Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsnate sana. Awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia kwa uongozi wake madhubuti katika nchi yetu ambao umeendelea ku-push maendeleo makubwa katika Taifa letu. Jambo ambalo kila mmoja wetu anashuhudia kila sehemu ya nchi yetu maendeleo yapo na ikijumuisha Jimbo letu la Serengeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri ndugu yetu Mchengerwa, nimesikia habari zako nimeona wakati ukiwa Wizara ile ya Utamaduni na kwa kipekee kabisa nimewahi kuleta kwako habari za kujenga kwa haraka barabara ile ya lami ya kutoka Tarime mpaka Mugumu, kutoka kule makutano mpaka Mugumu kwa ajili ya kuboresha utalii kufikika kwa Serengeti na nimeona jinsi ambavyo umepambana kusaidia na ku–push barabara ile. Kwa hiyo, nakupongeza nimeona kazi yako ni kubwa ni nzuri na nikueleze watanzania tunayo matarajio makaubwa sana juu ya mabadiliko katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wizara hii ni ya kibiashara, Watanzania tunahitaji fedha nyingi ili tuboreshe nchi yetu kwa hiyo utaenda kutusaidia kuhakikisha nchi sasa inapata fedha nyingikupitia Wizara hii. Tunampongeza pia Naibu wako Mheshimiwa Mary Masanja toka ameingia tumeshirikiana naye sana kila wakati kutatua changamoto mbalimbali kule na amekuwa mstari wa mbele sana katika ku–push ujenzi wa uwanja wa ndege katika Mji wa Mugumu kule Serengeti. Kwa hiyo tunakupongeza sana Naibu Waziri endelea kuchapa kazi pamoja na Waziri wako tuko pamoja na ninyi. Nampongeza pia Dkt. Abas, Katibu Mkuu kwa utendaji mzuri, Naibu Katibu Mkuu Bwana Anderson, Kamishna wa TANAPA ndugu yetu William Mwakilema, Mkuu wa hifadhi ya Serengeti ndugu Msindai wanafanya kazi kubwa nzuri kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Ilani yetu ya Uchaguzi 2025, tulibainisha kuwa tunahitaji kukuza kiwango cha watalii wanaokuja nchini waongezeke mpaka kufikia milioni tano. Ndipo sasa kwa muktadha huu ninayo mambo machache ya kuchangia kwa ajili ya kuona namna gani tunaweza tukafikia hili pamoja na kuboresha uhifadhi. Moja, niombe sana Serikali iende kuhakikisha inaongeza fedha katika utangazaji wa vivutio vyetu na hapa nishauri kabisa ni vyema tuone kuweka mfuko maalum kwa ajili ya promotion ya tourism sites au tourism attractions katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona Mheshimiwa Rais alikuja na ubunifu mzuri kabisa wa ile filamu ya Royal Tour baada ya pale hatujaona ubunifu mwingine ukiendelea, hatujaona kazi nyingine kubwa endelevu katika kuitangaza Tanzania kimataifa, lakini tukianglia sana wataalamu wapo na watu wapo weneye uwezo, nia wanayo. Tunadhani tu sasa Serikali iende kuongeza pesa ya kutosha kwa ajili ya kuona kwamba tunaitangaza nchi yetu kwa kiwango kiubwa, ili tupate fedha nyingi. Nimeona azma hii Mheshimiwa Mchengerwa unayo umeisema leo sasa basi tuiombe Serikali ikuongezee fedha za kutosha ili kazi hii ifanyike kwa ubora mkubwa kabisa, tuweze kujipata kipato kikubwa na nchi yetu ipate maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine tuhakikishge vivutio vyetu vinafikika vizuri kwa haraka na kwa gharama nafuu na katika hili nishauri kivutio kikubwa katika nchi yetu ninachokifahamu mimi. Vipo vingine lakini kivutio hiki katika hifadhi ya Serengeti cha crossing ya wale wild beast katika Mara River ni moja na vivutio bora kabisa duniani. Kiko katika vivutio 15 bora, lakini kwa nini hatupati watalii wengi katika eneo hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya sababu ni kwa sababu ni mbali sana, hapafikiki inachukua muda mrefu sana watalii kufika