Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. JACQULINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Kwanza kabisa nianze kuipongeza Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, Serikali imara, yenye Sera nzuri zinazokubalika na zinazotekelezeka. Niipongeze sana Serikali yangu ya Awamu ya Nne iliyokuwa ikiongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Katika Wizara hii ya Miundombinu ilikuwa na Jemedari wetu ambaye sasa hivi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Pombe Magufuli. Serikali hii imefanya kazi nzuri ya kuhakikisha ya kwamba mikoa yetu inaunganishwa na barabara za lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, inashangaza sana hata kama huna masikio, lakini hata macho hayaoni? Amesimama mlevi mmoja hapa, mimi namuita mlevi, amesimama mlevi akisema kwamba eti Serikali ya Chama cha Mapinduzi hamna chochote inachokifanya. Barabara hizi zimejengwa kwa 31% kwa miaka 15! Safari ni hatua, kama imefikia 31% ina maana Serikali inafanya kazi na inaendelea kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumtia moyo Waziri wa Miundombinu na Naibu wake pamoja na delegation yake yote, endeleeni kuchapa kazi, sisi tuko nyuma yenu, tunaendelea kuwaombea. Kazi mnayofanya ni nzuri na inaendelea kuonekana kwa hiyo, ungeni pale ambapo Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Dkt. Magufuli walipoishia ninyi endelezeni pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niseme tu kwamba, hakuna mwanamke yeyote yule atakayeweza kumsifia mke mwenzake hata siku moja. Mke mwenza ni mke mwenza tu na kama ikitokea ukamsifia mke mwenzako basi wewe kidogo utakuwa fuse down. Hali kadhalika, debe tupu ndilo lenye kelele, debe lililokuwa na ujazo mzuri halipigi kelele. Tunawashukuru wananchi wetu wa Tanzania ambao wameona umuhimu wa kukipa Chama cha Mapinduzi kura za kishindo na wakiwa na imani na Serikali yao kwamba ina sera nzuri na zinazotekelezeka na sasa hivi Chama cha Mapinduzi kiko mtamboni kitaendelea kutekeleza majukumu yake. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye nyumba za Serikali. Nyumba za Serikali zilizokuwa zinasemwa hapa ni nyumba ambazo ziliuzwa wakati wa Rais wa Awamu ya Tatu akiwepo Waziri Mkuu ambaye ndiye mwaka jana alikuwa miongoni mwa watu wa mabadiliko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Sumaye ndiyo ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa wakati huo na ndiye aliyesimamia. Kama alifanya kazi mbaya basi muone kwamba mabadiliko mliyokuwa mnaenda kuyafanya ni mabadiliko hovyo…
MHE. JACQUILINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwasababu hata ambaye alipewa ridhaa ya kuipeperusha bendera ya CHADEMA kwa mwaka jana naye ni hovyo, fisadi aliyepindukia na pia ukija na Mheshimiwa Sumaye naye ni tatizo! Ndiye aliyeuza nyumba hizo kwa mipango mibovu!
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisiharibiwe muda kwa sababu sindano zinapoingia na wao watulie kama wao walivyokuwa wanaingiza sindano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua lazima Wananchi watambue wazi kwamba, hata katika suala ambalo kwa mfano tunachangia humu ndani, upande mwingine ni kelele maana yake ni madebe matupu na upande mwingine wanatulia kwa sababu wana hoja. Na niseme tu kwa upande wa wenzetu wa Upinzani kwa wanawake wanaoweza kujenga hoja ni watu wawili, Mama Sakaya na Upendo, lakini wengine the rest hamna kitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende kwenye hoja ya msingi sana. Pamoja na kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, naomba niende moja kwa moja kwenye barabara yenye urefu wa kilometa 124, barabara ambayo inatoka Likuyufusi kuelekea Mkenda. Barabara hii ni ya muda mrefu, Waheshimiwa Wabunge waliopita, Mheshimiwa Jenista Mhagama, dada yangu Stella Manyanya na Marehemu John Komba na wengineo walisimama imara sana kutetea hii barabara ili iweze kujengwa, lakini mpaka sass hivi barabara hii haijajengwa, ni barabara ambayo inaunganisha Msumbiji na Tanzania. Naomba Waziri mwenye dhamana, barabara hii iweze kuanza kujengwa kwa kipindi hiki cha mwaka 2016/2017, utakapokuja hapa wakati una-wind up tafadhali naomba ueleze bayana barabara hii inaanza lini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende kwenye barabara ya Morogoro - Ruvuma; mimi hizo kelele hazinibabaishi kwa sababu ninyi kwetu, kwa lugha ya kwetu tunawaita mazindolo. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ambayo inaunganisha mkoa wa Morogoro na mkoa wa Ruvuma, na sisi kwetu hatuna aibu Wangoni hawana aibu hata kidogo kwa hiyo, barabara hiyo inatoka Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha mpaka kufika Songea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja.