Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote nikushukuru kwa kunipa nafasi. Maelezo aliyoyatoa Mheshimiwa Bashe jana kwenye Bunge hili ni vitu viwili tofauti na uhalisia uliopo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Rukwa na mikoa yote ambayo inazalisha zao la mahindi, bei ilikuwa nzuri sana katika kipindi ambacho soko lilikuwa huria. Mkoa wangu gunia la kilo 100 lilikuwa likiuzwa shilingi 90,000 mpaka shilingi 95000. Hali halisi baada ya maelezo ya Mheshimiwa Waziri, leo hii Mkoa wa Katavi mahindi ni shilingi 50,000, shilingi 60,000. Kwa hiyo, ni anguko kubwa sana kwa wwakulima.

Mheshimiwa Spika, maelezo ambayo yanazungumzwa na wenzangu na maelezo ya Mheshimiwa Musukuma ambaye amesimama hapa, asilimia kubwa ya maelezo hayo ni wale ambao ni madalali, walanguzi ndio wanaokwenda watachangia hoja hii, lakini uhalisia kwa mwananchi mkulima ambaye anazalisha ana masikitiko makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, NFRA hawana uwezo wa kununua mahindi kwa sasa na masharti yao ni magumu mno. Hata hivyo, namba mbili, mfumo uliozungumzwa na Mheshimiwa Waziri haujafunguka mpaka sasa, ni vitu viwili tofauti vinavyozungumzwa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri asisahau, alisimama kwenye Bunge hili akauthibitishia umma kwamba hakuna mkulima yeyote atakayezuiliwa kuuza mahindi mahali popote pale. Alishasahau? Ni jambo ambalo linafanywa tofauti kabisa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wazo kwa mikoa ambayo tunazalisha zao la biashara ambalo sasa hivi tumeambiwa na Serikali na wao wenyewe wakatuhamasisha, zao la mahindi ni zao la biashara na ni zao la chakula…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa kengele imegonga.

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, kazi ya Serikali ni kununua mazao. Kama hawana uwezo wa kununua, waaachie wakulima wauze mahali popote pale wanapotaka. (Makofi)