Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya uchache wa muda tuliopewa, kwanza kabisa nitumie nafasi hii kukushukuru sana wewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu katika Bajeti Kuu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, tukiwa kama Wabunge sisi tuna nafasi ya kusema vitu ambavyo vinatoa direction ya nchi. Kwa dhati ya moyo wangu niseme mafanikio yote tunayoyazungumza ya Serikali ya Awamu ya Sita katika Nyanja za kiuchumi, kijamii, kisiasa, nataka niseme kwa dhati ya moyo wangu, sisemi kwa sababu Waziri huyu wa Fedha ni kaka yangu. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba kaka yangu nataka niseme kwa dhati ya moyo wangu umeitendea haki sana Serikali ya Awamu ya Sita katika masuala mazima ya usimamizi wa fiscal policy and monetary policy na ndiyo maana tunapoangalia hali ya uchumi wa nchi za Afrika ya Mashariki ukiangalia masuala mazima ya inflation, bei za vyakula na bidhaa Taifa la Tanzania ndilo nchi peke yake stable katika mataifa yote ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa credit kama hizi hatuwezi tukaku-ignore kaka yangu Mwigulu. Niseme kwa dhati ya moyo wangu, unamfanya Rais wetu kuwa proud, na sisi kama Wabunge tunalisema mchana kweupe, wewe ni moja ya mawaziri bora kabisa kuwahi kutokea katika sekta ya fedha katika nchi yetu, keep it up kaka yangu kaza Kamba kazi iendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nalotaka kulisema; kuna maneno mengi yamesemwa mtaani, kuna watu wamefikia hatua ya kutaka kuligawa Taifa, na hili nalisema kwa sababu ni Bajeti Kuu ya Serikali. Rais anahangaika kutengeneza base za kuleta kodi kwenye nchi, uwekezaji unaozungumzwa, Rais wetu anahakikisha ili tuache kukimbizana na mikopo Taifa liwe na revenue zake. Rais amefanya mipango kupitia Serikali, tunao watu wa DP World. Kuna watu wamekwenda kusema nchi imeuzwa. Mimi nataka nisome vipengele vya kisheria ambavyo vinaonesha upotoshwaji uliofanywa mtaani ulikuwa ni makusudi na lengo la kuchafua na kuleta instability ya umoja wa kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Article One ya Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai ukurasa wa 9 katika land right; kwa sababu unaposema nchi inauzwa unamaanisha tumeuza mamlaka ya nchi na tumeuza ardhi. Article 1 inasema “land right shall mean all those rights excluding the right of ownership of land”, huu mkataba. Sasa hoja ya kusema nchi imeuzwa inatoka wapi? mkataba unasema right of ownership, exclusion imewekwa kwenye right ya ownership ya ardhi. Acheni kudanganya watu, achene kuchafua nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu Rais hawezi kuliuza hili Taifa na ndiyo maana ni Amiri Jeshi Mkuu. Tumemwamini, tumempa madaraka na hafanyi maamuzi kwa sababu ni Mzanzibar. Nataka niwaambie, Mzanzibar ana haki ya kuwa Waziri kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano na hatma iko kwenye muungano huu. Haiwezekani tukaanza kuleta mambo huyu Mzanzibar, tutavunja muungano wetu. Tunaomba wanaofanya hayo wakome mara moja Mama apewe maua yake kwa kuleta kampuni hii kuja kufanya uwekezaji utakaoleta tija katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine na mambo mengine kwenye mkataba wamezungumzia article 22 wanasema mkataba huu tumejifunga, amendment zimezungumzwa kwenye article 22. Jambo lingine wamesema mkataba huu, sheria sijui tukishtakiana wapi article 21 imesema governing laws zitakazotumika ni za Serikali ya Tanzania. Mheshimiwa Waziri nataka niwaambie kafanyeni kazi, sisi kazi yetu tulihaidi, sisi ndiyo tuna Ilani, msitishwe na mtu, tunawaunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ninalotaka kumshauri kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu na Serikali. Wananchi wetu na viwanda vimekuwa vikilalamika, bei ambayo imekuwa ikitozwa katika electronic stamp imekuwa ikisemekana ni kubwa. namshauri Mheshimiwa Waziri kwa nini wasiwaite wawekezaji wa SICPA wakae nao, wawaombe washushe bei ili kusudi wafanyabiashara waweze kuwa na manufaa katika gharama hizi zinazozungumzwa. Najua wamefanya kazi kubwa pamoja nao ya kizalendo, mapato ya Serikali yameongezeka, uchumi wa Taifa unakua, miradi inaendelea kuwa financed kwa sababu ya mapato anayokusanya kaka yangu. Wakae na watu wa SICPA, wazungumze nao ili washushe gharama…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, nakuomba radhi sana dada yangu. Jambo la mwisho nataka niseme kama alivyosema kaka yangu Kwagilwa Mama Samia apewe maua yake. Ripoti zinaonyesha mwaka 2001 net in flow ya foreign direct investment ilikuwa asilimia moja. Mwaka mmoja baada ya Mama kuingia madarakani ikapanda mpaka 1.4

Mheshimiwa Spika, UNCTAD wametoa ripoti wanaonyesha uwekezaji kwenye Taifa umeongezeka kwa asilimia 34, ripoti ambazo alikuwa anasema kaka yangu, inaonyesha kwamba Taifa limepanda katika ratio za kimataifa katika masuala mazima ya kiuchumi. Nani kama Mwigulu jamani? Hivi kweli tutasema hatuna Waziri imara wa Fedha. Naomba kaka achape kazi, Wabunge tunamuunga mkono, Rais tuko nyuma yake, waharakishe katika uwekezaji wa bandari, wasitishwe, tutatoka hapa, tutakwenda mtaani, tutawaeleza wananchi umuhimu na manufaa ya uwekezaji huu kwa maslahi ya Taifa letu, ahsante sana. (Makofi)