Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo Kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Kumi na Mkutano wa Kumi na Moja pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Nane na Mkutano wa Tisa

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo Kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Kumi na Mkutano wa Kumi na Moja pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Nane na Mkutano wa Tisa

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi hii. Nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani ambayo ameendelea kunipa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Naungana kabisa na maoni mazuri ya Kamati ambayo yametolewa na sisi tumeyapokea na tunaendelea kuyafanyia kazi. Nitumie nafasi hii kusema kwamba majukumu ya Bunge kwa mujibu wa Katiba yetu Ibara ya 62, 63 na 64 ni pamoja na kuisimamia Serikali, kupitisha bajeti na kutunga sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaposema kutunga sheria ni majukumu ya Bunge, ndani yake ni pamoja na kurekebisha sheria mbalimbali. Hivyo, sheria zinavyopita hapa kuja kutungwa, kurekebishwa ndiyo majukumu ya msingi ya Bunge letu. Nalishukuru sana Bunge letu kuwa na Kamati maalumu ya Sheria Ndogo. Kamati hii maalum ya Sheria Ndogo ni muhimu sana, inatupa maoni mengi mazuri ya kuboresha ya sheria mbalimbali. Kwa hiyo, nilitaka tu kwanza tukumbushane kwamba suala la kutunga sheria ni na kurekebisha sheria ni majukumu ya msingi hivyo. Hivyo, sheria imnaweza ikaja hapa kufuta sheria ya nyuma, kurekebisha, kuongeza na kuboresha. Ndiyo majukumu ya msingi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea maoni mbalimbali na hivi sasa tunakwenda kuboresha Sheria ya Tume yetu ya Kurekebisha Sheria. Tunakwenda kurekebisha sheria hii, tunataka sheria zote za Bunge zinazotungwa, kabla ya kutungwa tupitishe Tume ya Kurekebisha Sheria (Law Reform Commission). Lengo la kupitisha, ni kwamba zifanyiwe tafiti kuona kama sheria hii inafaa, ipo kwa muda muafaka na kama itasaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, maoni haya yanatokana na Kamati zetu ikiwa ni pamoja na Kamati ya Sheria Ndogo. Tunaposema tuziangalie hizi sheria vizuri, kwa hiyo, tunakuja na maboresho, na huu ni mwanzo. Maoni mengi mazuri yametolewa, tutaendelea kuboresha. Kwa hiyo, lazima sheria iendane na Katiba, lazima tufanye tafiti. Tumesema sasa sheria hizi wakati wa marekebisho lazima zipitiwe na tume yetu ya kurekebisha sheria, kufanya uchambuzi na tafiti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kuunga mkono hoja na kuendelea kukumbushana kwamba jukumu la Bunge ni kutunga sheria na kurekebisha. Pia tuzazo halmashauri zetu ambao pia wanalo jukumu la kutunga sheria ndogo kutokana na eneo lenyewe. Kama eneo lina changamoto ya kipindupindu basi watu wasitupe taka hovyo. Kama kuna changamoto ya masuala mbalimbali, nakumbuka wakati wa Covid nchi nyingine walisema lock down lakini sisi tulisema tunafanya kazi. Kwa hiyo, badala ya lock down wengine wanasema basi kutembea iwe mwisho saa fulani ili kudhibiti masuala ya magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Covid.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na kuipongeza sana Kamati ya Sheria Ndogo ambayo inafanya kazi nzuri na maoni mliyotoa tutayachukua na kwenda kuyafanyia kazi tukianza na marekebisho ya Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria. Zitapitiwa, zitafanyiwa uchambuzi, zikija huku zinaendelea kuwa vizuri na zitapita katika Kamati zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)