Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi na kwa sababu ya muda nitakuwa brief sana. Nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa aliyofanya kuongeza tija kwenye kilimo. Ya kwanza, tumeona bajeti imeongezeka sana, kutoka bilioni mia mbili karibu na tisini na kitu mpaka bilioni mia saba na hamsini na kitu. Hilo kwa kweli ni a right step in right direction. Nimpongeze pia Mheshimiwa Rais kwa kazi za alizofanya Dubai Expo, tumeona mikataba mingi imesainiwa ya kuongeza tija katika kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze pia Waziri wa Kilimo, ndugu yangu Mheshimiwa Bashe; Naibu Waziri, Mheshimiwa Mavunde; Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na timu nzima ya Kilimo kwa kazi kubwa wanayofanya. Kwa kweli tumeona a revival ya kilimo na tunategemea mengi sana zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto ni food basket na nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa sababu alitembelea Kiteto. Nilikuwa nasoma taarifa hapa lile ghala la Ngusero ambalo liko chini sana asilimia 16 na anajua kwa nini iko hapo kwa sababu ya mkandarasi aliyekuwepo, Mheshimiwa Waziri a-push ili tumalize hili ili wananchi wa Kiteto wakapate kuhifadhi mahindi. Kiteto ripoti zake ukizisoma ile post-harvest loss ni karibu 40%, kwa hiyo hii itatusaidia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana pia Mheshimiwa Waziri, wananchi wa Kiteto wamefarijika sana kwa kilo 25,000 alizogawa za mbegu ya alizeti. Big up kwake, wananchi kwa kweli wamefarijika sana. Nakushukuru vilevile kwa kazi inayoendelea sasa ya kuhamasisha watu kuhusu alizeti. Kwa kweli tumeshajiwekea mkakati kama Taifa kwamba ili tuweze kupata mafuta ya alizeti hapa nchini, ni lazima tupate mbegu nzuri na vilevile wananchi wa Kiteto wako tayari…

TAARIFA

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mzungumzaji kwamba Mheshimiwa Waziri asithubutu kuruhusu GMO. Akiruhusu GMO ataua kilimo chetu kwa sababu tutategemea teknolojia ya kigeni, ni unyonyaji kwa wakulima na tutapoteza asili ya mimea. Kwa hiyo Waziri asiruhusu kabisa suala la GMO kwenye nchi yetu ya Tanzania. Ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ole-Lekaita, taarifa hiyo unaipokea?

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa sijaongelea mambo ya GMO, but I agree with her. Ni kweli alishasema Mheshimiwa Waziri hapa siku moja na biashara ya GMO ni biashara kubwa sana, ina issues nyingi sana, inahitaji mjadala mkubwa wa kitaifa, kwa hiyo nakubaliana naye sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nazungumza kuhusu Kiteto na jinsi wakulima wangu walivyo tayari kwa ajili ya kuzalisha mafuta na mbegu za alizeti. lakini wanachotaka ni kitu kimoja tu, Serikali iweke mkakati tujue price ya alizeti ili tuhamasike tujue kabisa projection ya prices mwakani zikoje ili wananchi waweze kuhamasika. Nadhani tukifanya hivyo itamshawishi kila mtu na ataingia kwenye kilimo hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana kwenye hotuba ya bajeti ya Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 130, walisema walikuwa na nia ya kuwawezesha vijana 400 katika mikoa tisa na Manyara ikiwemo. Nilipiga mahesabu ni karibu vijana 45 kila mkoa na ukipiga mahesabu ya wilaya zile Kiteto ilikuwa inapata vijana sita sio chini ya sita. Sasa nataka Waziri atujibu hili wameshalifanya kwa sababu sisi Kiteto hatujasikia popote, vijana wale sita ambao walitakiwa kuwawezesha kuwapa zana hizi, nataka nisikie kwenye hitimisho. Tusije tukakaa tunapitwa, kwa hiyo please, comment on this.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii inaongelea sana kuhusu umwagiliaji na ni kweli is a shame as a country kwamba projection ukiangalia data za umwagiliaji tuko chini sana, less than 2. 5 %...

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

TAARIFA

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mzungumzaji kwamba pamoja na hao vijana ambao wamemtaka Mheshimiwa Waziri katika hitimisho lake aseme chochote, wako vijana kwa ushirikiano wa Tanzania na Israel kila mwaka kama 100 wanaenda Israel kujifunza mambo ya kilimo lakini wakirudi hapa wanabaki idle.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ole-Lelekaita, taarifa hiyo unaipokea?

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea.

MWENYEKITI: Malizia, dakika moja.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa sababu ya muda naendelea kuzungumzia kuhusu suala la umwagiliaji. Ni kweli wameweka pesa nyingi kutoka bilioni 17 mpaka bilioni 51, fine, lakini tunapoteza maji mengi sana wakati wa mvua, tusipofanya hii, nadhani tungekuwa na like a rapid fund fulani ili mvua zinapotokeza tusipoteze maji kwa ajili ya umwagiliaji. Tukifanya hivyo tukawa quick itatusaidia tusipoteze maji mengi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda, niishie hapo lakini kwenye umwagiliaji vilevile kama tunataka kufanya vizuri zaidi, mashine zile zinazotusaidia kwa ajili ya umwagiliaji, Mheshimiwa Waziri apiganie ili kodi ziondoke ili wananchi wapate encouragement.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kabisa kabisa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)