Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ione namna ambavyo itakuza utamaduni kwenye maeneo ambayo yanapakana na mbuga zetu au maeneo ambayo watalii wengi hutemebelea kwa nia ya kusaidia kukuza utalii na kuongeza ajira nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Iringa kama lango la utalii liangaliwe pia hasa ukizingatia historia ya watu wa Iringa na Chifu Mkwawa. Pia kuanzisha matukio mbalimbali kama mashindano ya ngoma, mbio na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wizara ibuni njia muhimu za kushirikiana na wadau kuinua utamaduni wa sehemu husika na kuibua vivutio mbalimbali vilivyopo kwenye miji nchini ili kuimarisha ustawi wa afya ya jamii miongoni mwa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.