Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya kuboresha uchumi na maisha bora kwa Watanzania. Kwa hakika naomba nifanye nukuu kutoka kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri na nimekuwa nikilisemea hili kwamba Mama Samia anapiga kote kote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo anafanya miradi mikubwa na midogo, wakati huo huo wastaafu wanapata stahiki zao, wafanyakazi wamepandishwa madaraja na wamelipwa mishahara. Hakika Mama anastahili maua kama alivyosema Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba. Vile vile, tunasema Mama yuko kazini na kazi inaendelea. Pia, wale ambao waliofikiri Mama Samia hawezi, hakika wameona anakwenda anafukunyua, anaibua ili kuhakikisha kwamba anafanya kazi yake sawasawa. Kwa hiyo, niwaombe Watanzania waelewe kwamba hakuna wakati wa kumpangia. Kuna wakati watasema ana–copy na ku–paste kwa sababu wanawake hawawezi, Hapana, wanawake tunaweza, tuna–initiate, tunabuni na tunasogeza. Mama yuko kazini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie bajeti hii ya 2023/2024. Niipongeze Serikali kwenye suala zima la kuongeza mapato. Nitachangia vipengele viwili vya ukurasa wa 27 na ukurasa wa nane kwenye Mapato na Uchumi wa Kidigitali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali, Desemba, 2022 waliweza kufanikiwa kukusanya zaidi kwa kupata trilioni 2.53 ambazo hazijawahi kutokea kukusanywa, zimekusanywa kipindi hiki cha Mama Samia Suluhu Hassan. Vile vile, Serikali imekiri kwamba mafanikio yale yalitokana na kuboresha mifumo. Hata hivyo, bado naamini na Serikali inaamini hivyo kwamba tunaweza kukusanya zaidi mapato yetu ya ndani. Pia, wengi wamezungumza hapa kuhusu suala zima la kuongeza mapato ya ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nishauri kwenye suala zima la uchumi wa kidigitali. Sasa hivi Serikali imebuni lakini tunategemea EFD machine pekee katika kuhakikisha kwamba tunakusanya kodi. Hata hivyo, kwenye EFD tunajua kulingana na baadhi ya Watanzania ambavyo walivyo, hawataki kulipa kodi utakuta mtu amenunua kitu cha 100,000 anapewa risiti ya 10,000 au wakati mwingine hapewi risiti kabisa. Sasa, nini kifanyike kuhakikisha kwamba automatic by default mfanyabiashara atahakikisha analipa kodi? Nafikiri ni increase visibility ya cash flow ya mfanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Taifa tunaweza kujua kila simu ya Mtanzania inayoingia imepigwa kwa dakika ngapi na shilingi ngapi, nina hakika kabisa kwa kutumia uchumi wa kidigitali, tunaweza kujua cash flow ya kila mfanyabiashara nchini. Pia, iwapo cash flow yake itakuwa visible, there is no way huyu mtu atakwepa kulipa kodi, atalipa kodi accordingly.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa kutumia uchumi wa kidigitali, naomba sana tu–encourage kulipa malipo kwa Lipa namba, tu–encourage kuhakikisha VISA Card zinatumika, tuhakikishe kwmba tuna–discourage malipo ya cash (cash money isitumike katika kuhakikisha tunafanya manunuzi). (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapokuwa tunalipa cashless kwa kutumia card, tuna increase visibility ya cash flow ya biashara yoyote ile nchini. Pia, itakuwa ni rahisi ya kuhakikisha kwamba mfanyabiashara analipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niishauri Serikali kuhakikisha kwamba inaweka utaratibu na mikakati ya kuhakikisha kwamba Watanzania hatulipi fedha taslimu (tunalipa kwa kutumia lipa namba na tunalipa kwa kutumia VISA Card). Of course, mwanzoni tutahitaji elimu, lakini hata mbuyu ulianza kama mchicha. Naamini Tanzania imeweza kubuni mambo mengi na ndio sababu tumeweza kusogea. Hivyo, hili pia linawezekana, tu–increase visibility ya cash flow ya mfanyabiashara yeyote yule, ni solution pekee ya kuhakikisha kwamba kodi inalipwa. Vile vile, through EFD only bado kodi inakwepwa. Hilo ni la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 43 umezungumzia uwezeshaji, viwanda na biashara. Sasa, wakati Serikali inasema imeendelea kuboresha mazingira ya kibiashara, nimekuwa najiuliza, kwa nini viwanda ambavyo vimekwishaanzishwa vinakufa? Serikali imefanya tathmini gani katika viwanda ambavyo vinakufa ili kuhakikisha havifi na vinasaidia kusimama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kule kwetu Tanga, mimi roho inaniuma sana. Kiwanda cha Kutengeneza Mazulia ambacho kipo Tanga Mjini kimekufa wakati sisi ndio tunazalisha mkonge. Kwa nini Serikali haikuona haja ya kuweka juhudi kuhakikisha kiwanda kile hakifi? Kwa nini kule Lushoto Kiwanda cha Usambara Factory ambacho kinatengeneza tomato na nyanya zinazalishwa Lushoto, kwa nini kiwanda kile kimekufa? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali watakapokuja ku–windup watupe kwa nini viwanda hivi vimekufa na Serikali wamefanya juhudi gani kuhakikisha viwanda hivi havifi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)