Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi ya kuzungumzia habari ya suala la mahindi.

Mheshimiwa Spika, Kiteto ni hub na ndio bread basket ya ukanda huu. Tangazo la Serikali la kufunga kupeleka mahindi nje tunaamini ilikuwa ni nia njema sana. Lakini kwa mfano Kiteto, mahindi kwa gunia ilishafika elfu tisini lakini baada ya zuio hilo, na nimetoka jana Kiteto imekuwa shilingi 55,000.

Mheshimiwa Spika, tunachosema, wazo la Serikali kununua mahindi hapa limepokelewa vizuri sana na wakulima. Tunachoomba Serikali inunue kwa bei ambayo wakulima walikuwa wauze huko. Tukitoa tangazo na likashusha bei itaumiza wakulima. Kwa hiyo tunachoomba ni rahisi sana, Mheshimiwa Waziri wa Kilimo mahindi yalishafika bei elfu tisini kama mnatoa na kwingine naambiwa imefika laki na ishrini.

Mheshimiwa Spika, kama mnataka kununua mahindi yote na fedha zipo, tengenezeni vituo na tuwe na navyo Kiteto na kila Kanda ya nchi hii na tukubaliane bei hapa na Mheshimiwa Waziri, tangaza bei hiyo, tena chukua ile ambayo ni the highest kama ni laki na ishirini ndio imekuwa the highest Serikali inunue kwa hiyo laki na ishirini. Mkifanya hivyo wakulima mtakuwa mmewatendea haki sana.

Mheshimiwa Spika, mwaka huu mvua ilikuwa kidogo, upatikanaji wa mahindi umekuwa ni mgumu sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa, kengele imeshagonga.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.