Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Bismillah Rahman Raheem, Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, muumba mbingu na ardhi, aliyenijalia mimi na sote tuliomo humu ndani uzima na tukawa hapa leo, kwa matashi yake tu na siyo kwa ujanja wa yeyote katika sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nishiriki kidogo kuchangia katika mada ambazo ziko mbele yetu hapa. Nianze kwa nasaha, nafanya hivi kwa sababu kuna wenzangu kadhaa walipokuwa wakichangia wameonesha kama kukata tamaa; kwamba tunasema tu Mheshimiwa Mtolea mpaka akasema it is boring kusema hilo hilo, kweli wana falsafa wengi tu wanatuambia, kufanya jambo lile lile kwa namna ile ile, ukatarajia mambo tofauti kuna tatizo. Lakini mkubwa zaidi kwenye falsafa Mwenyezi Mungu, pia naye anaonya kuhusu hilo, kwa kemeo kubwa kabisa kwamba hao anawaita ni wale ambao wana mioyo hawaelewi kwa mioyo, wana masikio hawasikii kwa masikio hayo, wana macho hawaoni kwa macho hayo, na hilo ndio Mwenyezi Mungu anasema ni dalili na ndiyo njia ya kuangamiza jamii, hebu tusiende huko. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa na kwa nini tunaendelea kusema, tunaendelea kusema kwa sababu Mwenyezi Mungu huyo huyo, ametuambia kumbusha. Hakika ukumbusho huwafaa wenye kuamini na mimi naamini sote humu ndani tunaamini, kwa itikadi zetu tofauti, kwa sababu tulishika kitabu cha Mwenyezi Mungu, kwa kila mtu kwa imani yake, tukiamini na tukiahidi kwa yule, nguvu hiyo ya juu, kwamba atusaidie kuendesha nchi hii kwa uadilifu na kwa maslahi ya sisi tuliopo na mustakabali wa vizazi vijavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nianze pia kwa kusema kwamba katika mambo ambayo hayapendezi ni kufanya haya mambo as formality, budgeting is a very serious process activity kwenye nchi jamani, kupanga ni kuchagua. Sasa tunafanya bajeti gani hapa ya kuigiza igiza tu, tunapitisha pitisha tu, hata tukisema hili halijakaa sawa twende tu, amesema mdogo wangu Sophia pale, tunakwenda kwa mambo ya kiitikadi za vyama, vyama tutaviacha hapa, siku ya siku utaulizwa wewe na kile kitabu ulichokishika pale na siyo chama chako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi siyo halisia humu, kuna takwimu zinatajwa, kuna maelezo yanatolewa yale maelezo tumekuwa tukiyasema, tukiyasoma, tukiyasikia siku zote hakuna kilichobadilika. Kwa nini tuwe ni jamii ya kwenda kwa kauli mbiu na misamiati, mara kasi mpya, mara kasi zaidi, mara hapa kazi tu, tuko pale pale, tubadilike ndugu zangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme elimu inasemwa hapa, elimu bure kila mtu anapiga makofi, kwenye Jimbo langu la Mafia nilipokuwa natembelea shule kadhaa zote zipo kwenye hali taabani. Mwalimu mmoja akaniambia Mheshimiwa sasa tunarudishwa analogue, ametumia term hiyo, akasema sasa kwa hii mnayotuambia elimu bure mmeturudisha analogue, hatuwezi tena kuchapa hata karatasi tuza mtihani wa mwisho wa mwaka. Ule uwezo mmetunyanganya, mmetuletea wanafuzi hatuna mahali pa kuwaweka, walimu wenyewe hatuna mahali pa kukaa, tunasema elimu bure, watu wamependa hawakupenda wafanye nini, hebu tuseme na mioyo yetu katika haya tunayoyafanya. Tusishangilie namba tu, quantity haina maana yoyote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia nilipokuwa na shule moja ya sekondari sikupata division one, sasa hivi kuna shule sita hakuna division one. Tofauti kati ya watoto 39 na watoto 400 haipo, kwa nini tunashangilia hii namba isiyokuwa na maana? Hebu tuende kwenye quality, tusisingizie tu kwamba mbambo yamekaa sawa, mambo hayajakaa sawa na kuna mengi wengine wamesema kuhusu elimu, matatizo yaliyopo, wala sina haja ya kuyarudia kwa sababu muda wenyewe haupo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu afya, Serikali ya Wilaya ya Mafia ndiyo zahanati ya kijiji cha Kilindoni, na ndiyo kituo cha afya cha kata ya Kilindoni. Maabara yake kwa wakaguzi wa Wizara ya Afya haifai ilikuwa ifungwe, Maabara ya Wilaya ya Mafia, hospitali yake kwa vigezo vya wakaguzi kutoka Wizarani Serikalini kwamba ile ni unqualified kabisa ifungwe. Lakini tunaifunga? Tunao madaktari? Hatuna x-ray sasa hivi, hatuna ultra-sound. Kibinadamu tunasema tulimpoteza mtu kwa sababu hiyo tu. Alipata ajali ya kugongwa na pikipiki, ikashindikana kumfanyia x-ray, usafiri Mafia hakuna, ndege hizo tunazosifia na airport sijui ni wale private wanaleta watalii wao basi, mpaka alipopata ndege siku ya pili amekata roho kabla hata hajafika Kilwa kwa sababu ndege ilikuwa inapita Kilwa kabla ya kuja Dar es Salaam. It is a Coastal Air wanapeleka watalii wao kwanza, kabla ya kutoa huduma kwa Watanzania. Jamani hii ndio hali ambayo tunakwenda nayo, tunashangilia humu, haifai. