Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niunge mkono hoja iliyotolewa. Hakuna mtu anayepinga mambo ya Wizara. Wizara ilitoa maelekezo kwamba wafanyabiashara watafute leseni, watafute TIN number ili waweze kufanya biashara zao vizuri. Elimu hiyo haijawafikia watu wengi. Kwa hiyo watu wanahangaika, wanatupigia simu kila mara, utaratibu upi ufanyike?

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kabisa tangu Mheshimiwa Bashe akiwa back bencher alikuwa ni mtetezi wa wakulima. Tunamwomba ajipambanue ili wakulima waweze kuuza mazao yao maeneo mbalimbali wanakotaka. Kwa sababu mpaka sasa hivi wakulima walikuwa tayari wamepata wateja kutoka maeneo mbalimbali katika mikoa mbalimbali. Kwa mfano, sisi Kigoma tuko mpakani walikuwa wanapata wateja kutoka Tabora, Musoma, Kagera na wengine kutoka Uganda. Tunaiomba Serikali iweze kutoa tamko, wakulima waendelee kuuza mazao katika sehemu mbalimbali. Hivyo basi, tunafahamu Mheshimiwa Bashe ni mkulima na anawapenda wakulima…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, tunaomba atoe mchanganuo ili wakulima waweze kunufaika kwa kuuza mazao yao nje. Ahsante. (Makofi)