kusema kwamba, nianze kumpongeza Rais kwa jinsi alivyounda hizi Wizara mbili, Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Utumishi na jinsi alivyozipanga na kuhakikisha Wizara hizi zinakuwa chini yake, nimpongeze kwa kuwachagua Mawaziri mahiri, Mheshimiwa Angellah Kairuki, na mwenzake Mheshimiwa Simbachawene. Hakika Mawaziri hawa wana weledi mkubwa, wanafanya kazi kwa uaminifu mkubwa, ni watendaji ambao ni wachapakazi na kwa kweli tuna imani nao. Ukweli umedhihirisha jinsi walivyoandaa hotuba zao, na jinsi ambavyo wameziwasilisha kwa kwelie napenda nichukue nafasi hii kuwapongeza.
Vilevile nimpongeze Rais kwa jinsi alivyoanza, kuhakikisha anapunguza na kumaliza tatizo kubwa sana sugu la mishahara hewa katika nchi yetu ya Tanzania. Ni ukweli usiopingika mara tu baada ya Rais kuchagua Wakuu wa Mikoa aliwapa siku 19 wahakikishe wanabaini watumishi hewa, lengo likiwa ni kuhakikisha fedha zilizokwenda kwenye mishahara hewa ziweze kwenda kwa wananchi.
Naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Rais, kipekee niwapongeze sana Wakuu wa Mikoa kwa kazi njema wanayoendelea kuifanya kuhakikisha wanabaini wafanyakazi wote hewa ili fedha itakayokuwepo iweze kwenda kwenye miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Rais jinsi anavyobana matumizi, katika uendeshaji wa Serikali, ni ukweli usiopingika kwanza amechagua Baraza dogo, vilevile hata yale matumizi yasiyokuwa na tija Mheshimiwa Rais ameyabana, ninaomba aendelee kufanya hivyo ili kuhakikisha fedha zile ambazo zilikuwa zinatumika katika matumizi ya kawaida ziweze kuelekezwa kwa wananchi na hasa katika masuala mazima ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Rais kwa kweli kwa utendaji wake bora, amesimamia nidhamu ya watumishi na uwajibikaji katika Serikali yake aliyoiunda. Ni ukweli usiopingika tangu ameingia madarakani wafanyakazi wote nchini wameonesha uwezo mkubwa kufanya kazi kwa kuwajibika, wanawahi kazini, wameendelea kuwa waaminifu, wanafanya kazi kufa na kupona ili kuhakikisha dhamira ya Mheshimiwa Rais inakutekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoweza kusema wale wote wanaobeza juhudi za Rais naomba Watanzania tuwapuuze kwa sababu ndiyo kawaida yao, maana kila siku wanaamka na jipya, tulipokuwa kwenye Serikali ya Awamu ya Nne walisema Serikali hii siyo sikivu, Serikali imechoka, Serikali ina watu wapole sana; amekuja Dkt. John Magufuli, ameanza kazi leo wameanza kulalamika. Naomba wananchi muwapuuze na Dkt. John Pombe Magufuli endelea kuchapa kazi, akina mama na Watanzania tuko nyuma yako na ninapenda kuwathibitishia Watanzania na Wabunge wenzangu kwamba kabla ya kuja hapa nimetembea zaidi ya Mikoa tisa wananchi wanasema kama kura zingepigwa leo ushindi wa CCM kwa nafasi ya Rais, Wabunge na Madiwani ungekuwa zaidi ya asilimia 100. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanasema, hata wale ambao hawakumchagua Mheshimiwa Magufuli, wanatamani uchaguzi ungerudiwa leo na hata wale ambao hawakumchagua wanajuta, wanasema turudie uchaguzi leo ili wampigie kura zote Dkt. John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niungane na Dkt. Rweikiza alisema ukiona kule watu wanaanza, ukiona wanafanya jambo halafu wapinzani wanapiga kelele umewabana pabaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Dkt. Magufuli endelea tuko nyuma yako na nakuomba endelea kutumbua majipu na hata yale yaliyosababisha mishahara hewa na mengine yako humu ndani na ndiyo maana mengine yalikimbia ili nchi yetu ipate tija, kwa maendeleo yetu...
MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mara baada ya kusema hayo napenda niendelee kumwomba Mheshimiwa Rais asisikilize porojo na propaganda zozote kwa sababu suala zima la mihemko huwa lina wakati wake na mihemko ina mwisho wake.