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwahi kusema wakati fulani, kuna zahanati ambayo inafanya kazi ya kituo cha afya, mbaya zaidi anayetusaidia pale ni Medical Attendant, is not even a Medical Officer, au ni nurse not even a nurse, a Medical Attendant. Halafu mwenyewe huyo anamuona mgonjwa, akimaliza ile karatasi yake pale anaenda kumpima maabara, akishamaliza yeye anasoma yale matokeo aliyoyapima, halafu yeye anamuandikia dawa huyu, nimesema hapa miezi miwili iliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni nchi gani, hii ni Serikali gani isiyokuwa na huruma na watu. Hapa halafu tunazungumzia utawala bora, utawala bora gani ambao una watumishi ambao ni very insensitive, ina watumishi na watendaji na viongozi ambao wanagawa jamii kimaeneo. Sisi watu wa pembezoni tutaendelea kuwa wa pembezoni, inagawa watu kijinsi wanawake waendelee kufa tu kwa sababu afterall ni 400 tu, kiitikadi na kidini, kwa nini tunakuwa na nchi ya namna hii, utawala gani huu usiofuata sheria, usiojali haki za binadamu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mashekhe limesemwa siyo leo, siyo jana, wala siyo juzi, kosa lao nini, hatuambiwi. Sijui kama nitauruhusu mshahara wa mdogo wangu kaa vizuri tu, tutaelezana vizuri. Tunaambiwa kuna memorandum of understanding, waislam wamelalamika jamani wamepewa upande mmoja tu, sisi hatuna hatupewi majibu, tunafanyiwa kejeli. Waislam walilalamika pia kuhusu NECTA, kwamba hawakuwa na imani na Mtendaji Mkuu pale, ikaundwa Kamati kufanya uchunguzi, hatukuambiwa matokeo yake lakini mtu huyo huyo amekwenda nafasi ya juu zaidi na mbaya katika eneo lile la elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnataka waislam wasimame wapi, waielewe vipi Serikali hii, sipendi kuzungumza maneno yanayoonesha division, lakini is a very serious thing, ukiwa na Serikali ambayo ni very sensitive, ukiwa na watendaji ambao in very sensitive, hiyo tunajichimbia shimo jamani, tutaangamia na binadamu akifikishwa pahala ambako he has got nothing to lose ila roho yake wala haoni hata hiyo thamani ya roho. Roho ina thamani kama itaishi maisha ambayo ni quality, lakini roho ambayo inaishi maisha ya kubangaiza, maji hajui, kula yake hajui, vaa haijui, nyumba anayokaa haielewi hayo siyo maisha ndugu zangu tutumie budgeting process seriously, tupange mambo kwa ajili ya jamii yetu, tuweke vitu vyenye kueleweka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa muache Mafia kuendelea kuifanya sehemu ya pembezoni, hivi kweli mnanipangia DAS Office budget ya usafiri in country laki nne. Tumelia mara ngapi jamani msitumie kigezo cha watu tu, tumieni geographical factors pia. Kumsafirisha mtumishi kutoka Mafia afike headquarter ya Mkoa wa Kibaha, ni ghali kuliko kumsafirisha mtumishi kutoka Kinondoni akaenda Morogoro, sasa nawaambia kama mnaona laki nne zenu ni nyingi sana, au kama watumishi wa Mafia hawaitaji maslahi mazuri, pesa yenu bakini nayo, nitatoa pesa mara nane yake, hiyo mliyopanga ninyi nitatoa quarterly kwa ajili ya kuiwezesha Halmashauri yangu ifanye kazi, hata hili jamani hebu tuhurumieni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi mahsusi ambayo ningeweza kuyachangia lakini nina wasiwasi sana na suala la muda. Watumishi sasa hivi sijui hii by-law imetoka wapi, kwa nini hii TAMISEMI Head Office isiwe ndiyo mwajiriwa wale watumishi, walimu, watumishi wa afya na wengine, badala ya kuiweka Halmashauri ambazo baadae zinanyanyasa watu. Mwalimu amekaa kituoni miaka kumi, anaambiwa huondoki mpaka ulete mbadala, yaani mwajiriwa akatafute mwajiriwa mwenzie akamlete Mafia, kama yeye anapaogopa yule mwingine atakujaje? Hebu jamani tuwe na utaratibu.
MWENYEKITI: Mheshimiwa muda wako umekwisha.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru, ahsante sana.