Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa heshima na kutoa mchango wangu mdogo katika Wizara yetu hii muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mwanadiplomasia Namba Moja ambae ni Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan. Uimara wa Wizara hii ya Mambo ya Nje, chini ya Dada yangu na Kiongozi wetu Mheshimiwa Dkt. Stergomena Tax pamoja na Naibu wake, kwa kiwango kikubwa mafanikio na kukimbia kwa kasi kubwa sana katika diplomasia ya uchumi hatuwezi kutaja mafanikio haya na kumuacha Mheshimiwa Waziri wetu wa Mambo ya Nje, Dkt. Stergomena Tax na Naibu wake. Hongereni sana viongozi wetu wazalendo mnampa Rais wetu heshima Kubwa, mnalipa Taifa letu heshima kubwa sana katika masuala mazima ya diplomasia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme mambo yafuatayo; Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania ndiyo roho ya mambo yote yanayohusiana na maendeleo ya uchumi ya Taifa la Tanzania. Wizara ya Mambo ya Nje inajihusisha na mambo makubwa yafuatayo ambayo baadhi ya Wabunge wameyasema. Hauwezi kuzungumzia suala la uwekezaji kwenye nchi yetu ya Tanzania bila kuigusa Wizara ya Mambo ya Nje, hauwezi kuzungumzia masuala ya utafutaji wa masoko bila kugusia Wizara ya Mambo Nje, hauwezi kuzungumzia Mambo ya Grants and loans bila kuzungumzia Wizara ya Mambo ya Nje, hauwezi kuzungumzia habari ya kuwavuta watalii kutoka katika pande zote za dunia bila kuzungumzia Wizara ya Mambo ya Nje, hauwezi kuzungumzia mafanikio ya mikutano mikubwa ya Kitaifa na Kimataifa ambayo Viongozi wote wa Kidiplomasia wa nchi wanahudhuria bila kuigusia Wizara ya Mambo ya Nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimkakati (Strategically) Wizara ya Mambo ya Nje tukiamua kuiweka kuwa Wizara ya Kimkakati ndiyo roho ya kufanya transformation ya uchumi na uwekezaji katika Taifa letu. Nimeyasema hayo kwa sababu tumekuwa tukiichukulia Wizara ya Mambo ya Nje kama Wizara tu ya watu kwenda kwenye mikutano. Nataka nikwambie, ninatoa rai kwa Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ni Wizara inahitaji kupewa fedha za bajeti kubwa ya kwanza kwenye Taifa hili ni Wizara ya Mambo ya Nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano mdogo, hapa tunaposema tumejenga, tumejenga barabara kubwa, tukisema tunapanua bandari, juzi tumezungumza jambo la bandari hapa, ni nani walifanya juhudi kuhakikisha kwamba wawekezaji hawa wanapatikana ni Wizara ya Mambo ya Nje. Kitu cha ajabu inapofika kwenye kuzindua miradi hii hawa watu hata hakuna mtu anayejali wala kujua kwamba kazi kubwa ya kizalendo imefanywa na Wizara ya Mambo ya Nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuambie strategically as a nation kama tunataka kufanya transformation ya kiuchumi, transformation ya uwekezaji, transformation ya kukuza diplomasia ni sharti Serikali tubadilishe mindset watu hawa wapewe fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ninapozungumza ni nani anaetafuta masoko ya parachichi za Tanzania ni Mambo ya Nje. Nani anamsaidia Mheshimiwa Mwigulu kwenda kutafuta mikopo? Mambo ya nje. Halafu, nenda ukaangalie bajeti yao utaona kama nchi bado hatujadhamiria kulibadilisha Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa wito Serikali kama tutakuwa tumechelewa mwaka huu na tunae Mwanadiplomasia Mama Tax, Kiongozi mtulivu na mwenye uwezo mkubwa sana, yeye na Naibu wake, kama tutakuwa tumechelewa mwaka huu tujipange mwaka unaofuata tudhamirie kuleta transformation ya kiuchumi tuweze ku–empower Wizara yetu ya Mambo ya Nje ili FDI zije za kutosha Taifa letu liweze kupiga hatua ili changamoto za ajira alizozisema Daktari na watu wengine ziweze kumalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka nizungumzia Zanzibar leo.

MWENYEKITI: Malizia nusu dakika.

MHE ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba nimalize tu Zanzibar. Zanzibar hawana Wizara ya Mambo ya Nje, hili naomba niliseme na univumilie kidogo sana. Zanzibar hawana Wizara ya Mambo ya Nje, wanategemea Wizara yetu hii ya Mambo ya Nje kuweza kuwasaidia watu wetu wa Zanzibar katika kuleta FDI katika kuleta utalii na masuala mazima ya uwekezaji katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Wizara ya Mambo ya Nje, chochote mnachokifanya Mambunge mengine yatakuja tutawahoji ni uwekezaji kiasi gani umekwenda kwa wenzetu wa Zanzibar ambao ni partner iko kabisa katika Muungano huu tulionao wa Tanzania. Wazanzibari wanatakiwa wasaidiwe sana kwa sababu wao hawana Wizara inayojitegemea nje ya hii. Mheshimiwa Waziri tunaimani na wewe tunakuomba, Rais Mwinyi anafanya kazi kubwa na nitaoa rai Rais Mwinyi apatiwe utulivu Zanzibar, aendelee kuijenga Zanzibar. Choko choko ziachwe Zanzibar ili Rais Mwinyi kwa uwekezaji huu ninaouzungumza aweze kufanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwishop lakini siyo kwa umuhimu ninaunga mkono hoja.