Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niwapongeze kwa uteuzi, dada yangu, Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Chana, nimetoka naye mbali UVCCM kule, najua uwezo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nimpongeze Binamu, rafiki yangu, wasanii wanasema ile Master’s ya Uingereza walikuchangia, kwa hiyo wanataka waone matunda yake. Wanajua uko sehemu sahihi ya kubadilisha industry yao lakini na uwe mfano kama kijana wa Kitanzania ambaye umepitia huko unajua changamoto zao, matokeo wanataka wayaone; mimi sina shaka na wewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi kwanza nianze na jambo moja, Mheshimiwa Waziri wa Fedha tunaomba, hii michezo ya kubahatisha iende kwenye Wizara husika. Tunalia hapa watu hawana bajeti, wewe una vyanzo vingi vya fedha; una majengo, una mambo ya matrilioni huko, mabilioni, sasa hawa ambao vyanzo vyao vidogo hata michezo ya kubahatisha? Kwa sababu hata hicho kinachokwenda kinakwenda kama hisani, wapewe fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na Waheshimiwa Wabunge, tupambane humu ndani hii Wizara iheshimike kama tulivyoipambania Wizara ya Maendeleo ya Jamii. Hii Wizara itatengeneza ajira mpya, hii Wizara ikipewa fedha za kutosha Taifa litakuwa na furaha. Watanzania wanapenda michezo, tutapata Timu bora ya Taifa; haviwezi kuja hivihivi kama tusipowekeza. Lazima Wizara hii ipewe fedha ya kutosha iwe na vyanzo vya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema Mheshimiwa Tarimba hapa, wanakusanya mabilioni kwenye michezo ya kubahatisha halafu wanapewa vipesa vidogo, haiwezekani. Hicho ni chanzo chao cha sahihi, wapewe waweze kuwekeza maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Waheshimiwa hapa wanasema tunawaona tu wasanii wakubwa, ni kweli, huko mikoani kuna wasanii wengi. Kama Wizara haina fedha itawezaje kutengeneza mazingira mazuri ya kuwasaidia wale wasanii wengine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Mara tuna wasanii bwana; kuna Lady Jay Dee pale Bunda, lakini alifika hapo kwa taabu, hatuhitaji wengine wa-suffer kama Lady Jay Dee. Tuna Isha Mashauzi, Mkurya wa kwanza kuimba taarabu. Tunahitaji Wakurya wengine kule tuwaibue waimbe taarabu. Tuna Getrude Mwita, ‘Kibibi’, anaigiza vizuri. Tunahitaji hii Wizara iwezeshwe ili watokee akina Kibibi wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bila kuwekeza, siyo kwenye football peke yake, kwenye sanaa, kwenye utamaduni, hii Wizara ikiwekeza vizuri tunaamini tutapata wasanii wengi walio mikoani huko watatambulika na hii nchi itajivunia wasanii mbalimbali kutoka pande mbalimbali za nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mara sasa hivi Mungu ametujalia tuna timu mbili kwenye Ligi Kuu; tuna Biashara United. Lakini Uwanja wa Musoma ni mbovu, unahitaji ukarabati, una jukwaa moja tu, zikichezwa pale timu kubwa mapato yanakuwa madogo, kwa hiyo klabu inakosa mapato ya kutosha, tunahitaji uwanja ukarabatiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunda tuna Uwanja wa Sabasaba, tuna Bunda Queens, wameshinda kucheza Ligi Kuu ya Wanawake, lakini Uwanja wa Sabasaba hohehahe; ni lini mtaukarabati Uwanja wa Sabasaba ili Timu ya Bunda Queens iwe na uwezo wa kucheza uwanja wa nyumbani? Hayo mambo tunahitaji majibu sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabondia wetu wanahitaji na wenyewe wawe na viwanja vyao. Zamani ukisikia bondia anapigana unasikia DDC, viwanja vyao. Watengenezewe mazingira mazuri, na tunapata mapromota hapa akiwemo Mheshimiwa Mwakagenda, mabondia wamechoka kwenda kupigania kwenye viwanja vya mpira; hilo ni jambo sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna jambo la msingi, sasa hivi wakipata matamasha kwenda kupigana nje ya nchi anatakiwa kwenda peke yake; anawezaje kushinda bila kocha? Iwe kama timu za mpira wa miguu, inaposafiri timu inakuwa na kocha na benchi la ufundi. Ukienda wasanii akisafiri anakuwa na meneja wake na dancers wake. Kwa nini kwa upande wa mabondia anatoka yeye, yaani atoke Mwakinyo peke yake bila benchi lake la ufundi, bila kocha wake; hii haiwezekani. Mchezo wa ngumi umekua hivyo lazima upewe thamani yake; hilo ni jambo la msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tujue mchaka wa Vazi letu la Taifa umeishia wapi? Iliundwa kamati, imeyeyukia wapi? Yaani Watanzania wakiwa wanadai Vazi la Taifa ndiyo mnaanza kuwakusanya wanamitindo mbalimbali. Mchakato wa Vazi la Taifa umeishia wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani sasa hivi kila mtu anaamua tu anachagua vazi analolipenda, mimi na mwili wangu najua nikivaa Kihindi hapa nikipiga Sari, Punjabi ntakaa sawa, mwingine anachagua tu Vazi la Uganda, Vazi la Rwanda. Jamani, Taifa hili lina historia yake, tuna mavazi mengi, tupendekeze tukija humu Bungeni hata siku moja moja na sisi kama Wabunge tuna Vazi letu la Taifa. Lazima muweke historia ya kumaliza mchakato wa Vazi la Taifa; hilo ni jambo la msingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine, Mheshimiwa Mwana FA na Mheshimiwa Waziri, wewe ume-perform nchi mbalimbali, tunahitaji arenas. Leo hii msanii mkubwa ndiye mwenye uwezo wa kwenda kukodi pale Mlimani City. Ukumbi ule si chini ya milioni 30, bajeti yake ili aweze kuandaa tamasha anatakiwa atenge kama milioni 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na arenas nyingi hata ya watu 20,000, tukiwa na arenas za kutosha ushindani utakuwa mkubwa, hata bei itapungua. Watakaoukuwa na uwezo wa ku-meet standard ya kwenda kwenye arena watakuwa wengi, gharama itapungua…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)