Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Kilimo

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi ya kuchangia Wizara ya Kilimo. Kwanza niishukuru Wizara kwa kupitia Waziri wake Mheshimiwa Bashe na wenzake wote na Mavunde wanafanyakazi nzuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu ni moja tu, jana nimesikiliza Ufaransa, wanasema Waziri Mkuu waliyopewa Ufaransa baada ya Emmanuel Macron kushinda ni mwanamke. Kwa hiyo, wenzetu nao wanaanza kuiga nchi za kiafrika kama Tanzania, kwamba akina mama wanafaa kushika uongozi wa ngazi ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini dhana yangu hapa nataka kuzunguza ni kitu kimoja tu kwamba, kilichompa uongozi wa uwaziri mkuu ni kwamba alipokuwa Waziri wa Kazi aliongeza ajira za kutosha Ufaransa. Sasa kwa nini, kwa sababu nchi za wenzetu ukimpa Waziri kazi unamuamini na unampa full mandate ya kufanya kazi hiyo. Mama Samia amekuja kwenye nchi yetu amewapa mawaziri wetu madaraka yote wafanye. Leo nchi yetu ikifeli kwenye kilimo; na ni wazo tu, kuna Waziri mmoja alikuwa anazungumza hapa juzi, akasema “akili ya afya”; alikuwa anazungumza Mbunge mmoja, sahani siyo Waziri; Mbunge mmoja, Balozi, anasema akili ya afya Watanzania inafanya tunakuwa masikini. Waheshimiwa Wabunge tumuachie Mheshimiwa Bashe na watu wake na Mheshimiwa Mavunde na watu wake. Kwa sababu wana uwezo wa kuonesha wana uwezo wa kufanya kazi tuwaachie madaraka yote wafanye tuone. Tumuulize Bashe wizara kwenye bajeti ijayo kitu gani kitafanyika?

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

TAARIFA

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, taarifa yangu ni fupi tu, kaka yangu Mwita pale anachangia anasema “akili ya afya” ni “afya ya akili” siyo “akili ya afya”. (Makofi/Vicheko)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Getere.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ni dada yangu ni Kiswahili na mimi Kiswahili sikijui, namshukuru tuendelee. Kwa hiyo, niombe tuwape mandate ya kutosha. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kuzungumza jambo moja kubwa sana. Waziri Bashe atuambie atakapokuja hapa, ni mikakati gani ataweka ili kuokoa ushirika nchini? Ushirika wetu umeyumba kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, dhana ya kuwepo kwa ushirika nchini ni nzuri sana, lakini ushirika wenyewe umekuwa na uwezo wa kutosha. Ni kitu gani anafanya, ni sheria gani atatumia, ni kanuni gani atatumia, kama ni kanuni ndogo au kanuni kubwa, ni utaratibu gani atatumia kupunguza wezi wa mali za ushirika nchini? Atuambie mikakati yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimshukuru Mheshimiwa Bashe Mheshimiwa Rais wameleta Pikipiki 7,000. Niwaombe sasa, hizo pikipiki 7,000 basi akazifungie GPS. Pikipiki ukipeleka huko mtu anaishi Bunda, pikipiki inakaa Bariadi; mtu anaishi Tanga pikipiki inakaa Pwani. Pikipiki zetu zimekuwa za kutembeza kama bodaboda zifungieni GPS ili watu wajulikane wapo wapi, wanafanya kazi gani, wanafuatilia nini nadhani hili litakuwa jambo zuri sana kuwadhibiti wale maafisa ugani ambao umewapa nafasi ya kuhudumia wakulima…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana kwa mchango mzuri.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.