Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie. Mheshimiwa Waziri anajua kwamba Bunda tunalima pamba na kuna ginnery za pamba Bunda zimekufa. Wananchi wa Bunda wana stress kwenye mbegu, stress kwenye masoko, stress kwenye ginnery ambazo zilikuwa zinatengeneza ajira kwa vijana wengi wa Bunda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyozungumza Mheshimiwa Waziri maghala 24 ya kuuzia pamba na kuhifadhia yako kwenye hali mbaya. Mheshimiwa Waziri Misisi, Sazila, Mlimani Ligamba, Mheme, Taramanka, Balili, Kunzugu, Bukole, Mihale, Nyamatoke, Changuge, Jembemali, Mchalo, Jitume, Kisangwa, Tairo, Guta, Ibiti, Kunanga, Rwagu, Nyamilila, Kabasa, Kamkenga, Kalisumu, Bitaraguro, Kagetutya, Lindala, Kiwasi na Bunda Store; hizi zote zina hali mbaya. Pamba itaenda kuuziwa wapi? Itaenda kuhifadhiwa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kaka yangu Mheshimiwa Bashe najua ni mchapakazi, ametoka kwenye maeneo yanalima pamba. Wananchi wa Bunda baada ya kuona hivi, wanataka kujua Serikali mtakarabati lini haya maghala wanusuru kilimo hiki cha pamba ambacho ni kilimo ambacho kinachowasaidia wananchi wa Kanda ya Ziwa? Wananchi wa Mkoa wa Mara, wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuona kuna tatizo hili, wananchi wa Bunda wamejiongeza, wanaanza kulima alizeti. Hivi ninavyozungumza, Mheshimiwa Waziri wametenga hekta 10,000 kwa ajili ya kilimo cha alizeti, lakini hamjawapelekea mbegu. Sisi pale Bunda tunahitaji tani 30 tu za kuanzia na wamepanga kuvuna kilo 4,000,000 za alizeti ambazo watakuwa na uwezo wa kuzalisha mafuta lita 1,080,000. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa huku wameshindwa kujikamua, wamejiongeza kwenda kwenye alizeti, tena kwenye Kata ya Guta, Kabasa, Sazila, Waliku, Mcharo na Kunzugu. Naomba sana tupelekee mbegu. Kule Maafisa Ugani wako tayari, hata kama wengine wa pale Mji wa Bunda mnawachelewesha kuwapandisha madaraja. Sijui tumeelewana kaka yangu Mheshimiwa Bashe! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huku mtukarabatie maghala, lakini huku kwenye alizeti tunaomba mbegu. Tuna target ya kuvuna lita 1,080,000 za mafuta. Kwa hiyo, tunaomba sana Mheshimiwa Bashe…. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)