TAARIFA...
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa nimeipokea na huo ndiyo ukweli, wataisoma namba, mara baada ya uchaguzi huo sasa...
MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya utangulizi huo naomba nijielekeze kutoa mchango wangu katika maeneo machache ambayo nimeyachagua na kuyatilia mkazo kama ifuatavyo; pamoja na kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya kupeleka fedha kwa ajili ya mifuko ya wanawake na vijana asilimia kumi kwa ajili ya vijana na wanawake, na mkakati uliopo kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi, wa kupeleka shilingi milioni 50 katika kila mtaa na kila kijiji, naomba kutoa ushauri ufuatao:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kupeleka asilimi kumi ya vijana na wanawake, kwenye baadhi ya Halmashauri imekuwa ni kitendawili, bado kuna baadhi ya Halmashauri hapa nchini na Manispaa na Miji na Majiji agizo hili hawalitekelezi kikamilifu, ombi langu nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri atakaposimama hapa mbele yetu, atuambie hivi suala la kupeleka asilimia kumi kwa ajili ya vijana na wanawake ni la hiari, ni la kisheria, ni la utaratibu gani, na kama ni la kisheria ni kwa nini Halmashauri, Manispaa na Majiji hawatengi fedha kama ilivyokusudiwa na Serikali yetu? Nitapenda Mheshimiwa Waziri atakapokuwa akihitimisha hotuba yake, atuambie kama jambo hili siyo la kisheria, je, yeye kama Waziri ambaye ameaminiwa na Mheshimiwa Rais ana mkakati gani kuhakikisha, anaileta hii sheria hapa Bungeni ili tuweze kutunga hiyo sheria itakazozibana Halmashauri, Majiji na Miji ambayo hawatengi asilimia kumi ya vijana na wanawake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu wanawake wa vijijini, wanawake wa mijini, wanavikundi vya VICOBA, wanavikundi vya ujasiriamali, wana SACCOS lakini Halmashauri zetu na Miji yetu bado wanafanya mzaha katika kupeleka fedha zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali, katika ule mkakati wa kutekeleza Ilani ya CCM ya kupeleka shilingi milioni 50 kila kijiji na shilingi milioni 50 kila mtaa, naomba kabla ya Bunge hili halijaisha tunataka kuona fedha hizo, nataka tuone fedha hizo hata kama zinapitia kwenye Serikali za Mitaa, hata kama zitapitia Benki ya Wanawake, hata kama zitapitia Benki ya NMB, hata kama zitapitia kwa Wizara yenyewe ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, hata kama zitapitia kwenye Mfuko wa Vijana, tunaomba fedha hizi, kabla ya Bunge hili halijafungwa, Waziri wa Fedha aje hapa mbele yetu atuambie fedha hizi ziko wapi, tuziangalie katika kitabu hiki ziko wapi, na zianze kupelekwa vijijini kama ambavyo zimekusudiwa ili wanawake na vijana wa Tanzania waweze kunufaika na mpango huu wa Chama cha Mapinduzi kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimedhamiria kuwaondoa katika umaskini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijielekeze katika masuala mazima ya maslahi ya wafanyakazi. Wafanyakazi wa Tanzania, wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana ya utendaji kazi katika nchi yetu, hata haya matunda tunayoyaona mazuri ya utekelezaji wa ilani ya CCM, wafanyakazi wa Tanzania wana mchango mkubwa. Ombi langu katika kupeleka mishahara ya wafanyakazi, ile Bodi ya Tume ya Mishahara iangalie uwiano, tusipishane sana, unakuta Mbunge anapata mara mbili, unakuta kiongozi wa shirika anapata mara tatu, lakini huyu karani, huyu dereva, huyu askari polisi, huyu nesi, huyu daktari, tufanye uwiano ili mishahara na hao wafanyakazi wa kawaida wanaofanya kazi zilizo sawa, waweze kutendewa haki maana kwa kweli ndiyo tegemeo letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la wafanyakazi, kuna nyumba za wafanyakazi, kuna maslahi yao na hasa wanaoishi vijijini walimu wetu, manesi, madaktari, askariā€¦
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja, mengine nitayaleta kwa maandishi, ahsante sana.