kule, magari yanaharibika sana njiani, watalii huchoka sana, wanatumia masaa mengi barabarani, wanakosa comfortability, gharama kubwa ya kufika huko, barabara zinakuwa mbovu muda mwingi, umbali mrefu siyo mzuri kwa usalama wa watalii na hivyo basi wamewahi kufanya tafiti na tumesoma ripoti nyingi za wale mawakala wakubwa wa utalii duniani, wakiwemo Hot Wire, wakimwemo Agoda na wakiwemo Expedia wamesema ili watalii waende katika sehemu fulani kwa ajili ya kutalii, yako mambo yanayo-lead ile decision yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, 42% ni ubora wa kivutio, 20% ni ubora wa huduma za malazi, chakula na usalama, 20% ni kufikika kwa kivutio, ubora wa miundombinu ya barabara na usafirishaji, 18% ni unafuu wa gharama. Sasa basi ukiangalia pamoja na kivutio kizuri, pamoja na uwepo wa vivutio vingi sio sababu ya kutosha watalii kuendela kuja kwa wingi katika nchi yetu. Mfano mzuri tunaona Serengeti na hata nikienda kwa mfano mmoja rahisi tu, ukiangalia kutoka katika viwanja yetu vya ndege mpaka kufika sehemu hii ya kwa Kogatende ambako wanyama wale wanakatiza ule Mto Mara kuingia upande ule wa Kenya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka KIA mpaka Kogatende ni kilomita 610, kutoka uwanja wa ndege wa Arusha mpaka kwa Kogatende ni kilomita 557. Kutoka Mwanza Airport mpaka Kogatende pale Mara River ni kilomita 340. Kutoka Seronera kutoka Musoma, uwanja wa Musoma mpaka pale kwa Kogatende ni kilomita 187, kutoka Seronera central Serengeti mpaka kwa Kogatende ni kilomita 183, lakini kutoka Mji wa Mugumu mpka kwa Kogatende ni kilomita 56 peke yake na hili ndilo eneo ambalo limependekezwa kujenga uwanja wa ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nikuombe sana andika historia, jenga uwanja ule 147,000,000 wataalam wameshauri, tafiti zimefanyika, nikuombe Mheshimiwa Mchengerwa chukua hatua, hii itasaidia watalii kuongezeka, itasaidia kukua kwa uchumi kwa watu wa Mkoa wa Mara hususani Wilaya ya Serengeti ambao sisi tunapakana na hifadhi hii, tunahitaji kuona pia na sisi tunanufaiuka na utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutawasaidia watalii wengi kupunguza gharama za kuja kwetu, kupunguza umbali huu maana ya ke ni kupunguza gharama. Ni kupunguza kulala vituo vingi na hii itafanya watalii kwa comfortability kubwa tukijenga uwanja ule. Pia tunaenda kuongeza ajira nyingi kwa watu wa Mugumu na Serengeti kwa ujumla, tunaenda kusababisha kuongeza au kuboresha utalii na ule uhifadhi kwa sababu sasa ule utitiri wa vile viwanja vya ndege ndani ya Serengeti vinaenda kupungua. Pia tunaenda kuongeza maeneo ambayo watu wengi wanaweza wakajenga mahoteli ya kitalii katika Mji wa Mugumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kuomba sasa wizara hii iende kuangalia namna bora ya kuongeza na kuboresha...

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: …uhifadhi katika hifadhi ya Serengeti kwa kushirikisha sana wananchi ili kupunguza migogoro ya wanayama wanaingia na kuvamia wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja nakuomba dakika moja tu nimalizie. Sasa wananchi wengi sana wa Serengeti wamepata shida, wanyama wanaingia kila wakati, Mheshimiwa Mchengerwa nikuombe sana tusaidie kuona kwamba tunawashirikisha wananchi. Kama hatuweki tutumie teknolojia ya fensi, basi twende kuchukua wananchi wengi waweze kuelimishwa, waweze kuelekezwa, mambo ya kukamata wanayama wale ng’ombe na nini na wananchi wanaoingia waelimishwe sana.

MWENYEKITI: Haya ahsante sana Mheshimiwa kwa mchango wako.

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)