Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia. Nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja iliyoko mbele yetu ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa nafasi. Pili nimshukuru sana Waziri wa Fedha na Wizara ya Fedha kwa ujumla. Katika Hotuba ya Waziri wa Fedha, katika mpango wa mwaka ujao wa fedha amesema wazi kabisa, katika miradi ya kielelezo na miradi ya kipaumbele, miradi ya umwagiliaji itakuwa ni eneo la kwanza ambalo Serikali itaweka fedha. Nitumie nafasi hii kumshukuru sana. Vilevile nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa guidance anayotupa na maelekezo anayowapa wenzetu wa Wizara ya Fedha kuangalia uwezekano wa kuweza kuweka kipaumbele katika eneo hili la kilimo namshukuru sana Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge, wametoa ushauri na wamesema mambo mengi. Kwanza nitumie Bunge lako Tukufu kuwaambia kwamba kwa mara ya kwanza tangu tumepata uhuru uzalishaji wa zao la kahawa tumefika metric tons 82,000 ambazo tumeziuza mwaka huu. Vilevile zao la tumbaku uzalishaji wetu sasa hivi unakwenda tani 120,000. Hizi zote ni effort ambazo Mheshimiwa Rais amefanya na tunaendelea na masoko na masoko yanaendelea vizuri tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hali inavyokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wengi wameongelea eneo la mafuta ya kula na eneo la ngano. Nataka nitumie nafasi hii kuwaambia Waheshimiwa Wabunge tumewasikia na tumekaa na Wizara ya Fedha tumekubaliana tutakuwa na tax measures na tutakuwa na administrative measures ambazo zitaonekana kwenye finance bill ambazo zitafanya uzalishaji wa mafuta tuweze kuwa na tax ambazo zinaweza kumlinda mkulima. Serikali inaweka fedha tumegawa mbegu nyingi sana za ruzuku na safari hii mashamba yetu yote ya kuzalisha mbegu yatakuwa yanatumia pivot technology. Mwenyezi Mungu akitujalia mpaka kufika mwishoni mwa mwaka huu baadhi ya mashamba ambayo yamefungwa mifumo ya umwagiliaji ya kutumia technology ya center pivot yataanza kufunguliwa ili tuweze kuzalisha mbegu mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo nataka niseme kwamba Waheshimiwa Wabunge wameongelea sana suala la tija. Ni ukweli kwamba mchango wa sekta ya kilimo na ukuaji wa sekta ya kilimo hauakisi tamaa tulionayo kama Taifa. Ili tuweze kufikia huko ni lazima tuwekeze kwenye tija. Serikali inafanya jitihada kubwa sasa hivi ya uwekezaji kwenye maeneo ya kuongeza tija. Mmepitisha bajeti ya Wizara ya Kilimo na Bajeti Kuu ya Serikali; na mwaka kesho mtaona tunaanza kutekeleza miradi katika majimbo yenu ya kuchimba visima kwa ajili ya wakulima wadogowadogo na kuwawekea irrigation kit ya hekari 2.5 kila mkulima ili wakulima waweze kuzalisha kwa wingi na waweze kuwa na uhakika wa kuzalisha kuwa na resilience kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni uwekezaji, tumeshatangaza tender sasa hivi za kufanya feasibility study na detail design kwenye mabonde yote 33. Na ninawashukuru Wizara ya Fedha kwa kutupa kibali. Tumeshatangaza tender na mikataba imeshasainiwa wakandarasi wanaanza kufanya feasibility study kwenye mabonde ya Ziwa Victoria, Lake Tanganyika Lower Basing ya Ruvuma na mabonde ya Rifiji. Yote haya tunayafanyia detail design ili tuweze kuanza mipango ya kujenga miradi ya umwagiliaji ili Mwenyezi Mungu akitujaalia tukikamilisha hizi zaidi ya hekta laki tatu na kitu zitatuongezea eneo kubwa la uzalishaji wa mwaka mzima katika maeneo tunayofanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine Wabunge waliongelea pamba, wakatoa concern yao kuhusu bei. Nataka niwakumbushe mwaka 2020/2021 tulianza msimu kwa bei ya shilingi 800 tulimaliza msimu kwa bei ya 1200. Mwaka 2021/2022 tulianza na msimu kwa bei ya shilingi 1500 tukamaliza msimu na bei ya shilingi 2200. Mwaka huu tumeanza na bei ya 1060 ninaamini kwamba bei ya pamba itaimarika namna ambavyo competition inavyoongezeka na soko la dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, njia pekee ambayo tunaongea na wenzetu wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha, ni kutengeneza mfumo ambao utatufanya sisi wakati wakulima wanalima, wanavuna, wanapata assured good price na tunahifadhi, tunaenda katika mfumo wa TMX na kuangalia namna gani tutawasaidia waongezaji wa thamani, waweze kuongeza thamani ya pamba yetu na kutengeneza financing scheme. Tuko kwenye majadiliano na Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara, naamini ndani ya miaka miwili, mitatu tutafika katika eneo hilo. Hii ni safari haiwezi kutokea haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tamaa yetu ya kuwa na stabilization fund, kama mtakumbuka mwaka jana wakati tunapitisha Finance Bill tulianzisha Agricultural Development Fund hapa ndani ya Bunge. Sasa hivi tuko hatua za kukamilisha kanuni ambapo tutakuwa na Mfuko wa Fedha ambao unatumika kwa ajili ya kuwalinda wakulima wetu na changamoto za masoko ili pale ambapo wanapata hasara tuweze kuwa–cover. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo na mlimsikia akiwa Mwanza, alitoa maelekezo ya kuiongezea fedha National Food Reserve Agency, tumepata approval ya bilioni 320 na tumeshaanza kuzitumia hizi fedha. Nawashukuru sana Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tunaweka fedha kwenye National Food Reserve Agency? Pia sasa hivi tumetangaza feasibility study kwa ajili ya kuongeza uwezo wetu wa kuhifadhi. Mpango wa Serikali katika kipindi cha miaka mitano mpaka minane ijayo tuwe na uwezo wa kuwa na maghala ya kuweza kuhifadhi mazao yasiyopungua tani milioni saba ndani ya nchi yetu. Kwa kutumia njia hiyo ndiyo tutaweza kuwalinda wakulima wetu na kuweza kujiwekea usalama wa chakula katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetupatia fedha kwa ajili ya Kampuni ya Serikali na niwapeni good news, tulifanya majaribio TFC na Profesa Mkenda ametoka nataka nimshukuru mbele ya Bunge hili, akiwa Waziri wangu ali–champion hili jambo. Leo TFC tumeipatia fedha, baada ya kuipatia fedha imefanya biashara ndogo na imepata faida. Matokeo yake Wizara ya Fedha wametuelewa, wametupatia bilioni 40 kwa ajili ya kuipa TFC na tumepata dola milioni 25 kwa ajili ya kuipa TFC na sasa hivi TFC imeshaagiza mbolea kutoka nje ili tuwe na mbolea ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndoto ya nchi kuwa na blending facility ambayo Serikali ina share, TFC sasa hivi tuko kwenye maongezi ya mwisho na OCP, lakini niwahakikishie Wabunge tusipoelewana na OCP tutawekeza wenyewe facility ya ku–blend mbolea ndani ya nchi na tutafuta wawekezaji wa Kitanzania kuwakabidhi waweze ku–run hilo eneo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie wakulima wa korosho, nimesikia kilio cha kwamba mfumo tuliouweka na equation tuliyoiweka ya miche 100 kwa mfuko mmoja tumeshawaagiza Bodi ya Korosho wafanye review na mgao wa pili utakapotoka watatoa kutokana na idadi ya mikorosho na ukubwa wa mikorosho. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge wa korosho, wakulima sasa hivi wanapokea pembejeo kwa kutumia teknolojia ya biometric, tuendelee kuwahamasisha wajisajili. Akijisajili akiwa na namba yake hata wakati wa kuuza korosho atauza korosho kwa kutumia namba yake aliyosajiliwa nayo ili tuwaondoe hawa wote ambao wanachukua mazao ya wakulima katika kipindi hiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo Wabunge wamekuwa wakisema sana. Wabunge wa Nyanda za Juu Kusini, naomba niwahakikishie, Wilaya ya Makete msimu ujao ngano tunawapa ruzuku ya tani 1,000 kwa ajili ya kwenda kufanya pilot. Wamefanya majaribio na niishukuru Halmashauri ya Makete kutoa ten percent kuwapa wale wakulima katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwaombe tu Waheshimiwa Wabunge matarajio tuliyonayo, Rais ana nia na Wizara ya Fedha imekuwa flexible kwa ajili ya kutoa fedha. Ndani ya miaka miwili, mitatu tutayaona matokeo makubwa katika sekta hii kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru sana. (Makofi)