Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nami niongee mawili katika hii Wizara ambayo ni moja kati ya Wizara kubwa bahati mbaya sana tunaweza tusiwe tunaona ukubwa wake. Ukubwa wake hauonekani, moja katika bajeti kwa sababu bajeti ina-signify au bajeti inaonesha ni kwa kiwango gani watu mnachukulia serious Wizara husika ambayo mnaisemea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Michezo, Sanaa na Utamaduni inapaswa kuwa ndiyo definition halisi ya sura ya nchi lakini leo na bahati mbaya sana wakati ninatafakari nikafikiria pengine Wizara ya Michezo, Sanaa na Utamaduni tunaichukulia kama Wizara ya Michezo, yaani tunai-qualify kwamba ni mchezo na ndiyo maana tunafanya mchezo na ndiyo maana bajeti yetu inakuja ikiwa ya mchezo mchezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niulize, hivi shilingi bilioni 35 unaweza ukafanya nini, unaongelea fedha ya maendeleo shilingi bilioni 11 imeeleza vizuri Kamati hapa unaweza ukafanya nini? Siyo hiyo tu, tumeona hata bajeti iliyokuwa imetengwa mwaka jana haijaenda kwa asilimia 100. Kwa hiyo ni vitu ambavyo moja ni vichekesho, mbili inatuonesha hata sisi tunaochangia hatuko serious tunafanya sanaa kama Wizara tunavyoiita ya sanaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema siyo sahihi? Moja, mnachopaswa kujua, michezo, utamaduni ni moja kati ya vitu ambavyo tunaweza kupata foreign currency. Ni maeneo ambayo nchi ikiamua kuwekeza vizuri, leo ukiitaja Marekani inajulikana Marekani kwa kucheza rugby. Ukitaja Marekani inaonekana kwa kucheza basket, ukiongelea Kenya wanajulikana kwa kukimbia kwa riadha. Leo ukiitaja India kwa mbali utasikiliza utafikiria Bollywood. Ukiitaja Nigeria utaongelea Nollywood. Sisi tunajulikana kwa lipi? Hatuwezi kukimbiza kuku, hatuwezi kukimbia, hatuwezi kufanya chochote, is it true? Siyo kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi vyote tunaweza kuvifanya. Tumekosa utashi wa kufanya hayo yote. (Makofi)

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

TAARIFA

MWENYEKITI: Mheshimiwa Anatropia kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ramadhan Ramadhan.

