Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza Mheshimies Rais kwa kuhamasisha michezo, utamaduni wetu na sanaa. Pili nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa anayofanya. Nampongeza anavyohamasisha, mkononi mwako tumeshuhidia ushindi kwa vijana wetu wa Fountain Gate School, lakini pia hatua iliyofikiwa na timu ya Yanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia Naibu Waziri - mtu mwema, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote, niwapongeze pia kwa kuwa na utaratibu wa mikopo kwa ajili ya kukuza utamaduni na sanaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya Wizara ni ndogo mno, ni vyema iongezewe ili kuwezesha maendeleo ya majukumu yaliyokusudiwa. Nyasa tumeanza kujenga uwanja wa mpira, mnatuchangia nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.