Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi leo kuchangia katika bajeti hii ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yangu Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazozifanya kwa kuwatumikia wananchi wake wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nampongeza Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi kwa kazi nzuri naye anazozifanya kule Zanzibar. Pia naipongeza Wizara hii ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi hoja yangu kuhusu vijana wanaokwenda JKT. Pamoja na kuwafunza uzalendo na mambo mbalimbali, niiombe Serikali iongezewe fedha Wizara hii ili iweze kuwaajiri vijana hawa katika vitengo mbalimbali. Tukifanya hivyo, tutaweza kuwanusuru vijana hawa wasirudi mitaani bila ya kuwa na shughuli rasmi ya kufanya, kwa kuwa vijana hawa wameshafundishwa hadi kushika silaha.

Mheshimiwa Spika, hoja yangu ya pili, Mheshimiwa Waziri unapokuja hapa kujibu hoja ya bajeti yako, uniambie Serikali imefikia wapi kuhusu ujenzi wa jengo la Wizara ya Ulinzi ndani ya Zanzibar. Pia kuhusu majengo ya Hospitali ya Bububu kwa ajili ya faragha ya viongozi wetu wa Kitaifa pale wanapoumwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa haya machache naunga mkono hoja. (Makofi)