Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa kuwasilisha hotuba yake nzuri inayoonesha mwelekeo mzuri wa kuletea maendeleo Taifa letu. Pia nimpe changamoto kwamba ajitahidi kwa sababu Wizara hii ndiyo Wizara ambayo iko kwenye kioo cha kila mtu. Kwa hiyo, akifanya kweli ataonekana na asipofanya ataonekana hata kabla ya kuja hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kuchangia kuhusu hali ya anga la Tanzania. Kwa uono wangu kimataifa tunajulikana Tanzania tuna anga la Tanzania, hakuna anga la Zanzibar wala anga la Tanzania Bara. Hivyo basi, ni muhimu tunavyotoa huduma za anga tuzijenge kulenga kufanikisha kwa sifa ya Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na mawasiliano ya muda mrefu kati ya TCAA na Mamlaka ya Kiwanja cha Ndege cha Zanzibar. Kiwanja hiki kwa muda mrefu hakijafungwa kifaa cha Instrument Landing System (ILS) ambacho kilikuwa kifungwe kipindi cha miaka minne, mitano iliyopita, kila siku ahadi inakuwa kitakufungwa. Kweli huduma za ndege zinaendelea lakini hiki ni kifaa muhimu kinachowasaidia marubani kutua wakati wa usiku, mawingu na mvua kwa uhakika na usalama zaidi.
Niombe basi Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa atuambie kama hili jukumu si la TCAA, ni bora watoe kauli dhahiri inayosema kwamba hiki kifaa hawatakifunga na hakiwahusu ili sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iweze kuchukua jukumu la kutafuta hicho kifaa na kukifunga kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, si vizuri vitu kama hivi vikawa vinatupwa kama mpira. Ni bora kuambizana ukweli ili kila mtu afahamu jukumu lake, lakini litekelezwe ili kuleta ufanisi wa kazi tunazozifanya za kila siku. Tukipata sifa ya anga, nasema mara ya pili, ni sifa ya Tanzania na likitokea tatizo bado mamlaka hizi zitahusika na kutakiwa kujibu maswali ambayo kwa kweli nahisi hayatakuwa muhimu na ya msingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nichangie hilo lakini nimkumbushe Mheshimiwa Waziri akisaidie kiwanja hiki cha ndege cha Zanzibar. Nakumbuka lilitolewa jibu lakini nimsisitize tu awasaidie kulipwa lile deni lao la shilingi milioni 230 na ATC. Tunasikia au tumeambiwa madeni yatahamishiwa Hazina, lakini nimuombe tu alipe uzito ili kuwasaidia wenzetu hawa kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliomba dakika tano na nahisi zimenitosha kwa kuchangia jambo hili muhimu sana. Na mimi naunga mkono hoja.