Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia hoja hii. Wazo la Serikali la kuwa na vituo hivi ni la muhimu na ni la msingi kwa ajili ya faida ya mkulima wa chini kabisa. Lakini vituo hivi vya NFRA viko vichache, na mwendo wa mkulima kutoka kata moja kwenda sehemu ambayo wameweka kituo ni mbali sana na hivyo kuongeza gharama katika ununuzi wa mazao hayo. Kwa mfano, mkulima anabeba mahindi anapeleka zaidi ya kilometa 100 kwenda kuuza; obvious ile bei ya shilingi mia nane itamkata mkulima. Kwa hiyo tunaomba vituo viongezeke viwasogelee sehemu ambapo wakulima wapo.

Mheshimiwa Spika, lakini mbili wale wauzaji ambao Mheshimiwa Bashe ni watendaji wako kule chini wengi sio waaminifu wanaenda kusema mahindi haya hayafai ni reject lakini wakati huo huo wanaenda kuuziwa wao pembeni nakuja kuuza ndani. Of course hili suala linahitaji utafiti wa kiintelijensia ili uweze kuhakikisha hilo suala, kwa sababu leo mkulima kabeba mahindi kilometa zake tano, sita amepeleka kwenye kituo mnunuzi anasema mahindi haya hayafai.

Hilo nililisema hata kwenye parachichi haya, lakini usiku watu wachache, wajanja, madalali wananunua na tena wanayapeleka kwenda kuyauza kesho yake. Tunaomba uangalizi wa karibu uwepo na kuhakikisha maadili yanakuwepo kwa wale wanunuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia, hili ni soko huria, tunaomba wananchi wapewe uhuru wa kuuza. Nimelima mahindi yangu, nahitaji kumpeleka mtoto shule, nikauze ninapotaka mimi, baadaye itatusaidia sisi kuweza kujua bei itakuwa juu na mkulima atajisikia vizuri akiuza anapotaka. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)