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa mzungumzaji kwamba sisi ukitutaja tunajulikana kama Swahiliwood. (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Anatropia taarifa unaipokea?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo mbaya hata kuwa Swahiliwood siyo mbaya ni lugha kama ambavyo wengine ni Englishwood ni Indianwood lakini we have to go far, lazima tuende mbali na hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ikabidi niitafute dira, dira ipi inatuongoza kufanya kazi? Dira ipi imekuwa instrument ya Wizara, tena nimesoma ikawa, “Kuwa Wizara inayohakikisha ushiriki wa ushindani katika michezo, sanaa na utamaduni wa kitaifa unaolenga maendeleo ya Taifa.” Nikataka niwaulize ninyi mmeisaidiaje hizi tasnia kuwa washiriki wenye ushindani? Mmesaidiaje michezo kwa maana ya mipira kuwa kwenye ushindani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Yanga niwapongeze watani wangu Yanga mmejaribu baada ya miaka 30 ya Simba leo mmejaribu. Niwapongeze Yanga, mmeona Yanga wamewekeza wakaleta wachezaji wazuri wamepata walichokipata. Vivyo hivo kwenye michezo mingine wanasema numbers don’t lie, eh? Ukiwekeza unapata matokeo, wamewekeza wamepata matokeo. Tunataka tupate matokeo gani kwenye Wizara ya Sanaa na Michezo tukiwa tumewekeza shilingi bilioni 35? Tukiweka hela ya maendeleo ambayo ni shilingi bilioni 11 kwenye bajeti amesema hapa msemaji anasema out of 15 trillion ya fedha za maendeleo, sisi tumeweka shilingi bilioni ngapi, bilioni 11 ambayo ni 0.08 kwenye fedha za maendeleo. Hivi tunataka maajabu kutoka nchi gani tuweze kufanikisha hii sera? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini ninasisitiza umuhimu wa Wizara hii? Moja ni source kubwa ya kupata ajira. Mbili; ni source kubwa ya kupata fedha za kigeni. Tatu; ni source kubwa ya kusaidia hata vipato vya kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma mchango wa Wizara hii katika Pato la Taifa ni 0.03! Siyo sawa, tunaweza kufanya vizuri kama tukiamua. Mimi ningekutana na Mheshimiwa Rais kama ananisikia ni lazima tufanye overhaul. Yaani tufanye a total transformation. Moja; jinsi ambavyo tunaitafsiri michezo katika hii nchi. Hatuwezi kuchukulia michezo kama kitu eti tunataka kufurahisha watu, tumeshaenda zaidi ya kufurahisha watu, tunataka kupata fedha, kupata utajiri kutoka kwenye vipaji vyetu. Kwa hiyo, nitamshauri Mheshimiwa Rais afanye transformation. Pia hii Wizara aipe uzito kama zilivyo Wizara nyingi na kubwa katika nchi hii. Yaani ukiacha Wizara ambayo tunaiona ni kubwa, ya pili inapaswa kuwa Wizara ya Michezo, Utamaduni na Sanaa kwa sababu ya umuhimu na ukubwa wake kugusa watu wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafikaje hapo. Moja; ni lazima turudi sasa kwenye tulivyoanza miaka ile, tufungue vyuo mbalimbali vya michezo. Tu-train walimu wa kutosha wa michezo. Ni lazima tu-recruit. Serikali ina maana ni vitu viwili; sera na uwekezaji wa Serikali. Kama sera yetu ikijikita ikaendana sambamba na uwekezaji wa Serikali tutafika tunakokutaka na hapo tunakuja kuongelea mambo ya scouting. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuna vipaji kadha wa kadha mitaani. Nitatoa mfano Mheshimiwa Waziri. Kuna baadhi ya vijana niliwatoa Kyerwa kuja kuwasaidia kwenye academy mbalimbali kwenye hii nchi. Nataka nikwaambie nimehangaika hata kuwatafutia timu za ku-train mpaka nimechoka. Yaani huwezi hata kupata timu hata kama kijana ana uwezo wa kiasi gani wa kucheza mpira, kupata hata timu ya kuchezea ni changamoto kubwa sana, na hao ni watu ambao at least wanamjua Mbunge, vipi wale ambao hawana hata wa kuwashika mkono? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hiyo tu, walimu uwaandaliwe wa kutosha kwenye vyuo, lakini hivyo vyuo kuna baadhi ya academy leo zina-train michezo. Moja; zipewe ruzuku kidogo lakini zipunguziwe gharama ili ziweze kuwekeza zaidi katika ku-spot na kutengeneza walimu na wanamichezo vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu; Lazima tutafute partnership. Bahati nzuri wanamichezo tulipata ridhaa ya kwenda Southern Sudan. Tuliona Southern Sudan wanajiandaaje kushika dunia ya michezo. Kila ulikoenda wamefungua academy za basketball, za football, za netball, sisi tunafanya nini hapa? Viwanja vya michezo vilivyokuwepo kwenye maeneo yetu leo vyote vimevamiwa. Maeneo ya wazi yote leo watu wameyafanya mabaa, watu wamejenga na hakuna anayeongelea tena na Wizara hapa sijaona inaelezeaje tunawezaje ku-promote michezo bila kuwa na viwanja vya michezo hususan mpira wa miguu naongelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tuna safari ya kwenda, tuna safari ya kwenda kabla ya kujua tunafikaje kule na hiyo inaanza na total transformation na hiyo inaanza na kubadilisha mindset na hiyo inaanza na political will ambayo sasa hiyo ni bajeti ya Serikali. Nakushukuru. (Makofi)