Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ili niweze kuchangia katika mada ambayo iko mbele yetu. Kwanza naunga mkono hoja ya Waziri aliyoiweka hapa mezani. Pili, niseme tumepokea maoni ya Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwatoa wasiwasi Waheshimiwa Wabunge, Wizara hii ya Michezo, Utamaduni pamoja na Sanaa ni Wizara mojawapo kati ya Wizara za kipaumbele. Niwaombe waendelee kuiona katika sura hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, tuna Mheshimiwa Rais ambaye ni mwanamichezo kweli kweli, tena sio tu mwanamichezo ni mwanamichezo ambaye pia maono yake yana baraka, unaweza ukaona namna ambavyo timu zetu zilivyoweza kufanya vizuri. Taja timu zote ambazo umeona Mheshimiwa Rais ameweka mkono zimeweza kufanya vizuri sana ukianza na timu za wanawake, uje timu za vijana, uje timu za ngumi, taja kila aina ya mchezo unaweza ukaona ambavyo umefanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo moja tu ambalo linaweza likawa linatofautiana kwa nadharia halafu mpaka ikaonekana labda bajeti ya Wizara hii ni ndogo sana. Ni mategemeo ya Serikali na ni uelekeo wa Serikali ambapo tumeona vile vitu ambavyo vinaweza vikafanywa kwa ufanisi tuna Sekta binafsi, sio lazima Serikali iweke fungu kutoka kwenye Bajeti Kuu. Hii ni kwa sababu ya kukua kwa mahitaji katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakwambia experience nzuri tu ambayo Waheshimiwa Wabunge wametoa mifano hapa katika nchi zingine nyingi tu ambazo wamefanikiwa kwenye michezo, waliweka dirisha linalotoa fursa kwa sekta binafsi kwa makampuni yaweze kushiriki katika shughuli za michezo na kile watakachokuwa wamekitoa kwenye michezo kinakuwa deducted kwenye kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wenyewe walipitisha mwaka jana, jambo hilo lipo kwenye hatua zetu za kikodi. Kwa maana hiyo ni vile ambavyo labda hamasa haijaweza kukolea lakini jambo hili Bunge lako lilipitisha na huu ndio utaratibu mzuri ambao duniani kote sekta ya michezo inakuwa financed kwa namna hiyo, kwa hiyo nitoe rai kwa makampuni yashiriki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli tutakuwa hatuitendei haki sekta binafsi, tukitaka hata magoli ya uwanja kwamba lazima yatengewe fedha kutoka Mfuko Mkuu. Kuna vitu vingi ambavyo tunaweza tukavifanya ambavyo sekta binafsi haiwezi ikafanya, lakini kwenye haya ya michezo tuna fursa nyingi ambapo sekta binafsi inaweza ikafanya na ika-complement bajeti ya sekta hii ikawa kubwa tu. Kwanza masuala ya michezo kwa jinsi yalivyo siyo mambo ambayo unaweza ukaya-streamline halafu ukaachia kila wakati yatoke Mfuko Mkuu. Kwa hiyo, nasema kwamba tunaendelea nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika pongezi hizi mnazoona mwaka jana, mwaka juzi hata hii five percent ambayo inaenda kwenye Sekta ya Michezo haikuwepo. Tumshukuru Mheshimiwa Rais mwaka jana akasema tutoe five percent ikaenda kule, lakini akaweka na ahadi nyingine kwamba tunapoenda kwenye Bahati Nasibu ya Taifa tutaweka kiwango kingine ni vile tu hatujapata total figure ni kiasi gani, lakini mchakato wa manunuzi utakapokamilika tutakaa na Wizara kwa sababu hilo linatarajiwa lianze tunapoenda mid-year review, tutakaa na Wizara tuwaongezee kiasi kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sio hilo tu, tumekaa na Wizara tumewapa fursa EPC+ F kwenye ukarabati na ujenzi wa viwanja ambayo ni bajeti kubwa tutaisemea tunavyokuja kwenye bajeti kubwa ile inayokuja, lakini tulishatoa fursa kwenye bajeti hii inayomalizika wanayo hiyo commitment ili Wabunge waweze kuona ni kwa namna gani Serikali inaweka uzito kwenye jambo hili ambalo wameliongea…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato wa bajeti ni mchakato, tumesikia maoni yote haya kwa ujumla wake, tunakokwenda mbele tutaendelea kuboresha ili tuweze kuya-incorporate haya maoni ambayo yametolewa na Waheshimiwa Wabunge katika kuboresha michezo. Mheshimiwa Rais ni mwanamichezo, mimi mwenyewe ulevi pekee nilionao ni huo wa michezo na nazitakia kila la heri timu zote, nikiipongeza Yanga, sisi ni Mabingwa na nitatoa mwondoko, mabingwa wanaondokaje, Mabingwa wa Afrika nitakapokuja kutoa Bajeti Kuu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)