Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii ili niweze kuchangia. Nitanukuu maneno ya Waziri wa Sekta. Ukifuatilia mjadala niliona kuna maeneo hivi ambayo yalikuwa yanaleta confusion kidogo. Kwa hiyo, naomba nisisitize ambayo Mheshimiwa Waziri wa Kisekta alisema, Serikali haijafunga mipaka.

Mheshimiwa Spika, nadhani tukiongelea kufunga mipaka, tukiongelea NFRA tunaleta mkanganyiko. Serikali haijafunga mipaka na hili Waziri wa kisekta alilisisitiza sana. Serikali imetoa utaratibu wa namna ya kuvuka hiyo mipaka. Vile vile, Waziri wa Viwanda hapa amesisitiza na ameonesha jinsi ambavyo masharti yale yamepunguzwa. Waheshimiwa Wabunge, kwa maana hiyo na jana Mheshimiwa Spika alitoa maelekezo, nadhani tungejikita sana kwenye kuhamasisha hawa wenzetu ambao wanauza hayo mahindi, wawahi wachukue hizo leseni na wapeleke hayo mahindi nje. Wanunue, kila mtu aende anunue, wala hatujafunga soko, wala hatujapunguza hiyo competition.

Mheshimiwa Spika, kila mtu aende achukue leseni, anunue na apeleke anakotaka kupeleka. Pia, tukishafanya hivyo ingekuwa ni vema sana tungekuwa tunajadili kama upatikanaji wa leseni ni mgumu, hilo ndilo lingetakiwa liwe jambo la mjadala na sio kuhusu mipaka kwa sababu mipaka iko wazi, lakini kuhusu leseni watu wachukue leseni.

Mheshimiwa Spika, niombe Waheshimiwa Wabunge tuelewane vizuri kwenye hilo. Serikali imekwenda kuwekeza na kuona kwamba potential ya nchi yetu iko kwenye kilimo. Nikiongea kilimo naongea kwa dhana pana ambapo kuna kilimo, mifugo na uvuvi. Kama huo ndio mwelekeo, ni vizuri sana tuendelee kuweka misingi ya kufanya urasimishaji kwenye eneo hili, vinginevyo tutawafanya watu wetu waumie, halafu hiyo nguvu yote, watu watakuwa wanajiingilia tu kama matunda ya mti wa barabarani, kila mtu anachuma na kuondoka ambacho sio kitu kizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu NFRA hiyo tumeongezea ushindani tu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Sekunde thelathini, malizia Mheshimiwa Waziri, kengele imeshagonga.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, tuimeongezea fedha NFRA ili na yeye aweze kununua. Ndio maana mwaka 2022 ilikuwa Sh.100,000 tu sasa hivi tumeenda Sh.400,000 na fedha hiyo imekwishapatikana. Kwa maana hiyo itakwenda kuongeza bei kwa mkulima na kuweka uhakika.

Mheshimiwa Spika, nadhani tuwaelimishe watu wetu, wawahi wakate hivyo vibali na waweze kuuza mazao wanakotaka kuuza.