Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nichukue nafasi hii kwanza kabisa niwashukuru wananchi wa Jimbo la Serengeti kwa kunichagua kuwa Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Mbunge wa kwanza wa CHADEMA tangu Serengeti iwe Wilaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache nahitaji kuchangia kwenye Mpango. Jambo la kwanza ni kuhusu mapato ya Serikali. Nimekuwa Diwani tangu mwaka 2010 katika vipindi vilivyopita ambapo Mpango wa kwanza ulianza, kwa kweli hali ya makusanyo ya mapato ilikuwa ni hafifu sana. Tangu niwe Diwani nimewahi kuona fedha za maendeleo kwa miaka miwili tu na hata hiyo miaka miwili fedha za maendeleo zinazokuja ni 20% au 22%. Sasa kwa namna hii haya malengo ambayo tumejiwekea hayawezi kufikiwa hata siku moja. Kama hatuwezi kukusanya kiasi cha fedha zinazotosha kwa ajili ya maendeleo yetu ni ngumu sana, tutaendelea kudanganyana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu elimu. Kwanza niwashukuru sana wazazi wa nchi hii kwa moyo wao mkubwa wa kujitoa kujenga shule na madarasa mbalimbali. Natambua Serikali ya CCM inajinasibu kwamba wao wamejenga shule kila kona lakini ukweli wajenzi wa madarasa, wanunuzi wa madawati ni wazazi. Kwa hiyo, nawashukuru sana wazazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tusipofanya mambo yafuatayo bado hatuta-improve chochote kwenye elimu, mimi kitaaluma ni Mwalimu. Ukiangalia shule za binafsi zinafanya vizuri sana kuliko shule za Serikali, tatizo ni nini? Walimu walewale wanaotoka Serikalini wakienda kule private wanafanya vizuri kwa nini wakiwa Serikalini wanafanya vibaya? Nilichogundua ni kwamba hakuna motivation kwa Walimu wa Serikali. Mwalimu mshahara uleule anaoupokea ndio huohuo afanyie mambo yote, haiwezekani! Lazima ifikie sehemu Serikali iwatazame Walimu, iwa-motivate Walimu mkiwaacha hivi wanakuwa demoralized hawawezi kufanya kazi kwa moyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine Serikali imesahau elimu ya chekechea. Huwezi uka-base kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba bila kuangalia elimu ya awali. Elimu ya awali tumeiacha kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni issue ya maabara, wazazi wetu wamejitahidi wamejenga maabara kila shule lakini sasa vifaa vya maabara hamna. Siamini kama Serikali hii miaka mitano itaisha ikiwa imepeleka vifaa kwenye shule zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Serengeti ni Jimbo ambalo sehemu kubwa ya Hifadhi ya Serengeti ipo. Serengeti ni mbuga ambayo inaongoza kwa kuwa na watalii wengi kuliko mbuga zote za wanyama zilizopo katika nchi hii. Hata hivyo, ukija katika Wilaya ya Serengeti, siongelei Serengeti National Park, naongelea wanapoishi binadamu, Mheshimiwa Maghembe nakumbuka mwaka jana umekuja pale, maji ya kutumia ni shida. Kilichosababisha nikawapiga CCM kwa muda mrefu maji hakuna. Tangu 2009 limejengwa Bwawa la Manchila mpaka leo hakuna chujio, hakuna usambazaji wa maji. Kwa hiyo, maji yale yako kwenye Bwawa la Manchila lakini namna ya kuyachukua yale maji kutoka pale kuyasambaza hakuna. Ingawa feasibility study ilishafanyika tangu mwaka 2009 mpaka leo implementation hakuna.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeupitia Mpango huu kwenye ukurasa wa 14, nilitegemea kuona Bwawa la Manchila lakini sijaona. Sijui huu Mpango ume-base kwenye nini. Ukiangalia kwenye huu Mpango ukurasa ule wa 14 kuhusu maji naona wame-base Dar es Salaam sijafahamu miji mingine itakuwaje. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango unapokuja ku-wind up tuambie kwamba mji mingine kwenye Mpango kwa nini haikuingizwa? Nimeona mme-base zaidi Dar es Salaam, je, miji mingine ambayo iko nje ya Dar es Salaam mnafanyaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni barabara, kwenye ukurasa wa 10 - 12 wa Mpango, nilikuwa najaribu kuangalia barabara za mikoa, karibia mikoa yote nchi nzima imeunganishwa kwa miundombinu ya barabara isipokuwa Mkoa wa Mara. Sasa nikasema ngoja niangalie Mkoa wangu wa Mara kama umeunganishwa na Mkoa wa Arusha. Mwalimu Nyerere kabla hajaondoka madarakani ali-propose ujenzi wa barabara ya Musoma – Butiama – Isenye - Nata - Mugumu - Tabora B na kadhalika lakini mpaka leo zimepita awamu nne barabara ile haijajengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mimi sijawa Mbunge nilikuwa natazama Bunge nasikia kwamba zimetengwa billions of money kwa ajili ya ujenzi wa barabara ile, lakini hata mita moja ya lami haijawahi kujengwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango unapokuja ku-wind up kwenye huu Mpango, hebu tuambie watu wa Mkoa wa Mara barabara ya kutuunganisha na Mkoa wa Arusha itaanza kujengwa lini na itakamilika lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni vizuri tufahamu kwamba Mkoa wa Mara na hususan Wilaya ya Serengeti kitega uchumi kikubwa tulichonacho ni Serengeti National Park na Game Reserve zilizopo lakini watalii ili waje Serengeti ni lazima tuwe na miundombinu mizuri ya barabara. Kwa mfano, barabara ya kuanzia Tarime - Mugumu, barabara ya Musoma - Sirori Simba - Magange - Ring‟wani - Mugumu, ni vizuri zikawekwa lami ili watalii wanapokuja basi waweze ku-enjoy sasa hivi ni za vumbi hata hazieleweki. Haiwezekani mji wa Mugumu ukakua kwa haraka. Ndiyo maana hata Mheshimiwa Rais wakati anafanya kampeni mwaka jana Serengeti hakuja kwa sababu ya tatizo la barabara. Barabara za Serengeti ni mbovu kuliko zote nchi nzima. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Mipango unapokuja ku-wind up hebu tuambie watu wa Serengeti ni lini barabara ya Musoma – Makutano –Butiama - Nata, Isenye - Tabora B - Clains na Loliondo itakamilika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kilimo. Serengeti kwa sasa chochote tunacholima tunatengenezea tembo. Ukilima mahindi, mihogo, jua unasaidia tembo kushiba. Tukakubaliana wananchi wa Serengeti tulime tumbaku lakini tumbaku tunayoilima haina soko. Sasa tukimbilie wapi watu wa Serengeti? Nyie CCM mmepewa nafasi na wananchi wa nchi hii kwamba muiongoze nchi hii, lakini nawaambia kama msiposimamia rasilimali za nchi hii fursa zikaenda kila eneo mwaka 2020 mtapigwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana Mheshimiwa Profesa Maghembe jana umetupokea na kwa kweli wananchi wangu wa Serengeti wamekushukuru sana. Naomba utusaidie wananchi wa Serengeti, tumesaidia tembo kutoka 3000 – 7000, sasa hivi tembo wanatutesa, hebu tusaidie basi hata gari moja. Serengeti nzima unapokuja hatuna gari hata moja ambalo mmetupa ninyi Wizara, gari moja tulilonalo alitupa mwekezaji, Grumeti Game Reserve ambalo kwa sasa limechakaa haliwezi kufukuza tembo hebu tusaidieni magari kwa ajili ya kufukuzia tembo. Namshukuru Mungu kwamba tumepata zile ndege (drones) najua zitasaidia lakini haziwezi kusaidia kama hawana magari. Tusaidiane magari ili tuweze kufukuzana na hawa tembo. Sisi watu wa Serengeti tumeamua ku-conserve mazingira ya SENAPA na tumeamua tushirikiane na watu wa Serengeti National Park hebu basi na nyie tuoneni majirani wenu kwamba tunaumia na tembo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ni kuhusu madeni ya Walimu. Nimekuwa Mwalimu Serikalini, nimekuwa Mwalimu private, Walimu wana shida kubwa sana. Sijaona kwenye Mpango kama kuna sehemu yoyote ambayo mmekusudia kuwalipa Walimu. Mheshimiwa Waziri utakapokuja ku-wind up utuambie ni lini mtalipa madeni ya Walimu.
MWENYEKITI: Mheshimiwa muda wako umeisha.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. (Makofi)