Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi niweze kuchangaia katika bajeti iliyoko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza kwa maombi. Ombi langu la kwanza niliuliza swali siku moja hapa ni kwa kiwango gani Mkoa wa Kagera unachangia kwenye Pato la Taifa, nilijibiwa kwamba tunachangia kwa asilimia 2.3 na swali langu la nyongeza nilisema hatutendewi haki kama Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kagera ina rasilimali za kutosha na inaweza ikachangia sana kwenye Pato la Taifa na sababu kwa nini haichanagii, Moja, hakuna viwanda lakini tunazo rasilimali za viwanda. Ni kazi sasa ya Serikali kuvutia wawekezaji kwa kuweka zile pull factors, kupunguza kodi kadha wa kadha lakini na masharti ya uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni miundombinu na ndiyo ninachotaka kuongea leo. Ninaiomba Wizara kwa namna ya pekee, tunaomba barabara ambayo inaenda Murongo kutokea Mugakorongo iweze kutengewa na kupatiwa fedha sasa wananchi walipwe fidia na barabara ianze kujengwa. Barabara ya pili ni barabara ya Omurushaka ambayo ni Bugene kuja Nkwenda kuja Kaisho mpaka Murongo. Tuweze kuunganisha hizi barabara mbili tuweze ku – boost uchumi wa Mkoa wa Kagera na sisi tutafurahi kupitia kahawa, kupitia mahindi, kupitia mazao yote ambayo kama Mkoa tunazalisha, tuweze kuchangia hata asilimia 10 kwenye pato la Taifa. Uwezo huo tunao, tuna misimu ya mvua miwili na mambo kadha wa kadha.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nitaongelea. Tunaongelea bajeti leo ambayo ni ya trilioni 44 point something, lakini ukiangalia ile bajeti ya trilioni 44 point something, bajeti ya fedha za maendeleo imeshuka. Ukiangalia bajeti ya trilioni 41 fedha ya maendeleo ilikuwa juu kidogo ilikuwa ni trilioni 15 lakini leo tuna bajeti ya trilioni 44 lakini fedha za maendeleo zinakuja kwenye trilioni 14. Unaona kwamba kuna kushuka, sasa hatuwezi kuji–confine kwenye kutumia ni lazima tuji–confine kwenye kuendeleza vitu tulivyonavyo, kujenga barabara na vitu kadha wa kadha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunchopaswa kufanya ni kuanza kama siyo kufunga mkanda basi ni kuongeza tax base na hilo ndiyo nataka nilitoe. Bajeti ya sasa inaonesha kwamba asilimia 68 itaenda kwenye matumizi, hiyo nadhani haiko sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho wengi wameeleza na mimi nieleze, nimpongeze pia Mheshimiwa Rais amefanya kazi nzuri sana, lakini katika kumpongeza Mheshimiwa Rais ni task kwenu. Alichokifanya Mheshimiwa Rais ndio alichokifanya Yesu siku ya Alhamisi Kuu aliwanawisha miguu Mitume baada ya ya kuwanawisha miguu wakasema nenda fanya na kwa wengine. Rais alivyozindua Royal Tour hakumaanisha yeye aendelee kuandaa Royal Tour na kufanya films. Alitaka ninyi wasaidizi wake nendeni mfanye kama alivyofanya yeye, amefanya mara moja ameweza ku-boost sekta ya utalii zaidi ya asilimia 109 kwa utalii wa ndani, lakini pia na utalii wa nje umekua kwa zaidi ya asilimia 59. Ninyi ambao mmeoneshwa ninyi mitume mmefanya nini? Hilo ni swali kwenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ninalolileta kwenu. Bado tuna nafasi ya kufanya kwa ajili ya kuongeza, mimi lengo langu ni tuweze kukusanya zaidi. Nimesikitika Halmashauri zetu zaidi ya 180 kushindwa kukusanya hata trilioni moja. Leo projection imeonesha twende mpaka trilioni moja point something, lakini kwa Halmashauri nyingi tulizonazo kushindwa kukusanya trilioni moja siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ina maana na ukweli ni kwamba hela inapatikana kwa watu masikini lakini fedha inavuja. Mheshimiwa Waziri umeeleza Mama Samia, Mama yetu hapendi rushwa na ameagiza watu wale waliohusika kwenye ufisadi washughulikiwe. Tunataka taarifa kamili watu wote waliohusika kwenye Halmashauri kutorosha fedha mbichi, kutorosha fedha za hao walipakodi, wameweza kushughulikiwa kwa kiwango gani ili tuweze kupunguza kukopa? Hilo ndilo nalileta kwenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri mambo yafuatayo: -

Kwanza; kama Wizara au Serikali lazima m–build trust kwa walipa kodi. Siyo ku–build trust lakini m–prove kwamba kodi mnazokusanya zinatumika sawasawa. Huo ndio ushauri wangu wa kwanza. Kwa kuziba mianya yote ya kodi.

Pili; ni lazima tuwe na mfumo wa ukusanyaji kodi ambao ni rahisi na rafiki kwa kila mtu.

Tatu; ni lazima twende kwenye digital kwenye kukusanya mapato. Tumeongelea suala la TAUSI kwenye Halmasahuri, ni kwa kiwango gani halmashauri zimekuwa zikitumia Mfumo wa TAUSI katika kukusanya mapato. Tumeendelea na mifumo ambayo ni manual inaruhusu watu kuendelea kuchezea mapato ya Serikali, siyo sawa. (Makofi)

Nne; ni lazima tuongeze tax base. Huu mfumo ambao nimekuwa nikieleza mara nyingi wa 28 rules inasababisha watu wakwepe kulipoa kodi. Moja, walipakodi ni wachache na wanapaswa kutoa mzigo mkubwa, kwa hiyo lazima watakwepa. Tutengeneze mfumo ambao katikati walipakodi ni wengi. Walipakodi wawe wengi na kodi zitakuwa nyingi lakini hapo hapo tuondoe mianya ya usumbufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kuna changamoto ya compliance kwa sababu ya ugumu. Tuliongelea blue print hapa kwa nini hamjaleta blue print ili tuweze kupunguza urasimu, usumbufu katika ufanyaji wa biashara hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo ni machache nakushukuru, muda ni mchache sana. (Makofi)