Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba pia nianze kwa kuwapongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara, wanafanya kazi yao vizuri. Kwanza naunga mkono hoja na ninaipongeza Serikali kwa ongezeko la bajeti ambalo limefanyika mwaka huu karibu asilimia 255, lakini pia dhamira ya dhati ya kutaka kuleta mabadiliko kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijazungumza ninayotaka kusema, nataka nimkumbushe Waziri, mezani kwake kuna andiko la Ibanda Irrigation Scheme, ambalo lilikuja ofisini kwake mwaka 2021. Ni imani yangu kwamba utekelezaji wa mradi huu utaanza mwaka huu. Mradi huu sisi Halmashauri ya Mji wa Geita tumekubali kwa niaba ya wananchi kutoa takribani Shilingi milioni 500 kusapoti Serikali ili mradi huu uweze kuanza. Kwa hiyo, tunaomba wasituangushe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nataka Mheshimiwa Waziri wakati ana-wind-up aniambie kuhusu ginnery ya Kasamwa na mkakati wa Serikali wa namna ya kuifanya ifanye kazi. Tunazo ahadi za takribani miaka sita, lakini tunaona hakuna kinachoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, juzi nilitembelea Morogoro, palikuwa na Maonesho ya Kilimo. Naomba kumpongeza Mheshimiwa Waziri, nilikutana na wadau wake wengi. Nilikutana na PASS nikakutana na TADB, nikakutana na watu wanajiita TACT na wengine wanajiita Tanzania Agriculture Trust Input Funds. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumza na Mheshimiwa Waziri, nitatamani ajaribu kutuonesha mchango wa haya mashirika yake yote kwenye kilimo. Nilizungumza na watu wa PASS ambao wanamchangia mkulima asilimia 20 mpaka asilimia 60 na asilimia 40 benki, lakini mkulima huyu akienda benki, anakwenda kukutana na commercial loans ambazo interests zake siyo rafiki wa mkulima. Ukienda TADB wanakopesha mpaka 75 percent halafu nyingine inayobaki ni ya kwako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu hapa ikawa, hivi hii 25 percent kwa nini isitafsiriwe kwenye value ya land ya shamba ili nikiwa na heka zangu 100, hiyo 25 percent wanipe 75 percent kwa sababu tayari value ya land inaweza ikafidia hilo eneo. Sikupata majibu sahihi zaidi. Nilikutana na wengine wanaitwa TACT (Tanzania Agricultural Catalytic Trust), hawa ni private firm hawajulikani sana, lakini ukiwasoma ni kama vile wame-centralize, wako Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hoja yangu hapa ni nini? Ukikopa leo Tanzania Agricultural Development Bank, wakikupa mkopo, kwa sababu mkulima wa Tanzania analima kwa hali ya hewa, mwakani usiporejesha kulingana na schedule waliyokupa, watakutembelea, watakuuliza sababu, na wata-restructure mkopo wao, kwa sababu interest yao siyo kuuza. Pia katika kipindi chote watakupa ile technical support na kukutembelea na kukufuatilia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shida kubwa uliyonayo kwenye Agricultural Trust Input Fund, wanajifungia ofisini, nami sijui kama huwa mnapima wamefanya nini kwa mwaka? Kwa sababu mimi sijawahi kuona wanachofanya. Wakikukopesha riba yamkopo wao wa Shilingi milioni 30, ni Shilingi milioni mbili labda, lakini mkopo ule ni wa miaka mitano. Shilingi milioni mbili ni kwa mkopo mzima, ni interest. Miaka mitano huyo mkulima kama ali-delay hapa katikati kulipa, utakuta interest ni Shilingi milioni 15.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaweza ukashangaa, interest ya principal nzima ni Shilingi milioni mbili, interest ya kuchelewesha ni Shilingi milioni 15. Mkulima huyo unayemkopesha ni mkulima ambaye anakopa kwa kilimo cha kutegemea mvua. Matarajio yangu ni kwamba, kabla hujamwekea interest na kabla hujaenda kutangaza kutaka kuuza mali yake, umemtembelea, umeona mwaka huu ali-plan kupata gunia 100 hajapata, umefika pale umegundua kwamba hana sababu ya kutokurejesha, ni kilimo cha hali ya hewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajaribu kufanya mabadiliko sasa hivi, mapinduzi makubwa ya kwenda kwenye Irrigation Scheme, lakini asilimia 95 ya wakulima wanategemea mvua ya Mungu. Sasa wewe unanikopesha mimi kwa mkataba wa mvua ya Mungu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Malizia.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: …mazao sikupata, unanipiga fine. Mimi nikanunue mvua wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mheshimiwa Waziri hawezi kufumua Agricultural Trust Input Fund, wanapoteza fedha za Serikali. Ni bora mwapeleke huko wakawe Mabwana Shamba au vinginevyo, hakuna kazi wanayoifanya kwa sababu hawam… (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Kanyasu.