Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata fursa hii kuchangia katika Wizara hii ambayo na-declare interest kwamba nahusika, mimi ni mdau mkubwa wa hii Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa sababu katika Wizara ambayo anaonyesha mapenzi ya dhati kabisa, kuwapenda kabisa ni Wizara hii. Ndiyo maana sasa hivi naona hamasa kubwa katika hii Wizara, tayari ameishaonesha dira kabisa kwamba hii Wizara ni watoto wangu, wanahitaji kulelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tayari Mheshimiwa Rais ameshaonesha dhamira ya dhati katika Wizara hii, Mheshimiwa Waziri na Waheshimiwa Wabunge waanze kuangalia Wizara hii kwa mnajili mpya kabisa, tukianzia hasa kwenye masuala ya bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri. Kusema kweli, mimi ni kati ya watu ambao nilishangaa kumwona Bakhresa amekuja kwenye hii Wizara, Mama ana jicho la mbali sana, lakini naanza kuona sasa namna gani umeanza ku-cope vizuri na wanasanii na wanamichezo. Tayari tunaanza sasa kuona siku ile kwenye Tuzo tulikuwa tunacheza sana pale, tunaanza kuona sasa Wizara imempata mtu ambaye anaweza akaifanyia kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumpongeze Mheshimiwa Rais pia kwa kumchagua kaka yangu Kipenzi Mheshimiwa Hamis Mwinjuma tayari huyu ambaye ana-idea anajua kabisa, anajua shida na chnagamoto za Wizara hii naamini kabisa kwa sababu yeye ni mwanamichezo lakini pia ni mwanamuziki ataenda kuleta ukombozi katika wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la bajeti. Kwa kuangalia zamani wakati nasoma tulifundishwa basic needs katika maisha na wakawa wanasema kwamba malazi, mavazi, usafiri ikawa ni kitu kama luxury sasa hivi usafiri siyo luxury tena ni lazima. Leo hii katika hii wizara tunaangalia kama entertainment kwamba hii Wizara ni kwa ajili ya entertainment hapana siyo kweli. Hii Wizara inaenda kuwa mkombozi mkubwa wa kupunguza ajira katika nchi hii. Kwa namna gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Wizara ikiweka mikakati mizuri kama ambavyo alivyoweka mikakati kaka yangu Bashe katika BBT. Hii Wizara italeta heshima ya kupata bajeti kubwa sana na kuweza kuendeleza Wizara hii katika uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu niambie Waheshimiwa Mawaziri hao wawili ambao tayari wamepewa dhamna katika wizara hii muhimu sana katika nchi yetu waangalie namna gani ya kuja kuwa–convince wabunge hawa waangalie mikakati gani waipange katika nchi hii, ili iweze kuondoa hii isuue ya bajeti. Leo hii bilioni 35 ni bajeti ndogo sana, ni bajeti ya aibu najisikia vibaya kwa sababu hii wizara ambayo inanihusu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Mheshimiwa Rais Wizara hii imeweza kutoa mikopo kwa badhi ya wasanii mnaweza kuona namna gani Mheshimiwa Rais anaipenda hii wizara, lakini leo hii Wizara ina bajeti ya bilioni 35, nazungumza hapa wasanii wakiwepo pale, nazungumza hapa wanamichezo wako humu ndani bilioni 35 inaenda kusaidia kitu gani katika hii Wizara? Tuangalie namna nyingine ya kufanya uwekezaji katika Wizara hii ili iweze kusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine Mheshimiwa Waziri mimi ni mmoja ya watu ambao tulikuja kwenye tuzo za wanamuziki pale the The Dom Masaki. Mheshimiwa Waziri na Wizara yako naomba niwapongeze sana mwaka jana hii shughuli imeanza na sasa hivi mwaka huu mmefanya kazi nzuri sana, lakini naomba niulize au niwaambie ni namna gani ya kufanya kwa namna moja ama nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri umewaandalia wasanii tuzo. Wasanii hawa ambao wameandaliwa tuzo. Tuzo zinatangazwa pale kwa ajili ya wasanii kupewa tuzo hawapo na wengine hawajaandaa hata wapokeaji wa tuzo hizi sasa unajiuliza ni kwamba lack of coordination ama ni shida iko wapi? Je, wasanii hawajazipokea hizi tuzo ama Mheshimiwa Waziri na jopo lako hamjaweza kuzitangaza hizi tuzo vizuri au kuwapa tarehe nzuri ya kujua tuzo ni tarehe fulani na wasanii wote wanapaswa kuwepo. Mimi sijawahi kuona huko nje kina Beyonce wakakosa kwenye tuzo, sijawahi kuona kina Rihanna wakakosa kwenye tuzo, kwa sababu ndiyo sehemu pekee ya kuonesha appreciation ya kazi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii unaenda pale unakuta nusu ya wasanii ambao wanaenda kupewa tuzo hawapo hii inaondoa hamasa na Ladha ya tuzo zetu za Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri tafuta namna ya kukaa na wasanii wako. Wasanii ni wasikivu na wanakuheshimu, wanaheshimu Serikali ya Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan. Fanya warsha mbalimbali, fanya semina mbalimbali, waelimishe mambo ambayo unataka kuwafanyia, waoneshe njia waoneshe upendo. Nina uhakika hao wasanii wako watakuwa wanashiriki kila tukio ambalo wewe na Wizara yako inaandaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mimi nilijisikia vibaya naona hadi wasanii ambao juzi tu wametoka eti na yeye hayupo. Ukiuliza yuko wapi? hujui. Yaani haijulikani yuko wapi nasema sasa hii tuzo ameandaliwa nani? Kama siyo wasanii. Kwa hiyo, tuangalie either kama shida iko kwa wasanii basi zungumzeni nao, lakini kama shida iko kwene menejimenti ya Wizara basi fuatilieni hili jambo mjue namna gani ya kuweza kwenda kusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu nataka nizungumze kuhusu mmomonyoko wa madili. Naisema huku kwa sababu wizara hii au tasnia hii ni sehemu mojawapo ya mmomonyoko wa maadli katika Tanzania yetu. Nasema hivi kwa sababu nimetokea huko nafahamu vizuri jinsi gani mtu anaona kwa namna moja au nyingine kwamba ili mimi niwe msanii lazima nivute bangi, ili niwe msanii lazima ninywe madawa ya kulevya, ili niwe msanii lazima ninywe pombe, ili niwe msanii lazima nicheze uchi yaani kuna vitu vingi sana katika wizara hii ambavyo Mheshimiwa Waziri kwa weledi wako, kwa muonekano wako, kwa namna yako na uzoefu wako utawaweza Kwenda kuvifanyia kazi, ili hii wizara au hivi vipaji wazazi huko nyumbani waweze kuruhusu watoto wao kutaka kuwa wasanii tulinde utamaduni wetu. Tulinde asili yetu tulinde utanzania wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la utamaduni unaweza ukaona sasa hivi dunia ilivyo badilika masuala ya utandawazi mambo yamebadilika. Watu tumepita kwenye phases za kubadilisha nywele, phases za kuweka kope za kujichubua…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. KHADIJA S. TAYA: …lakini sasa hivi kuna phases ambayo ni mbaya sana ya kubadilisha maumbile.

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Tunabadilisha maumbile yetu leo hii huyu mtu mwembamba hana shape lo hii kesho kutwa unamuona ana shape kubwa sana.

MWENYEKITI: Ahsante muda wako…

MHE. KHADIJA S. TAYA: Kwa hiyo naamini hii Wizara ya kuelimisha vijana wetu, watu wetu…

MWENYEKITI: Muda wako umeisha Mheshimiwa Khadija, ahsante sana.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa fursa hii lakini Serikali iangalie namna gani ya kusaidia vizazi vyetu Tanzania inaenda kunagamia kwa namna hii. Ahsante sana nashukuru sana. (Makofi)