Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wenzangu, nataka tu niwahakikishie, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Chama cha Mapinduzi haiwezi ku-institute sera wala utaratibu unaokwenda kummaliza mkulima. Hili ni jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, je, Serikali imezuia kuuza mazao nje? Jibu, Serikali haijazuia kuuza mazao nje. Pili, kuna hoja imesemwa na hata dakika tatu zikiisha naomba uniongezee nataka niongee pole pole kwa heshima, kwa unyenyekevu ili wanielewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfumo wa kutoa export permit unafanya kazi ama haufanyi kazi? Jibu, mfumo unafanya kazi. Jana peke yake tumetoa export permit zenye jumla ya tani 3,640 kwa siku moja. Toka tarehe Mosi mpaka siku ya tarehe 22 tumetoa export permit zenye jumla ya tani 32,000. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba mnielewe, kwa nini tumeweka utaratibu? Wiki iliyopita Wizara ya Kilimo tumepokea notice kutoka Mamlaka ya Afya na Chakula ya nchi ya jirani ikitu-notify kwamba mahindi yetu yaliyoingia kwao moisture content ni 18 percent. Mnataka tuue soko hili? Yaani nataka nijiulize hili swali, ni lini tunataka kuruhusu tuanze kufungua border tupeleke nje ikitokea condemnation moja tu inaua biashara yetu yote, na ni akina nani wanaopeleka? Siyo wafanyabiashara wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Aeshi yuko pale huwa ananunua mahindi Zambia, muulizeni lini kaenda kununua mahindi kama yeye? Lazima apitie kampuni ya Wazambia. Why do you want foreigners to come and go to our farms? Mnataka kuua small business? Yaani mtu atoke nje aingie kwenye mashamba ya nchi hii, aondoke na lori lake nimpe phytosanitary? sitampa phytosanitary, foreigner yeyote anayetaka kununua mazao ya Watanzania aingie asajili kampuni, aingie mikataba na makampuni ya Watanzania, hilo la tatu.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho. Ni hivi siwezi kuwa Waziri wa Kilimo ambae anataka mkulima akose soko la mazao ya chakula, tutayauza mazao ya chakula kwa utaratibu maalum. NFRA imefungua vituo, leo Magazeti yametangaza vituo 44 katika Mikoa minane na tumetangaza bei ya kununulia kati ya shilingi 600 mpaka 1,000 kutokana na kituo. Kuna hoja kwamba masharti ya NFRA siyo marafiki. Ni hivi, huko nyuma Serikali haikuwa na miundombinu ya kukaushia mazao. Tumeshafungua maghala manane na Mbunge wa Sumbawanga Mjini yule pale shahidi, katika kituo cha kwanza tulichoanza kununu mahindi nchi hii ni Sumbawanga Mjini. Tumenunua mahindi mpaka yana moisture ya 15 tunayaingiza kwenye mashine tunayakausha, ile asilimia tatu inayopotea tunaiongeza kwenye cost of our production, hatuendi kuchambua.

Mheshimiwa Spika, tumewaagiza NFRA mkulima akifikisha mahindi kwa kuwa tunajua wakulima wetu wanapovuna huwa wanapiga kwa fimbo yanakuwa yana uchafu, ten to 15 percent ya hayo mahindi yanakuwa yana uchafu. Tumewaagiza NFRA chukueni mahindi kwa wakulima, kwa kuwa Sumbawanga Mjini, kwa kuwa Manyara, kwa kuwa Katavi, haya maghala na vihenge vimekamilika, tutayapeleka hayo maeneo hayo, tutayakausha yatakuwa na moisture inayotakiwa, tutayasafisha ten percent wastage tunayoipata tunaiingiza kwenye gharama yetu ya ununuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge na ninataka nitumie nafasi hii kuwatangazia wakulima, usiuze mahindi yako kama uko Mkoa wa Katavi chini ya shilingi 800, usiuze mahindi yako kama uko Kiteto chini ya shilingi 800, usiuze mahindi yako kama uko Sumbawanga chini ya shilingi 800 na Serikali inachukua hatua hii ya kutoa bei elekezi ili competitors wote wanapotaka kuyanunua mahindi wayanunue juu ya bei ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja ya CPB.

SPIKA: Haya Mheshimiwa malizia dakika moja.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kama kuna changamoto tutazirekebisha, kama kuna changamoto lakini tukubaliane asisafiri mtu yeyote kutoka Mkoa mmoja kwenda Mkoa mwingine kama hana leseni ya biashara. Hii dhana ya kuwafanya wafanyabiashara na Watanzania walioko kwenye sekta ya kilimo kulitumia neno “wanyonge” neno wanyonge lisitumike kuhalalisha mambo ya ajabu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe sana, tutarekebisha kama kuna changamoto kama kuna difficulties za mfumo tuliouweka tutaupitia lakini hatujafunga mipaka, hatutafunga mipaka, lakini hatutaruhusu mtu yoyote kutoka nje kuingia shambani anunue kupitia Watanzania, asajili kampuni na yoyote anayetaka ku-trade a-trade kwa mujibu wa sheria za nchi hii na walioingia mikataba na CPB Mheshimiwa Mbunge wa Iringa Mjini…

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri, malizia.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, waliolipa fedha kwa CPB wana mikataba, na mikataba imeonesha kwamba wametoa benki, wale wamekuwa wajanja, walisaini mikataba ya bei ya juu walivyoona mavuno yameanza wanataka kurudi ku-renegotiate, wameshasaini mkataba fedha hazitarudishwa, watayachukua mahindi kwa bei ya shilingi 900 waliyosainia mikataba na tumeshawapa CPB export permit wawape hivyo vibali vya kupeleka nje, lakini watapeleka nje kwa bei ya mikataba tofauti na hapo hatutaruhusu. (Makofi)