Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanya kazi kubwa sana ya kuliongoza Taifa letu. Napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri pamoja na Makatibu Wakuu wote kwa utendaji uliotukuka katika sekta ya ardhi, Mungu awabariki sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajikita katika maeneo yafuatayo nikianza na urasimishaji; kwa kweli Mkoa wa Dar es Salaam tulipokea vizuri sana, lakini tuliingiliwa na watu ambao hawana maadili, wakavuruga na wakachukua fedha za watu na hati hazijatolewa mpaka leo hii. Wananchi hawajui hatma yao. Tunaomba Serikali itoe maelekezo jinsi watakavyofanya usuluhishi wa jambo hilo tuweze kwenda mbele.

Pili ni kuhusu ujenzi wa makazi ya gharama nafuu; naomba Serikali iangalie jinsi ya kujenga nyumba za gharama nafuu zisiwe na bei kubwa. Gharama kubwa za nyumba zinazosababisha nyumba hizo kuishi wenye fedha badala kuishi wananchi wenye kipato kidogo na kipato cha kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kodi ya ardhi; wananchi wengi wamekuwa na madeni makubwa ya kodi ya ardhi ni vyema Serikali ikafanya mahesabu ya madeni wakaangalia wastani wa makusanyo yao kama ni machache kuliko madeni Serikali iweke punguzo la kodi kwa kipindi cha mpito wananchi wengi waweze kulipa kodi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja.